Hebu tupumzisheni kidogo tafadhali

Hebu tupumzisheni kidogo tafadhali

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
371,548
Reaction score
860,660
Kama Imethibitishwa kuwa kuna watumishi elfu arobaini waliogushi umri, mnafanya uhakiki wa nini tena. Sio kwa vituko hivi!

Tunajua kizungumkuti kilichotokea kwenye kusaka watumishi hewa, halafu likafuatia zoezi lenye makengeza mengi la walioghushi vyeti... Zoezi hili lilifeli vibaya kwakuwa kuna maeneo hawakuthubutu kuyagusa kabisa huku baadhi ya watumishi wakiachwa ilihali wamethibitika kughushi.

Haya ya kupandishwa mshahara tuyaache kama yalivyo lakini hili la KUHAKIKI UMRI..... HAPANA si la kukalia kimya!

Umetumika mtambo gani huo kung'amua hili? Hili zoezi limechukua muda gani? Kwahiyo sio watumishi hewa na hawajaghushi vyeti ila wameghushi UMRI.... na mnataka kufanya uhakiki tena! Wa nini sasa wakati tayari mna takwimu zake?

OK huu uhakiki utachukua muda gani? Mnaua morali wa kazi kwa watumishi kwa kasi kubwa mno halafu bila sababu za msingi... Kwa hali hii tusitegemee matokeo makubwa yenye ufanisi huko serikalini... Maana watumishi wa uma wamekuwa kama vibaka....!!! Kibaka ni mtu wa kusingiziwa kila kitu.

Nina wasiwasi zoezi la kuhakiki umri likiisha litafuata la kuhakiki nyeti/jinsia... Hili litafanyika 2018, halafu 2019 litakuja la kuhakiki makabila na rangi..

Tupumzisheni kidogo tuwaze mengine sasa.. Hizi hakiki zimetukifu pomoni..
 
Nchi imekabidhiwa kwa Washamba na Malimbukeni.

Ivi Viongozi wetu ambao wengi wao ni Maprofesa na Madokta ndio wana akili za namna hii?
Mbona wanafanya vitu bila kufikiria!!

Kwa hili wanatutonesha vidonda ambayo vilianza kukauka, sasa makovu yametujaa, ni wakati sasa wa kusema basiii.
 
Watanzania mtajuta sana kwa kufanya uchaguzi usio sahihi
FB_IMG_1504503412971.jpg
 
Hili la kughushi umri kwangu mimi nipo tayari hata kama sio Kweli maana nataka nilipwe haki zangu nirudi kijijini, hili halihitaji uhakiki, wao watangaze tu kuwa anayetaka kustaafu hata kama hajafikia umri wa kustaafu mbona tutajitokeza wengi kuliko hao elfu arobaini
 
Hili la kughushi umri kwangu mimi nipo tayari hata kama sio Kweli maana nataka nilipwe haki zangu nirudi kijijini, hili halihitaji uhakiki, wao watangaze tu kuwa anayetaka kustaafu hata kama hajafikia umri wa kustaafu mbona tutajitokeza wengi kuliko hao elfu arobaini
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji144] [emoji144] [emoji144] [emoji144]
 
Hili la kughushi umri kwangu mimi nipo tayari hata kama sio Kweli maana nataka nilipwe haki zangu nirudi kijijini, hili halihitaji uhakiki, wao watangaze tu kuwa anayetaka kustaafu hata kama hajafikia umri wa kustaafu mbona tutajitokeza wengi kuliko hao elfu arobaini
Endapo akisema hivyo hautapata stahiki yako.

Maana utaambiwa umeamua mwenyewe kabla ya muda
 
Nimebaki tu nacheka nikitafsiri hayo maneno na kile kitendo cha kungonoka[emoji85] [emoji85] [emoji85] [emoji123] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Baadaye utafuata uhakiki wa watoto na vyeti vya ndoa kwamba mfanyakazi anapohamishwa kituo chake cha kazi analipwa hela za watoto wanne na mke wake wakati mke wa ndoa walitengana naye na alikuwa na watoto wawili tu, huko ndiko tunakoelekea
 
Back
Top Bottom