Hebu tumkwamue huyu dogo

Hebu tumkwamue huyu dogo

Aachane na habari ya advance
"kutoka Moshi kwenda Dar utapitia ya Segera Chalinze sio Arusha Babati Singida Dodoma then Chalinze ni ya mbali......mpeleke pale DIT akapige Diploma ya Mechanical,Electrical Engineering bàada ya miaka 3 ameshakuwa engineer
 
Mkuu, Dogo kwa ufaulu huo amejitahidi sana.Ila kwakuwa now umri umeenda kidogo simshauri arudi akasome A-Level anaweza kwenda chuo moja kwa moja tena kwa course za maana.

Ila simshauri asomee mambo ya Accounting and Finance atakuja lia uko mbele. Maana hiyo course ina utitili wa watu wengi sana.

Me namshauli aje kucheki course yoyote hapa Ardhi university, Au laah! Basi acheki course za Afya zinalipa mkuu.
 
A level nafasi atapata shule za private. matokeo yake mazuri sana hayo. kama vipi hizo accountancy na finance anaweza kuzisoma hata sasa kwa level ya certificate halafu akaunga diploma had degree.
hata hivyo ni vema kusoma kitu kitakacho mpa ujuzi na maarifa ya kujiajiri
 
Anaweza kuapply as private candidate kama bado anahisi anaweza kumudu masomo
 
Aende vyuo vya ufundi au afya kwanza kusoma sana ni kupoteza muda.
 
Kaa uongee naye vizuri....EGM kwa pass zake atapata shule za private...ila akiweza kusoma diploma itakuwa bora zaidi
 
~~>Ukiwa na walau C 5 kwa K.4 unaweza kusomea Diploma... Hivyo huyo anaweza kusoma Diploma ya kitu chochote kwa miaka mitatu.


Mpeleke DIT, Mist ama Arusha Tech asome FTC kqa miaka mitatu

Akimaliza hapo anaunga Degree
 
Wakuu wataalam wangu nashukuruni kwa ushauri wenu mzuri.
Naombeni mnifumbue kidogo kuhusu kozi nzuri za kusomea chuoni ambazo naweza kumshauri dogo endapo atapitia diploma. Pia mwenye link za kuview anaweza kutupia
 
Mpeleke DIT akapige kozi yeyote ya engineering au Unclas au vyuo vya afya km pale Tumbi hospitali kibaha kipo,diploma yeyote ni 3yrz usisahau.Uhasibu siku izi unasomwa sana wengi saana na CPA(T) kibao hawana kazi zakueleweka kiivyo.
 
Naomba mwenye ufahamu wa kuhusu kozi nzuri za engineering hapa nchini kwa maana ya fursa za ajira au kujiajiri. Mnivumilie wakuu.
 
Pia mwenye kujua kozi za afya zilizopo hapa Tanzania. Naomba anijuze ili tumsaidie mdogo wetu. Asanteni
 
##Electrical,Electronic and Telecom Engineering, ##Mechanical Engineering ,.....Computer Engineering zote hizo ni hot cake kwa sasa hapa TZ hasa Telecom inalipa na akipata kazi mbona atasahau shida maana zina mishahara minono
 
Ushauri wa bure kwa ufaulu huo anaweza akarudia akafeli zaidi angewasiliana na vyuo husika ili wamfafanulie.
 
Back
Top Bottom