Nimeshtushwa na habari iliyo katika Mwanahalisi ya Leo Toleo namba 249 yenye Kichwa "Mzozo wa Lowassa na Pinda: Ni uamuzi Mgumu, Utapeli au ajali ya kisiasa?" Ukurasa wa 11. Nanukuu baadhi ya vifungu:-
"Baada ya kusomwa kwa ripoti , (Ya Richmond) taarifa zinasema Lowassa alikwenda Chamwino kuonana na bosi wake ili kupanga mkakati wa kuzima maasi ya wabunge wa CCM waliokuwa wamesisimka ili kummaliza Lowassa, rais Kikwete na serikali yao. Katika mazungumzo yao usiku ule, Rais Kikwete na swahiba wake huyo wa zamani-Edward Lowassa-walipima upepo na kuona pendekezo la Lowassa kuwa rais aende upesi kukutana na wabunge wa CCM ili kuwaonya wasiiangushe serikali yao, lilionekana halifai kwa hofu ya mihimili hiyo miwili kuingiliana. Ndipo mpango ukasukwa kuwa Lowassa aandike barua ya kujiuzuru, lakini rais AICHELEWESHE kuijibu na Bunge liahirishwe ili kumpa nafasi rais kuonana na wabunge wa CCM ili kuzima maasi ya wabunge kabla ya mkutano mwingine wa Bunge wa April haujafanyika."
"Mpango ukakubaliwa na bila ajizi Edward Lowassa aliamini na kuandika barua ya "KUIGIZA" kujiuzuru na kisha akaondoka kurudi Dodoma mjini usiku ule. Yaliyotokea Chamwino baada ya Lowassa kuondoka inabakia kuwa siri ya Kikwete mwenyewe na aliokutana nao."
"Baada ya kusomwa kwa ripoti , (Ya Richmond) taarifa zinasema Lowassa alikwenda Chamwino kuonana na bosi wake ili kupanga mkakati wa kuzima maasi ya wabunge wa CCM waliokuwa wamesisimka ili kummaliza Lowassa, rais Kikwete na serikali yao. Katika mazungumzo yao usiku ule, Rais Kikwete na swahiba wake huyo wa zamani-Edward Lowassa-walipima upepo na kuona pendekezo la Lowassa kuwa rais aende upesi kukutana na wabunge wa CCM ili kuwaonya wasiiangushe serikali yao, lilionekana halifai kwa hofu ya mihimili hiyo miwili kuingiliana. Ndipo mpango ukasukwa kuwa Lowassa aandike barua ya kujiuzuru, lakini rais AICHELEWESHE kuijibu na Bunge liahirishwe ili kumpa nafasi rais kuonana na wabunge wa CCM ili kuzima maasi ya wabunge kabla ya mkutano mwingine wa Bunge wa April haujafanyika."
"Mpango ukakubaliwa na bila ajizi Edward Lowassa aliamini na kuandika barua ya "KUIGIZA" kujiuzuru na kisha akaondoka kurudi Dodoma mjini usiku ule. Yaliyotokea Chamwino baada ya Lowassa kuondoka inabakia kuwa siri ya Kikwete mwenyewe na aliokutana nao."