Haya ni mapenzi?

Oct 14, 2015
6
12
Habari za jumapili wadau, ni matumaini yangu mko poa nyote, to cut the long story short ni ivi, miaka miwili nyuma nilitokea kumpenda msichana mmoja mrembo sana, alikua ni msichana wa kisasa nikimaanisha alikua anapelekwa na matukio ya dunia kuparty sana, kunywa pombe,kuvaa mini skirts n.k lakini mbali na mapungufu yote hayo nilimpenda, kasheshe likaja kwenda kumtambulisha kwa wazazi, walimkataa baada ya kumuona, nililia sanaa maana G alikuwa ameuteka moyo wangu na sikuweza kumuona mwanamke mwingine kabisa.

Nikafanya ivi, niliwapuuzia wazazi wangu nikamuoa kwa nguvu, siku ya harusi Mama yangu alinipigia simu na kuniasa nisienda kufunga pingu za maisha kwani ndo utakua mwisho wa maisha yangu, nilipuuzia nikamuoa G

Wazazi walikua hawaji kutusalimia, Japo maisha yetu na G yalikuwa matamu sana, nilianza kumbadilisha G, niliacha kunywa pombe na yeye baada ya muda akaacha baada ya kukosa kampani ya ulevi, nilikua nikimnunulia nguo za heshima, automatically akaachana na zile nguo zake za kutembea nusu utupu.

Sasa ivi niko kwenye process ya kumpatanisha na familia yangu waweze kumpenda.

Kuna muda huwa nawaza haya mahusiano yasio na baraka za Mungu wangu wa pili (wazazi) yatatoboa kweli?. Kiukweli nampenda sana G licha ya mapungufu yake mengi.

Ivi huu ni ukosefu wa akili au niko sawa?
 
Wazazi wako wanaona mbali ndiyo maana hawamtaki huyo demu, believe it or not. Ni vigumu sana ukaja kuishi kwa raha na mwanamke au mwanamme ambaye wazazi hawamtaki, huyo mwanamke kama ana asili ya uchangu itakuwa vigumu sana kwako kuishi naye kwa amani. Kumbuka kuwa mgawaji ni mgawaji tu.....usijipe mateso ya moyo kijana.
 
Watamkubali hakikisha unambadilisha zaidi.huyo ndo chaguo lako, ndo anakupa furaha. Kuna siku wazazi watakupa baraka. Wala usitishike.binadamu anabadilika kutokana na mazingira.
 
Inaonekana huyo G wako ni mfumo wa maisha fulani ulimbadilisha lakini anaonekana ni mtu kwa kubadilika bila malumbano(kulingana na mwandiko wako).

Cha kufanya,tengeneza ukaribu wa yeye na wazazi wako ili wapate imani nae..matendo mazuri ni hazina...hakikisha mkiwa mnaenda kwa wazazi awe anavaa kiheshima tu Haitompunguzia kitu itamuongezea thamani.

Hakuna Baraka kwenye nyumba ambayo wazazi wako hawajaibariki.

Hakuna binadamu mkamilifu,mapungufu tumeumbiwa sisi gud thing ni kwamba G anaonekana yuko tayar kubadilika.ni muda tu taratibu mambo yatakaa sawa.

Afanye sehemu yake kama mwanadamu mengine amwachie Mungu atarekebisha taratibu.

A jitahidi kuwa karibu na mama ili kumletea imani katika familia.asiache kuwapelekea zawadi mnapoenda kuwaona wazazi.akifika nyumbani kwa wazazi ajichanganye kama mwanamke na sio kukaa tu amening’iniza mikucha kama ngiri akisubiria kila kitu afanyiwe.

Mungu awatangulie nyote wawili upendo kwa pande zote mbili utawale
 
Inaonekana huyo G wako ni mfumo wa maisha fulani ulimbadilisha lakini anaonekana ni mtu kwa kubadilika bila malumbano(kulingana na mwandiko wako).

Cha kufanya,tengeneza ukaribu wa yeye na wazazi wako ili wapate imani nae..matendo mazuri ni hazina...hakikisha mkiwa mnaenda kwa wazazi awe anavaa kiheshima tu Haitompunguzia kitu itamuongezea thamani.

Hakuna Baraka kwenye nyumba ambayo wazazi wako hawajaibariki.

Hakuna binadamu mkamilifu,mapungufu tumeumbiwa sisi gud thing ni kwamba G anaonekana yuko tayar kubadilika.ni muda tu taratibu mambo yatakaa sawa.

Afanye sehemu yake kama mwanadamu mengine amwachie Mungu atarekebisha taratibu.

A jitahidi kuwa karibu na mama ili kumletea imani katika familia.asiache kuwapelekea zawadi mnapoenda kuwaona wazazi.akifika nyumbani kwa wazazi ajichanganye kama mwanamke na sio kukaa tu amening’iniza mikucha kama ngiri akisubiria kila kitu afanyiwe.

Mungu awatangulie nyote wawili upendo kwa pande zote mbili utawale
Best advice ever
 
Inaonekana huyo G wako ni mfumo wa maisha fulani ulimbadilisha lakini anaonekana ni mtu kwa kubadilika bila malumbano(kulingana na mwandiko wako).

Cha kufanya,tengeneza ukaribu wa yeye na wazazi wako ili wapate imani nae..matendo mazuri ni hazina...hakikisha mkiwa mnaenda kwa wazazi awe anavaa kiheshima tu Haitompunguzia kitu itamuongezea thamani.

Hakuna Baraka kwenye nyumba ambayo wazazi wako hawajaibariki.

Hakuna binadamu mkamilifu,mapungufu tumeumbiwa sisi gud thing ni kwamba G anaonekana yuko tayar kubadilika.ni muda tu taratibu mambo yatakaa sawa.

Afanye sehemu yake kama mwanadamu mengine amwachie Mungu atarekebisha taratibu.

A jitahidi kuwa karibu na mama ili kumletea imani katika familia.asiache kuwapelekea zawadi mnapoenda kuwaona wazazi.akifika nyumbani kwa wazazi ajichanganye kama mwanamke na sio kukaa tu amening’iniza mikucha kama ngiri akisubiria kila kitu afanyiwe.

Mungu awatangulie nyote wawili upendo kwa pande zote mbili utawale
Kunguru afugiki
 
Kunguru afugiki
Ni bora shetani unaemjua kuliko malaika usiyemjua.

Hata shetani alikuwa ni malaika lakini akabadilika.

Ni vipi huyo G asibadilike wakati ni binadamu?au nijiwe asiweze kubadilika.

Kwa upande wangu naona ni bora mleta uzi kajua mapungufu yako wapi na ameshaanza kuyafanyia kazi.
 
Hii inaitwa uzi juu ya uzi!
Inaonekana huyo G wako ni mfumo wa maisha fulani ulimbadilisha lakini anaonekana ni mtu kwa kubadilika bila malumbano(kulingana na mwandiko wako).

Cha kufanya,tengeneza ukaribu wa yeye na wazazi wako ili wapate imani nae..matendo mazuri ni hazina...hakikisha mkiwa mnaenda kwa wazazi awe anavaa kiheshima tu Haitompunguzia kitu itamuongezea thamani.

Hakuna Baraka kwenye nyumba ambayo wazazi wako hawajaibariki.

Hakuna binadamu mkamilifu,mapungufu tumeumbiwa sisi gud thing ni kwamba G anaonekana yuko tayar kubadilika.ni muda tu taratibu mambo yatakaa sawa.

Afanye sehemu yake kama mwanadamu mengine amwachie Mungu atarekebisha taratibu.

A jitahidi kuwa karibu na mama ili kumletea imani katika familia.asiache kuwapelekea zawadi mnapoenda kuwaona wazazi.akifika nyumbani kwa wazazi ajichanganye kama mwanamke na sio kukaa tu amening’iniza mikucha kama ngiri akisubiria kila kitu afanyiwe.

Mungu awatangulie nyote wawili upendo kwa pande zote mbili utawale
 
Back
Top Bottom