Tuna tatizo kubwa, baadhi yetu, katika kuangalia mambo na kuyaelewa. Uhusiano wa kimapenzi una mapana na marefu yake; maana halisi ya mapenzi inatofautiana sana baina ya jozi za wapendanao; na mambo gani yanawafanya wapenzi wawe kwenye mapenzi yanatofautiana sana.
Tofauti hii ya mitazamo ndiyo huwa inaleta kutokuelewana baina ya watu; wazazi na wakwe zao; madada na wifi zao; makaka na shemeji zao; majirani, ndugu na jamaa kama mleta mada hii.
Yote haya yanatokea kwa sababu tunajaribu kufananisha mapenzi yetu sisi wawili, na yale ya wengine...kwa kufanya hivi, ni sawa na kuona mke wako ni mzuri kuliko wa wengine...ilhali unajua kabisa vionjo vyako si lazima viwe sawa na vya wengine, na kwamba mkeo hata kama ni mzuri namna gani, huo ni uzuri unaokufaa wewe tu. Sana Sana wengine wanaweza kuona ni mzuri kwa kazi fulani tu, na kwamba baada ya hapo ataendelea kukufaa wewe mwenyewe.
Kwa sababu niliziainisha hapo juu, ni vigumu sana kuyaelewa mapenzi ya huyo bwana anayeelezewa kwenye mada hii. Sana sana wengi wetu tutaishia kumkashifu tu; jambo ambalo halitakuwa sahihi. Mipango ya ndani ya nyumba, haifanani, na kama ni shughuli za ndani, hizi ni "socially learnt activities" ambazo hubadilika from time to time, na kutegemea mazingira halisi.
Wakati Tanzania ni nadra sana, na huwa gumzo anapoonekana mwanamama anaendesha lori, nchi kama Ubelgiji, Japan, Uholanzi nimeona wanawake wanaendesha trucks na ni jambo la kawaida. Kwa mtoa mada, pengine itaonekana hii ni kazi ya kiume na hawapaswi kufanya hivyo?
Masuala ya kazi sasa hivi hayafuati sana jinsia...yanabadilika haraka kutokana na hali halisi. Kwetu, Tanzania, kwa sababu ya society sensitivity ndiyo maana maendeleo katika eneo hili yanachelewa sana. Hawa akina dada wanaojiuza, kwa mfano, kwa sababu hawaoni cha kufanya zaidi ya hicho, wangeweza kuwa drivers kwenye taasisi nyingi tu...na masiaha yangekuwa bora zaidi. Taasisi nyingi za UN zinahimiza akina mama drivers.
Tubadilike. Sidhani kama tuna taarifa muhimu za kutosha kujadili anayoyafanya huyo jirani yako. Tutakuwa tunapoteza muda tu kwenye jambo tusilolijua. Mapenzi yana siri sana ndugu zangu, hayaishii kufuliana na kushikana mikono tu hadharani. Na, kama haikudhuru wewe, na hakuna sheria zinazovunjwa, na hasa kama mkewe ameridhia, na wanawe, ni vema tumuache. Vinginevyo, tutaonekana kama tunamuonea wivu huyo mama...