Dogo amejitahidi kuelezea upande wake,mwingine mwenye upeo mkubwa,amwage data hapa,
Mi Nina swali wakuu,wale wanaomlinda rahisi,ni askari wa kawaida tu,waliohamishwa vitengo wakapewa mafunzo maalum,ni jwatz,ni makomandoo,ni jkt,
Au kuna sehemu maalum wanapelekwa kujifunza.
Unapojibu hili,tilia maanani,wale usalama wa taiga,walioenda kumkamata mfanyabiashara wa msoma,Zakaria,wakaishia kutwangwa risasi,kama hawa jamaa wana mafunzo maalum,ilikuwaje watu saba wakazidiwa na MTU tena RAIA mmoja.
Miaka kadhaa nirikuwa kwenye mishe kahama,nikaibiwa tairi ya gari,nikaripoti ofisi ya mtaa,nikapewa vijana ambaye amepitia jkt,wakati huo ameajiriwa kama sungusungu,akaniambia nimuelezee tairi yangu inafananaje,
Akaniambia kama imeuzwa kahama stendi,ataiona tu,akaenda kituo cha mabasi madogo,akakagua kila hiace inayoingia,SAA tatu baadae,tairi ikapatikana,
Sasa Kama JKT anauwezo huo,niambieni uwezo wa hawa wa usalama wa taifa