Hawakumaanisha walichokisema

Hawakumaanisha walichokisema

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,207
Reaction score
829,193
1475783949584.jpg

Kuna mahali zamani sana nyumbani kwa ndugu yangu niliona picha ya simba yenye maneno haya NO POLITIC yaani kwa kinyasa hakuna siasa.

Kuna kipindi katika maisha yangu nilivutiwa na siasa wakati ule wa chipukizi na skauti ilikuwa mwaka 1983! Nilikolezwa nikakolea, nikawa na ndoto nyingi...hasa kuwa mwanasiasa mahiri!!!

Sisi kama nchi hatukuwa na uwezo wa kutengeneza gari zetu wenyewe hivyo kama nchi tukaingia mkataba na waingereza kutuuzia magari yao serikalini!

Huu ulikuwa ni mkataba rasmi na ndio maana kipindi chote cha mwalimu Nyerere tulitumia magari ya muingereza Landrover Range rover nk.

Mzee Mwinyi aliposhika hatamu mwaka 1985 akaamua kuvunja mkataba na waingereza na kuingia mkataba mpya rasmi na wajapani wakati huo waziri mkuu akiwa Mzee John Samwel Malecela na naibu wake akiwa ndugu Edward Ngoyai Lowassa.

Mkataba huu ulimaliza kipindi cha magari ya uingereza kutamba nchini na nchi ikaanza rasmi kutumia magari ya kijapani maarufu kama land cruiser, huu ni mradi mmoja mkubwa sana wa mabilioni ya dola!

Wajapani kwa Shukrani yao kwenye hili wakaanza kutuletea magari makuukuu kwa bei poa wakati ule kama jaba na vile vile kutufumba mdomo na kutuziba macho kwa misaada mbalimbali kama KAJIMA KOIKA ya sasa nk nk

Ni takriban miaka zaidi ya 30 sasa tunatumia magari ya kijapani, mapya na chakavu, tafsiri yake ni kwamba mpaka vipuri nk ni vya kwao, ukija kuangalia kwa jicho angavu wajapani wamefaidika na sisi zaidi kuliko sisi tulivyofaidika nao..hawawezi kirahisi tu kukubali watupoteze!

Kwenye duru za siasa serikali ikaanza kupigiwa kelele kuhusu kutumia magari ya gharama kubwa bila sababu! Hii ikawa ni kama mtaji wa kisiasa, na joto lilipozidi watu ili wapate kura wakaanza kutoa ahadi za kutonunua hayo magari tena.

Sensa zikafanyika na baadhi yakaanza kurudishwa serikali kuu ikiwa ni maandalizi ya kuacha kuyatumia! Ilikuwa ni hatua moja mbele muhimu sana kisiasa kuna waziri mmoja wa ujenzi akajizolea umaarufu kwenye hili....!

Alichosahau ni kimoja kwamba hivi vitu vina mikataba rasmi kuwa ili upate msaada fulani inabidi kila mwaka wa fedha uagize toka kwao si chini ya magari kadhaa.

Leo hii pamoja na kelele zote zile ndio kwanza ma land cruiser ya ukweli na new model yanabanana serikalini na wizara na vitengo vyake.

Ukitaka kufanikiwa kwenye lolote maanisha unachokinena na nena unachomaanisha.

Si kila kitu ni matamko ya kisiasa majukwaani, kuna mikataba rasmi kama yale magorofa ya mabepari zikipokuwa ofisi za umoja wa vijana.
1475785680983.jpg


ALAMSIKI.....!!!!
 
View attachment 413574Kuna mahali zamani sana nyumbani kwa ndugu yangu niliona picha ya simba yenye maneno haya NO POLITIC yaani kwa kinyasa hakuna siasa
Kuna kipindi katika maisha yangu nilivutiwa na siasa wakati ule wa chipukizi na skauti ilikuwa mwaka 1983! Nilikolezwa nikakolea, nikawa na ndoto nyingi...hasa kuwa mwanasiasa mahiri!!!

Sisi kama nchi hatukuwa na uwezo wa kutengeneza gari zetu wenyewe hivyo kama nchi tukaingia mkataba na waingereza kutuuzia magari yao serikalini! Huu ulikuwa ni mkataba rasmi na ndio maana kipindi chote cha mwalimu Nyerere tulitumia magari ya muingereza Landrover Range rover nk
Mzee Mwinyi aliposhika hatamu mwaka 1985 akaamua kuvunja mkataba na waingereza na kuingia mkataba mpya rasmi na wajapani wakati huo waziri mkuu akiwa Mzee John Samwel Malecela na naibu wake akiwa ndugu Edward Ngoyai Lowassa
Mkataba huu ulimaliza kipindi cha magari ya uingereza kutamba nchini na nchi ikaanza rasmi kutumia magari ya kijapani maarufu kama land cruiser, huu ni mradi mmoja mkubwa sana wa mabilioni ya dola!
Wajapani kwa Shukrani yao kwenye hili wakaanza kutuletea magari makuukuu kwa bei poa wakati ule kama jaba na vile vile kutufumba mdomo na kutuziba macho kwa misaada mbalimbali kama KAJIMA KOIKA ya sasa nk nk
Ni takriban miaka zaidi ya 30 sasa tunatumia magari ya kijapani, mapya na chakavu, tafsiri yake ni kwamba mpaka vipuri nk ni vya kwao, ukija kuangalia kwa jicho angavu wajapani wamefaidika na sisi zaidi kuliko sisi tulivyofaidika nao..hawawezi kirahisi tu kukubali watupoteze!

Kwenye duru za siasa serikali ikaanza kupigiwa kelele kuhusu kutumia magari ya gharama kubwa bila sababu! Hii ikawa ni kama mtaji wa kisiasa, na joto lilipozidi watu ili wapate kura wakaanza kutoa ahadi za kutonunua hayo magari tena
Sensa zikafanyika na baadhi yakaanza kurudishwa serikali kuu ikiwa ni maandalizi ya kuacha kuyatumia! Ilikuwa ni hatua moja mbele muhimu sana kisiasa kuna waziri mmoja wa ujenzi akajizolea umaarufu kwenye hili....! Alichosahau ni kimoja kwamba hivi vitu vina mikataba rasmi kuwa ili upate msaada fulani inabidi kila mwaka wa fedha uagize toka kwao si chini ya magari kadhaa .......

Leo hii pamoja na kelele zote zile ndio kwanza ma land cruiser ya ukweli na new model yanabanana serikalini na wizara na vitengo vyake....
Ukitaka kufanikiwa kwenye lolote maanisha unachokinena na nena unachomaanisha
Si kila kitu ni matamko ya kisiasa majukwaani, kuna mikataba rasmi kama yale magorofa ya mabepari zikipokuwa ofisi za umoja wa vijana
View attachment 413586

ALAMSIKI.....!!!!
Kusemakweli hizo ndiga ni tamuu Aisee. Ukipanda ndani kama hakuna kufa. Anyway hapa ndo inakuja ile dhama ya kuacha kuwa tegemezi ili kuwa huru kufanya mipango yako. Kama inafikia hatua ya kupewa hela mpaka ununue kwao ni sawa na utumwa
 
Kusemakweli hizo ndiga ni tamuu Aisee. Ukipanda ndani kama hakuna kufa. Anyway hapa ndo inakuja ile dhama ya kuacha kuwa tegemezi ili kuwa huru kufanya mipango yako. Kama inafikia hatua ya kupewa hela mpaka ununue kwao ni sawa na utumwa
Biashara matangazo unadhani zingekuwa kama hard top tungezishadadia kiasi hiki?
Kuna kosa moja kubwa sana tulilifanya hapo nyuma! Tuliipa siasa thamani kubwa isiyostahili leo ndio tunaona matokeo yake
 
Ila kwa lendkruza V8mjapani kacheza na ameuza si mchezo. Huko arabuni zimenunuliwa kama njugu. 83 thousands dollars unapata kitu V8 safi uingereza. V8, Hummer na renji are my dream cars. Ila nasikitika sitawahi kumiliki kwasabab nategemea tu kipato halali kwa kubeba boksi!

Maybe one day I can hit the jackpot in the lottery al keep on playing and buy tickets. Its the only journey of redemption.
 
....la kulia cake ya Taifa Mkuu, umesahau ukoo wa mapanya na mafisi Mkuu!? Hawa ndivyo walivyo Mkuu lazima watanue sana na kudai nchi yetu ni tajiri sana. Ukweli nchi yetu ni tajiri sana lakini utajiri wote unaishia mifukoni mwa wale wa ukoo wa mapanya na mafisi kwa njia zote haramu wazijuazo ikiwemo wizi, rushwa na ufisadi halafu wanaishia kujibaraguza tumechezewa mno! tumedanganywa mno! tumeibiwa mno! halafu wakishatoa kauli kama hii ya kujibaraguza hakuna hatua zozote zinazofuata ili kukomesha kabisa huku kuchezewa mno, kudanganywa mno na pia kuibiwa mno. Ukoo wa mapanya na mafisi katika ubora wao Mkuu.

RC Dar V8 la nini?
 
Ila kwa lendkruza V8mjapani kacheza na ameuza si mchezo. Huko arabuni zimenunuliwa kama njugu. 83 thousands dollars unapata kitu V8 safi uingereza. V8 Hummer bna renji are my dream cars. Ila nasikitika sitawahi kumiliki kwasabab nategemea tu kipato halali kwa kubeba boksi!

Maybe one day I can hit jackpot in the lottery al keep on playing and buying ticket. Its the only journey of redemption.
hahaaaa!!one day yes!!
 
unajua kitu flan mkuu mshana inasikitisha sana kuona nch maskin kama yetu ma SUVs yamezagaa mtaan its a nonsense showoff in a country where over 95% of its citizens are worried where the next meal will Come from.
Na guts za kusema watayauza yote kwakuwa serikali haitaki tena kuyatumia zimetoweka
 
Ila kwa lendkruza V8mjapani kacheza na ameuza si mchezo. Huko arabuni zimenunuliwa kama njugu. 83 thousands dollars unapata kitu V8 safi uingereza. V8 Hummer bna renji are my dream cars. Ila nasikitika sitawahi kumiliki kwasabab nategemea tu kipato halali kwa kubeba boksi!

Maybe one day I can hit jackpot in the lottery al keep on playing and buying ticket. Its the only journey of redemption.
Usikate tamaa, Leo unabeba box huwezi jua nini kifuatacho.
Kama hautaweza basi nitakupa japo lift maana na mimi nina ndoto kama hizo ila sijakata tamaa. Naamini nitaupata tu huo mkwanja hata kwa watu kuniingizia hela kwenye account yangu kwa lengo la kuzificha. Wakiingiza tu, nitaenda kuzi draw na kulinunua hilo...
 
Ila kwa lendkruza V8mjapani kacheza na ameuza si mchezo. Huko arabuni zimenunuliwa kama njugu. 83 thousands dollars unapata kitu V8 safi uingereza. V8 Hummer bna renji are my dream cars. Ila nasikitika sitawahi kumiliki kwasabab nategemea tu kipato halali kwa kubeba boksi!

Maybe one day I can hit jackpot in the lottery al keep on playing and buying ticket. Its the only journey of redemption.
Hahahaha inawezekana mkuu ukiamini na kupursue
 
Back
Top Bottom