Yegomasika
JF-Expert Member
- Mar 21, 2009
- 13,164
- 61,276
Du kweli Bongo tumetoka mbali CBS News pale USIS mi nikikuwa member mzuri sana, hivi kuna anaejua habari za Hilary Ndibalema?. Alikuwa mchezaji wa vijana Bulls enzi hizo!.mhhh sijui lakini kwa jinsi anavyoongea inaonekana alikuwa mjanja mnja huyu halaf si unajua wengine safari zao zilikuwa za kukamatiwa na hivyo hawakuhanithiwa na majitu kama akina aally mrisho au ule upuuzi wa kupelekana Tanga kwenye kambi za kujifunza kufunga kamba
we acha tuuu
anywa you never know lakini watakuja tuu hapa
ebwana hivi uliwahi kuwa member wa USIS katika miaka ya early 90's unajua tena amabo ya TV bongo ilikuwa bado huku Mohammed Farah Aideen alikuwa akipelekana puta na wanyamwezi kule somalia basi USIS walikuwa wanaonyesha 30 minutes video za CBS NEWS ...kama hupajui basi ni pale Tanganyika motors juu ...nadhani mwanakijiji atakuwa anapajua maana yule mwenezu ni mtu wa KLM!
Huyu Frank alikuwa na sister wake mmoja hivi kiboko sana, Carolyne nadhani alikuwa anasoma Kisutu huyu~hivi yupo wapi wajameni?.Ee bwana ee, Pundit si utani Henry yuko wapi siku hizi? Nakumbuka Mindu pale kwa kina Tasi na Bosi, jinsi Reggae na u-rasta tulivyokuwa tunau-mind na ndipo Justin Kalikawe(RIP) alipopata inspiration ya kuanza kuimba na kuwa dread... Mambo ya "Manhattan gym"... Chande naye yuko wapi? Marizanga aka Mario Kempes naye, Danny Mbotto, David Mswia aka Yellowman, Richard aka Ricardo, Maga Mix, Tony Ojjiki, Frankie Munuo, Gregory Msafiri, Chuche, Eliudi, duh! Sijui kama wengine tutakuja kuonana tena... Upande wa Seaview akina Tume, Job, the Luangisas from Peter, Samuel, Rose to Mao, Crispin(RIP), the Makotas, the Gundas, yaani the list goes on and on...
Dah hii thread imenikumbusha mbali sana
watoto wa Mjini utawajua tuu...thread imetazamwa na watu kibwena lakini wote wameingia mitini for simple reason walikuwa bado wako countryside wanawinda ndezi au walikuwa wako UD wanaandamana...na ni bora maana waatu tutajuana na tunaweza tukacheza santuri moja wale joni visomo wakija noma wataaanza na mamabo ohhh tunabaguliwa ohhh tulipanda meli ohh sijui nini yaani tabu tupu
Ebwana Rhymson nakumbuka alipata demu wa kijamaica ambaye ni mcanada na aliondoka naye lakini mara ya mwisho nilionyeshwa picha yake sikuamini jamaa naona ana kwenda kama YAAA'DI BWOY...au kuliko maana kawa mzee wa ROOTS
Ebwana hivi kati yenu nani alikuwa nakwenda GHRORFA ya SABA?PHP:
Topic hii ilianza vizuri lakini wameharibu walioanza kuingiza mambo ya shule, hapa tunaongelea Ma Mcs wa OldSkul wa Bongo,
Je nani anajua kwamba kulikuwa na Beef kati ya Salehe Jabir a.k.a Cool S na Adili Kumbuka The late Nigger One ( R.I.P) walishakutana fainali mara mbili Lang'ata kwenye mashindano ya Yo Rap Bonanza mara moja akshinda Nigger One mara ya pili Cool S hope so na nilikuwa nina tape ya mashindano hayo but so sorry kuna mtu alinizima
nigger One alikuwa anachana kiingereza sana na kishwahili kidogo nadhani hapa IST ilikuwa inachangia na alikuwa anamanda salehe kwa kuimba kiswahili na Salehe alikuwa mbaya kwenye kiswahili lakini alikuwa anacopy au anabadilisha nyimbo za wanamuziki wa nje kutoka kiingereza kuwa kiswahili. mfano nyimbo ya vanilla Ice, Black Box mfano ni mistari hiyo hapo chini;
....'Ice ice Baby nipo nipo na maprino invasion kitu kimenikaa moyoni na sasa naamua kukitoa mdomoni, werastop yoo I dont know kusema mengi naona choo, nipo kwenye steji nayakata madebe dance ngoma hii ya ajabu........ cassete ya Salehe jabir ninayo mpaka leo huwa naisikiliza na kucheka sana.
hizo verse kama ulikuwa hajazishika ilikuwa ngumu kuchukua totoz kwani ndio ulikuwa ujanja nakumbuka kuna mchizi primary madem walikuwa wanamfuata na kmwomba awashushie hiyo mistari yaani ilikuwa soooo.
Kitu kingine wadau wa Old Skul kulikuwa kuna dada mmoja tu ndio alikuwa anashika kipaza kitambo hicho naye alikuwa anaitwa Tass alikuwa anasoma IST huyu alikuwa anashiriki Yo Rap Bonanza alikuwa anakaa mitaa ya Obay.
All in all kulikuwa na wakali wengine kibao kama wakina Mc Cux, Dj Cux, fresh XE, ...... HiPhop was hot those days sio sasa wabana pua wengi
Ebwana unakumbuka enzi za PUZA WA TAMBAZA?
what about mamabo ya DON BOSCO tournament?
Hapo kwenye red, dahhh Don Bosco Zanaki na Tambaza
enzi za aaah msela mimi nampenda msela ingawa hana hela msela aaaaah msela
mmmmmh mselaaa.
Hayo makundi yaliibuka mika ya 90,miaka ya 80 tulikuwa hatujui hizo nyimbo zenu za ubongo wa fleva,tulikuwa tuna ruka debe mbowe,ushirika 1900,TKU DISCO rungwe,
hahaaaah wakati huu mimi nilikua Mwalimu wa pale Alharamain Muslim Seminary , Jamaa walinipa kibarua kwakua nilikua Muislamu na nilikua na Div 1 ya Azania, nakumbuka hicho kijiwe, umenichekesha sana, hakika miaka inakwenda kasi, ila hii post imenichekesa, kunikumbusha na kunifunza mengi.Ukienda KAriakoo basi unamkuta JK, Ditto na RO pale Saigon au kwenye ile baa ya mtaa wa Nkurumah kwa mzee Makange.
Bado uko Bongo? Kuna tukio hili la kukumbushana mbali - nasikia kutakua na hadi shindano la breki dansi:
WATOTO WA CHUO (UDSM) BOTRO BBQ Welcome to Facebook
Sunday, December 5 · 2:00pm - 8:00pm
LocationUDSM-VIWANJA INFRONT OF UDASA CLUBCreated ByBainas Wamunza, Huila C. Mlama, Tahir Haroub Othman, Kemmy Mutahaba, Martin Jay PShow all (5)
More InfoFor those who lived in and around Chuo (Mlimani) in the 80s and 90S karibu kukutana na marafiki wa zamani. Nyama choma, drinks, football, music, kids corner etc
mindhali umeleta habari za salamander basi poa
sasa unapajua NGAZI TANO? ni huu upande wa MKWEPU nyuma ya kwa Khery wa magazines ambaye naye pale si unajua tulikuwa tunajipatia ma RIGHT ON na WORD UP ( najuaOLE na wenzie watakuwa wanajiuliza sie tunazungumzia nini hapa( sasa pale NGAZI TANO kulikuwa na travel agency hiyo ukitaka VISA ya INDIA basi unaata na Ticket kwa hiyo watu wa midude wote walikuwa wanachukua ticket zao za kwenda shamba ...labda mpaka bombaya kisha machizi wanaingia zao PUK au wanajitwinga ndani ya PASHAWAR na kule si unajua kama unaroo ya paka basi unaweza kuingia na mzigo nyuma ya punda mpaka Iran ambako mzigo ulikuwa unanunulika kwa bei nzuri kinoma
Anywa back to salamander ebwana unamjua CARL LWEIS? nasikia naye yuko NY na MUSA yule mtoto wa Kipemba na wote wanakwenda kama FREAKY TAH maana si midreadlocks hiyo...
Hivi unamkumbuka LUGANO alikuwa nauza Juisi pale salamander? je unaikumbuka ile video library pale ilikuwa inatwa TAKE 5?
Lazima utakuwa na wewe ulishawahi kukutana na akina MWAKITWANGE, JESSE,SAIDI (nasikia yuko UJERUMANI alipatatoto la kijerumani) na bila kumsahau ndugu yetu bwana JOFREY na mwenzie DULA..japo dula aliamua kutukimbia na kwenda kijiwe cha WAUZA VIWANJA na MAGARI MNAZI MMOJA...kule nako noma ile mbaya maana kwanza hakuna kuitana kula wlala nini ...nazungumzia kijiwe cha Mnazi mmoja, pili kama una bahati basi umapate TALL ambaye mnapa cut yake ya laki moja na nyie mkipatalaki tatu poa, au ukiuza gari basi umpate NDAMA na enzi hizo mali asli walikuwa na yule JUMA NGIDA au juma NYAMIELA basi ahhh ndama alikuwa haaci kutupa shavu
ebwan uliwahi kuonana na MSOFE?
ehhh! bado ipo hewani hii? wachangiaji wa hii thread wapo kweli ?