Hatutarudi nyuma, utafiti wetu unaonyesha polisi walipotumia nguvu tumefanikiwa

mpk

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
3,115
3,864
Hivi karibuni tumepigwa mabomu na kusambaratisha mikutano yetu au kutuwekea vizuizi kama kule Mwanza, Kahama, Dar na Dodoma. Baadhi tumefikishwa mahakamani kwa makosa ya kufanya mikusanyiko isiyo na kibali na kukaiadi amri za polisi. Hili si jambo jipya sana na hapa chini ntawakumbusha matukio kama haya yalivyotunufaisha kisiasa huko nyuma

Kila mtu anakumbuka mabomu ya Mtwara wakati wa gesi na vurugu hizo zilisambaa mpaka Lindi. Kaulize leo maeneo hayo ambayo mwanzoni yalikuwa ngome madhubuti ya Ccm yako mikononi mwa nani? Kumbuka vurugu za Nyamongo Tarime ambapo polisi wamepambana na raia kwa miaka zaidi ya 10 leo majimbo yote ya Tarime yako mikononi mwa Chadema.

Kumbuka matukio ya Arusha, mpaka Lema akapachikwa sifa ya kuuvuruga mji wa Arusha. Mauaji ya Soweto ayatosahaulika, lakini lilipokuja suala la uchaguzi Ccm walibaki na diwani mmoja Arusha. Kumbuka kipigo walichopata wakulima na wafugaji ktk mkoa wa Morogoro, ulipokuja uchaguzi wakayapeleka majimbo manne Chadema. Mnakumbuka alivyokandamizwa Sugu na Msigwa majimboni kwao, ulipokuja uchaguzi wananchi hawakuwachagua wao tu bali waliwakabidhi na majiji kabisa kwa kuwapa madiwani wa kutosha.

Hakuna sehemu ambapo demokrasia inakandamizwa kama Zanzibar lakini ukweli ni kwamba nchi hii hakuna sehemu upinzani umeshamiri kama Zanzbar. Wanatumia jeshi la polisi kutuzuia na kuminya uhuru wetu kabla ya kufanya utafiti jeshi hilo linaonekanaje mbele ya jamii. Haliwezi likawa linatupandisha? Yetu macho, haturudi nyuma.
 
Tehetehetehetehe. Huo utafiti mmeufanya lini na hayo mafanikio mmeyapata katika angle ipi? Wewe endelea kuandamana humu JF.
 
Tehetehetehetehe. Huo utafiti mmeufanya lini na hayo mafanikio mmeyapata katika angle ipi? Wewe endelea kuandamana humu JF.

Huu utafiti naona umekuchoma kweli. Hebu lete wa kwako. Maana hoja hupingwa kwa hoja.
 
Zama zinebadirika sana. Huwa imezoeleka kuwa nchi zinatawaliwa kijeshi lakini hii ya Kwetu inatawaliwa Kipolisi.
 
Tangu bunge lisionyeshwe live mmetafuta media outlets nyingine hamna jipya shida yenu kubwa ni kuonekana kwenye tv hamna sera za kumguza mtanzania moja kwa moja zaidi ya maandamano
 
Tangu bunge lisionyeshwe live mmetafuta media outlets nyingine hamna jipya shida yenu kubwa ni kuonekana kwenye tv hamna sera za kumguza mtanzania moja kwa moja zaidi ya maandamano
Wanaotaka kuonekana kwenye tv ni wale wanaotaka kuwajibisha watumishi wakaita vyombo vyote vya habari
 
Udikteta wa magufuli utamzamisha Tanzania sio chato anadhani akina makonda watamsaidia wachumia tumbo
 
Tehetehetehetehe. Huo utafiti mmeufanya lini na hayo mafanikio mmeyapata katika angle ipi? Wewe endelea kuandamana humu JF.
Ungesema au ku-challenge kwa vigezo siyo taarabu
 
Mkuu mpk, utafiti wako ni sahihi kwa 100%...Hiyo mikoa uliyotaja ya Lindi na Mtwara, ni kweli kwamba ilikuwa ngome imara sana ya chama cha baba Je.sca, lakini leo hii, kutoka majimbo mawili ya upinzani, yameongezeka matano na kufikia 7. Majimbo hayo ni Kilwa Kaskazini, Kilwa Kusini, Liwale, Mchinga, Ndanda, Tandahimba na Mtwara Mjini. Majimbo kama ya Mtwara Vijijini, Newala na Masasi, 2020 haina ubishi yatabebwa na UKAWA. Huo ndo ukweli wenyewe.
 
Mkuu mpk, utafiti wako ni sahihi kwa 100%...Hiyo mikoa uliyotaja ya Lindi na Mtwara, ni kweli kwamba ilikuwa ngome imara sana ya chama cha baba Je.sca, lakini leo hii, kutoka majimbo mawili ya upinzani, yameongezeka matano na kufikia 7. Majimbo hayo ni Kilwa Kaskazini, Kilwa Kusini, Liwale, Mchinga, Ndanda, Tandahimba na Mtwara Mjini. Majimbo kama ya Mtwara Vijijini, Newala na Masasi, 2020 haina ubishi yatabebwa na UKAWA. Huo ndo ukweli wenyewe.
Lazima tuwakumbushe hawa makaburu weusi maana wanadhani wanafanya suala jipya kumbe sisi tumezoea
 
Back
Top Bottom