Siku hizi kusikia kwamba mwanachi asiye na hatia ameuwawa na Polisi si jambo la ajabu tena.Polisi nao sasa wanajichukulia sheria mikononi mwao.Matukio ya namna hii yameripotiwa na vyombo vya habari kule Dar es Salam,Arusha,Tunduma,na hivi karibuni kabisa kule Kyela.Nina hakika kwamba yako mengi ambayo kwa bahati mbaya yanapita kimya kimya bila kuripotiwa.Huwa mimi najiuliza kuna nini hasa?
Binafsi ningependa kujua kwa kina kwa nini hasa matukio haya yanatokea.Kwa bahati mbaya anayejua kwa usahihi kabisa sababu ya mauaji hayo ni muuaji,yaani polisi,lakini mara nyingi sio rahisi yeye kutoa ukweli.Lakini it all boils down to one fact,and that is,ameua.Sasa tutaendelea na mtindo huu wa Polisi kuua wanachi wasio na hatia mpaka lini?
Sio siri tena kwamba wanachi walio wengi hawana imani kabisa na jeshi la Polisi,nikiwemo mimi mwenyewe.Si jisifu,lakini mimi ni raia mwema kabisa.Lakini sijui ni lini jamaa hawa wataninyemelea na kutaka kunichuna kwa nguvu kama wale jamaa zangu wa Ifakara na hatimaye mauti kunikuta.Au hata sijui ni lini tutagongana mtaani!No,let's be serious we are in a very bad situation indeed.Polisi badala sasa ya kuwa walinzi wa wananchi wamekuwa watesi wao.
Niseme jambo moja wazi,katika hali kama hii,serikali inategemea wananchi wafanye nini.Wakae chini walie na huku wanaendelea kunyanyaswa na hata kuuwawa?Baya zaidi ni kwamba, kwa wale polisi wanaoua na kunyanyasa wananchi, mambo yanaisha kimya kimya tu,na haya yote wanachi wanaona na wanayajua.Namhurumia sana Zombe,wanaweza kumtoa kafara!
Naiomba serikali ijue kwamba mateso wanayopata wananchi kutoka kwa polisi ni mengi, tumepoteza imani na jeshi hilo kabisa.Labda ni vema serikali ikaunda tume ya maridhiano,ili kila aliyepata mateso kutoka kwa polisi apate nafasi ya kusema,na polisi aliyetesa aombe msamaha au achukuliwe hatua,vinginevyo tunakoelekea sio kuzuri hata kidogo.
Binafsi ningependa kujua kwa kina kwa nini hasa matukio haya yanatokea.Kwa bahati mbaya anayejua kwa usahihi kabisa sababu ya mauaji hayo ni muuaji,yaani polisi,lakini mara nyingi sio rahisi yeye kutoa ukweli.Lakini it all boils down to one fact,and that is,ameua.Sasa tutaendelea na mtindo huu wa Polisi kuua wanachi wasio na hatia mpaka lini?
Sio siri tena kwamba wanachi walio wengi hawana imani kabisa na jeshi la Polisi,nikiwemo mimi mwenyewe.Si jisifu,lakini mimi ni raia mwema kabisa.Lakini sijui ni lini jamaa hawa wataninyemelea na kutaka kunichuna kwa nguvu kama wale jamaa zangu wa Ifakara na hatimaye mauti kunikuta.Au hata sijui ni lini tutagongana mtaani!No,let's be serious we are in a very bad situation indeed.Polisi badala sasa ya kuwa walinzi wa wananchi wamekuwa watesi wao.
Niseme jambo moja wazi,katika hali kama hii,serikali inategemea wananchi wafanye nini.Wakae chini walie na huku wanaendelea kunyanyaswa na hata kuuwawa?Baya zaidi ni kwamba, kwa wale polisi wanaoua na kunyanyasa wananchi, mambo yanaisha kimya kimya tu,na haya yote wanachi wanaona na wanayajua.Namhurumia sana Zombe,wanaweza kumtoa kafara!
Naiomba serikali ijue kwamba mateso wanayopata wananchi kutoka kwa polisi ni mengi, tumepoteza imani na jeshi hilo kabisa.Labda ni vema serikali ikaunda tume ya maridhiano,ili kila aliyepata mateso kutoka kwa polisi apate nafasi ya kusema,na polisi aliyetesa aombe msamaha au achukuliwe hatua,vinginevyo tunakoelekea sio kuzuri hata kidogo.