Kama alivyosema Mzee Mkapa katika moja ya hotuba yake makini aliyoitoa mwishoni mwa miaka ya 2004 ambayo imenukuliwa katika vyombo mbalimbali vya habari na katika jarida la Mzalendo la Chama Cha Mapinduzi, kuwa CCM ikipiga chafya wengine wote wanapata homa"
Ukweli huo umebaki hivyo na utabaki hivyo milele kuwa CCM ndio Baba ndio Mama wa nchi hii, ni CCM pekee yenye kuweza kufanya uamuzi wa dhati wa hatma na mustakabali wa nchi.
CCM inakutana wiki hii mjini Dodoma kufanya maamuzi ya hatma ya nchi, kuamua nani anakuja kuwa mrithi wa Jakaya, nani anakuwa Rais wa awamu ya tano, maana ukweli ni kuwa mgombea wa CCM ndio Rais wa Tanzania kwani hakuna Chama wala kikundi cha walafi kinachoweza kutoa Rais ama chenye uhakika wa kupata hata wabunge 20 katika uchaguzi wa 2015.
Wananchi, vyombo vyote vya habari na vyama vya siasa wooote masikio yao yameelekezwa Dodoma kusikiliza nini CCM inataka kuamua, ndio ni kwa sababu CCM ndio baba wa Taifa hili na maamuzi ya baba ni maamuzi ya Familia nzima, CCM ikiamua Taifa limeamua.