Hatma ya Kagera ipo mikononi mwa wenyeji wake

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,125
7,889
Mimi huwa ni mfuatiliaji wa mada mbalimbali zinaziobukaga humu ndani kuhusiana na maendeleo ya mikoa mbalimbali ikiwemo ya Kagera.

Pamoja na kwamba mada nyingi huwa zinaishia katika mabishano ya kuwashutumu wanaKagera kwa majivuno, na wengine wakisema ni wavivu lakini kuna mambo fulani huwa yanasemwa huwa yanafikirisha sana.

Wakati huo huo kuna wengine wanakujaga kuwatetea wenyeji wa Kagera kuwa wamekuwa target ya kuwadhoofisha kimkakati kwa miaka mingi. Pia nakumbuka kuna mtu akipinga hoja ya umasikini wa Kagera alisema si kweli kuwa Kagera ni masikini, akatolea mfano kuwa route za ndege za Bukoba huwa zinajaa muda wote. Hii comment naikumbuka vizuri.

Tukio la hivi karibuni la ajali ya ndege linafikirisha sana. Response ya mamlaka za uokoaji na zile za usalama zinatia shaka siyo tu ufanisi wa taasisi hizi lakini pia dhamira ya serikali dhidi ya mkoa huo.

Kwa mtazamo wangu, na uko huru kutofautiana na mimi katika hili, wenyeji wa mkoa ule wamelitumikia taifa hili kwa uadilifu mkubwa kwa miaka mingi. Toka nimeanza kufuatilia mambo ya nchi hii, nimewasikia wenyeji wa mkoa ule wakifanya kazi za kiuongozi na kitaaluma.

Ukiacha shutuma dhidi ya watu wachache kipindi cha IPTL, nachelea kusema wenyeji wa mkoa ule hawastahili mambo yanayosemwa au kufanywa dhidi yao au mkoa wao. Inawezekana pia usomi na uwezo wa kufanya vizuri katika elimu wa wenyeji wa mkoa ule umezaa chuki au aina fulani ya husda kutoka kwa baadhi ya watanzania wenzao dhidi yao.

Sijui nini kitakuja kutokea kubadili dhamira ya serikali ila nikitazama naona ni wajibu wa wenyeji wa mkoa huu kutambua kuwa hatma ya mkoa huu ipo mikononi mwao wenyewe.

Kama kuna mtawala walimkosea, ingekuwa vizuri waambiwe ili ikibidi wazee wa mkoa waombe radhi ili adhabu yao ifikie ukomo.

PS. Mimi ni mwenyeji wa Nyanda Juu Kusini, nimeguswa tu na jambo hili. Hii mada nilitaka kuileta mapema nikaifuta maana sidhani kama itabadilisha chochote. Inaweza kuishia katika majibizano kama yale ya siku zote.
 
Nina kampeni ya Kulishtua Taifa kidogo akina Tinandebage, na wengine waloteka ndege Miaka ya 82 ni cha mtoto maana Wahaya wanaonekana Kama watu wa Kufanyia maigizo ya kupimana viatu Kwa kamba
 
Nina kampeni ya Kulishtua Taifa kidogo akina Tinandebage, na wengine waloteka ndege Miaka ya 82 ni cha mtoto maana Wahaya wanaonekana Kama watu wa Kufanyia maigizo ya kupimana viatu Kwa kamba
Naona wameamua kuufifisha uzi huu kitaalamu ila huu ni mjadala muhimu kwa mustakabali wa taifa.
 
Maendeleo hayahitaji uchawi, investment investment investment , Banks za maana (capital) na knowledge ni vitu muhimu sana, wangeanza na samaki waliojaliwa na mungu, investments kwenye ujenzi wa boat za kisasa, viwanda vya samaki vingewasaidia sana kuongeza mapato ya mkoa na watu wake
 
Maprofesa wa Kagera wanapaswa kijifunza jambo dogo: hatma ya Kagera ipo mikononi mwao!
 
Mimi huwa ni mfuatiliaji wa mada mbalimbali zinaziobukaga humu ndani kuhusiana na maendeleo ya mikoa mbalimbali ikiwemo ya Kagera.

Pamoja na kwamba mada nyingi huwa zinaishia katika mabishano ya kuwashutumu wanaKagera kwa majivuno, na wengine
fanya utafiti tena naona hapa unaongelea kiushabiki vile na inawezekana na wewe pia ni wa huko.kwani nchi hii waliosoma ni wahaya tu?wanyakyusa,wachaga,wapare nk nao je?matatizo ya wenyeji wa bukoba hii ni mengi.yako ya kijami,kisiasa na kiuchumi hivyo ili kujiridhisha na hayo yanayosemwa inabidi mtu ayafanyie kazi kweli kweli na si kwenda na ushabiki tu.kwa wale ambao tuliishawahi kukaa kwa miaka ktk mkoa huu tunafahamu angalau machache tuliyoyaona kwa macho yetu.moja ktk swala la kujituma kwa kagera hilo halipo,ni kweli ni watu wavivu tena sana tu na pia hupenda kupata pesa kwa njia za udanganyifu.ni watu ambao kama huko makini nao unaweza kulizwa wakati wowote hivyo kama wewe ni mfanya biashara inakupasa kuwa makini nao sana.issue ya kusoma watu huwa wanapenda ku generalize sana.ni sehemu chache sana ambazo kweli watu walichangamkia elimu lkn hata hao waliochangamkia elimu hawana mchango wowote kwa mkoa wao.wakisha elimika huuhama mkoa wao na kwenda kuishi sehemu tofauti kabisa na kwao.wanachokifanya ni kujenga majumba na kuyaacha kama magofu tu ambayo hayakaliwi na mtu yoyote bali utakutana na walinzi wa usafi tu.kundi kubwa la waliosoma mkoa wanaishi nje ya nchi hii na hawachangii lolote ktk uchumi wa mkoa huu hivyo kuufanya ubaki nyuma kimaendeleo.watu wa mkoa huu wanapenda sana kesi na malumbano yasiyo na tija hivyo kuwapotezea muda mwingi wa kufanya mambo ya msingi.ni watu wambeya na wanafiki fulani hivi na hata ukifanya nao hupenda sana kuongea kilugha chao.ni watu ambao hawana misimamo,na wanapenda kujisifu kila wakati.kuna mengi ya kuongelea kuhusu hii jamii ila watu wafanye tafiti wanatagundua strengths na weaknesses zao.
 
Sio Kagera tu,kunahitajika juhudi za makusudi za viongozi kusogeza huduma za muhimu kwa mikoa yote ya pemebezoni mwa nchi,nadhani unajua mambo mengi mazuri na matamu ya nchi hii yanaingilia au kuanzia Dar au yapo Dar,ndio maana ilikuja wazo la Dodoma kuwa makao makuu,kwani kwakuwa iko katikati ya nchi basi itasaidia huduma kufikia mikoa mingine kwa urahisi,hii nahisi ndio maana hata Raisi aliyepita pia alijikuta akitumia nguvu nyingi kutaka kulifanikisha hili ingawa muda haukuwa rafiki kwake...
 
Mimi huwa ni mfuatiliaji wa mada mbalimbali zinaziobukaga humu ndani kuhusiana na maendeleo ya mikoa mbalimbali ikiwemo ya Kagera.

Pamoja na kwamba mada nyingi huwa zinaishia katika mabishano ya kuwashutumu wanaKagera kwa majivuno, na wengine wakisema ni wavivu lakini kuna mambo fulani huwa yanasemwa huwa yanafikirisha sana.

Wakati huo huo kuna wengine wanakujaga kuwatetea wenyeji wa Kagera kuwa wamekuwa target ya kuwadhoofisha kimkakati kwa miaka mingi. Pia nakumbuka kuna mtu akipinga hoja ya umasikini wa Kagera alisema si kweli kuwa Kagera ni masikini, akatolea mfano kuwa route za ndege za Bukoba huwa zinajaa muda wote. Hii comment naikumbuka vizuri.

Tukio la hivi karibuni la ajali ya ndege linafikirisha sana. Response ya mamlaka za uokoaji na zile za usalama zinatia shaka siyo tu ufanisi wa taasisi hizi lakini pia dhamira ya serikali dhidi ya mkoa huo.

Kwa mtazamo wangu, na uko huru kutofautiana na mimi katika hili, wenyeji wa mkoa ule wamelitumikia taifa hili kwa uadilifu mkubwa kwa miaka mingi. Toka nimeanza kufuatilia mambo ya nchi hii, nimewasikia wenyeji wa mkoa ule wakifanya kazi za kiuongozi na kitaaluma.

Ukiacha shutuma dhidi ya watu wachache kipindi cha IPTL, nachelea kusema wenyeji wa mkoa ule hawastahili mambo yanayosemwa au kufanywa dhidi yao au mkoa wao. Inawezekana pia usomi na uwezo wa kufanya vizuri katika elimu wa wenyeji wa mkoa ule umezaa chuki au aina fulani ya husda kutoka kwa baadhi ya watanzania wenzao dhidi yao.

Sijui nini kitakuja kutokea kubadili dhamira ya serikali ila nikitazama naona ni wajibu wa wenyeji wa mkoa huu kutambua kuwa hatma ya mkoa huu ipo mikononi mwao wenyewe.

Kama kuna mtawala walimkosea, ingekuwa vizuri waambiwe ili ikibidi wazee wa mkoa waombe radhi ili adhabu yao ifikie ukomo.

PS. Mimi ni mwenyeji wa Nyanda Juu Kusini, nimeguswa tu na jambo hili. Hii mada nilitaka kuileta mapema nikaifuta maana sidhani kama itabadilisha chochote. Inaweza kuishia katika majibizano kama yale ya siku zote.
Kagera imeikosea nini CCM?
 
Back
Top Bottom