Hatimaye tapeli sugu wa viwanja nchini atiwa nguvuni

bongo dili

JF-Expert Member
Feb 13, 2015
12,371
24,601
Wasalamu, kupitia msaada wa mitandao ya jamii imefanikisha kulikamata tapeli sugu na maarufu nchini jina Yonah Kittah pichani chini.

Kwa miaka mingi amekuwa akifungia kampuni halali za kuuza viwanja na mashamba kwa kulipia kidogo kidogo kwa awamu.

Kisha ukishamaliza kulipa mkopo wako anaanza danadana ya kukupa kiwanja au shamba lako.

Alifungua ofisi Mbezi beach kwa jina la Yared investment akawatapeli watu viwanja walipomzonga kutaka viwanja au pesa zao akawambia.

Akaenda Ilala Mwalimu House akafungua kampuni inaitwa VKP youth development akiuza viwanja na mashamba ikiwemo kukopesha pikipiki na bajaji akatepeli zaidi ya bilioni moja Mimi ni mmoja wa mhanga kanipiga milioni 60, kwa kampuni pekee ya vkp tumepigwa jumla ya watu 250 kwa idadi ya walipoandikisha kesi mwaka 2020 kwa mikoa ya Arusha, Dodoma,Mwanza na Dar es salaam.

Alikaa ndani akatoka kwa dhamana kesi ikiendelea akakimbia dhamana ya shilingi bilioni moja.
Akaenda fungua kampuni nyingine ya kutapeli viwanja ofisi ikiwa Manzese Darajani akapiga hela, kafungua makampuni mengi tu ya kupiga Hela.

Kama wewe ni muhanga wa hizo kampuni kutapeli viwanja za mmiliki jina Yonah Kittah jongea central Dar ofisi ya upelelezi waone wahusika ukiwa na ushahidi wa documents zako zote wakutolee shimoni mtu wako ili uongezwe kwenye list ya watu waliotapeliwa na Yonah Kittah.

Kwa taarifa alienda Nigeria kujifunza jinsi ya kutapeli watu kitaalamu na jinsi ya kula na wakubwa na jinsi ya kudili na kesi.

Pana mtu kapigwa milion 60 na Yonah kwa ishu za viwanja na ndoa imevunjika mume haelewi somo.

Anachofanya huyu tapeli anaenda kwenye mashamba ya watu Usiku anapima code net kisha anachora ramani nzuri anavipa viwanja plot number anasajili mchoro ardhi kisha anatangaza anauza viwanja mnapelekwa site mnaonyeshwa viwanja pori mkiuliza mbona pori anasema greda lipo njiani kuchonga barabara za mitaa unaingia kingi unasaini mkataba unapewa account ya kampuni unalipia unakuwa unapewa risiti, kimbembe umemaliza unataka hati kiswahili kinaanza, ukienda eneo husika kumtafuta mmiliki anakwambia Mimi simjui Yona wengine wanasema tulifanya nae mapatano ya kununua shamba hakurudi Tena.

Mkiwa wengi mnamsumbua anafunga ofisi anatoroka wasiojua wao wanaendelea kurejesha pesa kwenye account siku unaenda na risiti zako za miezi labda 3 unakuta hakuna ofisi.

Ujinga wake pesa zote hizi anamalizia kwenye starehe hana hata Hela kwenye account zote anaponda raha kila mwanamke mzuri mjini hampiti.

So kama wewe ,ndugu yako au jamaa yako ni mhanga wahi central Dar.

Wahanga ni wengi wakiwemo hadi viongozi, watumishi ndio wa kada zote wakubwa kwa wadogo ni wahanga.

Screenshot_20230512_090130.jpg
 
Usikubali kuuziwa viwanja na hizi kampuni binafsi kwa kujiridhisha na ofisi nzuri location nzuri full documents za usajili ukutani bila kujiridhisha sana hakikisha wamiliki wa kwanza wa shamba Hilo unawajua pili usikubali kutoa pesa yako kwa kuonyeshwa code net au Raman kwa shamba pori eti mtasafishiwa kwa pamoja mkimaliza malipo.
Pana mama analiaa milion 36 imeliwa na Yona na ndoa chali kisa viwanja.
Huyu takataka hajali maumivu ya watu,na Serikali inacheka nae tu.
Watumishi tu mshahara kidogo anajinyima kapata unafuu wa kiwanja alipe kidogo kidogo baada ya mwaka awe na kiwanja aanze kujenga kumbe mwaka mzima unampa pesa mwanaume mwenzio anaenda kuzifanyia ngono,wewe unakula dagaa.
 
Wasalamu, kupitia msaada wa mitandao ya jamii imefanikisha kulikamata tapeli sugu na maarufu nchini jina Yonah Kittah pichani chini.

Kwa miaka mingi amekuwa akifungia kampuni halali za kuuza viwanja na mashamba kwa kulipia kidogo kidogo kwa awamu.

Kisha ukishamaliza kulipa mkopo wako anaanza danadana ya kukupa kiwanja au shamba lako.

Alifungua ofisi Mbezi beach kwa jina la Yared investment akawatapeli watu viwanja walipomzonga kutaka viwanja au pesa zao akawambia.

Akaenda Ilala Mwalimu House akafungua kampuni inaitwa VKP youth development akiuza viwanja na mashamba ikiwemo kukopesha pikipiki na bajaji akatepeli zaidi ya bilioni moja Mimi ni mmoja wa mhanga kanipiga milioni 60, kwa kampuni pekee ya vkp tumepigwa jumla ya watu 250 kwa idadi ya walipoandikisha kesi mwaka 2020 kwa mikoa ya Arusha, Dodoma,Mwanza na Dar es salaam.

Alikaa ndani akatoka kwa dhamana kesi ikiendelea akakimbia dhamana ya shilingi bilioni moja.
Akaenda fungua kampuni nyingine ya kutapeli viwanja ofisi ikiwa Manzese Darajani akapiga hela, kafungua makampuni mengi tu ya kupiga Hela.

Kama wewe ni muhanga wa hizo kampuni kutapeli viwanja za mmiliki jina Yonah Kittah jongea central Dar ofisi ya upelelezi waone wahusika ukiwa na ushahidi wa documents zako zote wakutolee shimoni mtu wako ili uongezwe kwenye list ya watu waliotapeliwa na Yonah Kittah.

Kwa taarifa alienda Nigeria kujifunza jinsi ya kutapeli watu kitaalamu na jinsi ya kula na wakubwa na jinsi ya kudili na kesi.

Pana mtu kapigwa milion 60 na Yonah kwa ishu za viwanja na ndoa imevunjika mume haelewi somo.

Anachofanya huyu tapeli anaenda kwenye mashamba ya watu Usiku anapima code net kisha anachora ramani nzuri anavipa viwanja plot number anasajili mchoro ardhi kisha anatangaza anauza viwanja mnapelekwa site mnaonyeshwa viwanja pori mkiuliza mbona pori anasema greda lipo njiani kuchonga barabara za mitaa unaingia kingi unasaini mkataba unapewa account ya kampuni unalipia unakuwa unapewa risiti, kimbembe umemaliza unataka hati kiswahili kinaanza, ukienda eneo husika kumtafuta mmiliki anakwambia Mimi simjui Yona wengine wanasema tulifanya nae mapatano ya kununua shamba hakurudi Tena.

Mkiwa wengi mnamsumbua anafunga ofisi anatoroka wasiojua wao wanaendelea kurejesha pesa kwenye account siku unaenda na risiti zako za miezi labda 3 unakuta hakuna ofisi.

Ujinga wake pesa zote hizi anamalizia kwenye starehe hana hata Hela kwenye account zote anaponda raha kila mwanamke mzuri mjini hampiti.

So kama wewe ,ndugu yako au jamaa yako ni mhanga wahi central Dar.

Wahanga ni wengi wakiwemo hadi viongozi, watumishi ndio wa kada zote wakubwa kwa wadogo ni wahanga.

View attachment 2694136


Na yeye aje tumsikilize, mji huo huo anafungua kampuni na anawapiga? Haya nyie mliopigwa mfungwe tu.
 
Back
Top Bottom