Hii ni simulizi ya yaliyomtokea mtoto wa marehemu rafiki yangu Mwinyi Mkila wa Bagamoyo.
***********
1. ALFA
Nilifahamiana na Mwinyi Mkila katika harakati za kutafuta shamba Bagamoyo na hatimaye kwa msaada wake nilipata shamba kubwa eneo la Sanzale miaka hiyo ya 1980's.
Mwinyi Mkila alikuwa na watoto kadhaa na mmoja wa watoto hao anaitwa Pazi. Kijana Pazi ndiye mzuwanda kwa Mwinyi Mkila kwa bi mdogo maana Mwinyi Mkila alikuwa na wake wawili.
Mwinyi Mkila mpaka mauti yanamkuta alikuwa akijishughulisha na shughuli za uvuvi na uchuuzi
wa mazao ya baharini. Alikuwa na Jahazi, Mashua, Dau, Ngalawa na Mitumbwi ambayo alikuwa akiwapa
wavuvi kwa mikataba maalumu ya kufanya nao kazi na kumuuzia kitakacho patikana.
Mazao hayo ya baharini hususani samaki yalikuwa yakipelekwa Dar es Salaam kwa ajili ya kuuzwa. Sasa huyu kijana Pazi ndiye aliyekuwa akisimamia zoezi zima la uuzwaji samaki hao na mazao mengine ya baharini katika soko la Feri (Dsm)
Miaka ya 1990's nilipokutana naye Feri wakati nimeenda kununua kitoweo, Pazi alikuwa hayupo kama kawaida, alikuwa amekonda na macho yamekuwa angavu zaidi na kama anatumia nguvu nyingi hivi
ili kuangalia.
Nilipo mjulia hali zaidi ndipo akaniambia kuwa amepata na maradhi yasiyo julikana na akasema kuwa hali yake kila siku inazidi kudhoofu.
Familia ya Mwinyi Mkila haikuwa na shida ndogo ndogo za kiuchumi kwani baba yao alikuwa mkwasi
na maarufu sana Bagamoyo na ukanda wa Pwani kwa ujumla na watoto wake karibuni wote wa kiume
walirithi kazi ya baba yao.
Bada ya mazungumzo ya muda mrefu na Pazi tukaagana na kila mmoja akaendelea na shughuli zake.
***********
Miaka kumi na moja hivi baadaye nilikutana tena na Pazi lakini katika hali tofauti sana na akiwa na afya njema na akaniomba nikapajuwe nyumbani kwake alipojenga sasa hivi.
Tulikutana na Pazi Long-room TRA mkabala na kituo cha mabasi Stesheni - Dar es Salaam siku ya Ijumaa. Akaomba niongozane naye hadi kwake 'Mbezi beach'. Kwa kuwa nilikuwa tayari nimeshamaliza shughuli zangu nilizojipangia kwa siku hiyo, nilikubali kuongozana naye na tukafika kwake eneo la Mbezi Juu kama unataka kwenda Salasala.
Baada ya mazungumzo ya awali ndipo akaanza kunihadithia.
"Baba, hujafa hujaumbika!" alisema Pazi.
"Enhe!?", niliitikia kwa shauku ya kutaka kujuwa zaidi na zaidi.
Pazi alianza kunisimulia:-
***********
Tangia nasoma shule ya Msingi Kizuiani Bagamoyo, nimekuwa nikimsaidia Baba kazi zake za uvuvi. Japo wakati huo nilikuwa siendi baharini kuvua, lakini vyombo (mashua nk) vinaporudi huwa nakuwa pwani ufukweni nikisimamia yale niliyopangiwa na wakubwa wangu.
Jahazi letu kazi yake kubwa ilikuwa ni kusafirisha mizigo kutoka huku Bagamoyo kwenda Unguja na mizigo ya Unguja kuileta Bagamoyo. Mashua ilikuwa kwa ajili ya kazi za uvuvi maalum ambapo chombo hukabidhiwa nahodha, yeye ndiye anakuwa na jukumu la kuwatafuta wavuvi atakao shirikiana nao katika zoezi zima la uvuvi. Dau mara zote tumekuwa tukiwakodisha 'Wakojani' kwa ajili ya shughuli zao za uvuvi wa 'juya' kisha wao huwa huru kuuza mavuno popote lakini hukilipia chombo kwa fedha taslimu kila siku warudipo kuvua kwa kadri tulivyo kubalina. Ngalawa na mitumbwi pia huwa wanalipa kwa fedha taslimu na wapo huru kuuza sehemu yoyote ingawaje mara nyingi huja kutuuzia sisi wenyewe.
Jahazi, Dau, Ngalawa wanatumia 'tanga', lakini mtumbwi wanatumia 'makasia' peke yake na kwenye Mashua wanatumia tanga pamoja na injini.
Baada ya kumaliza darasa la saba wavuvi wa mashua walipanga kwenda 'dago' maeneo ya Sadani na Mkwaja kwa ajili ya zoezi la kuvua 'kamba' na 'kaji' (prawns), na Kamba koche (robuster), niliamua kuongozana nao kwa kuwa sasa nilikuwa huru zaidi kuliko wakati nikisoma.
Tulijiandaa vyema kwa ajili ya safari hiyo ya kwenda kupiga kambi (dago) kwa kubeba unga wa ugali, mafuta kidogo ya kupikia na vifaa vya uvuvi kama vile nyavu maalumu kwa ajili ya kuvulia kamba na kaji, Petroli ya kutosha, tofali za barafu za kutosha na vifaa vingine.
Siku ya safari tulisubiri maji yajae kusogea ufukweni ili chombo kiweze kuelea kwa sababu 'yalikupwa'. Muda wa kuanza safari ulipowadia nahodha aliamrisha baharia mmoja ashike 'upondo' na kuanza kukitembeza chombo huku baharia mwingine akivuta kamba ya nanga kurahisisha uelekeo wa kuielekea nanga ili ipandishwe na safari ianze.
Nahodha aliwasha mashine Yamaha Enduro supa 40 (horse power 40), nanga ikang’olewa (ikaingizwa kwenye mashua) na safari ikaanza mdogo mdogo. 'Hatukutweka tanga' kwa kuwa hali ya bahari ilikuwa shwari hivyo hakukuwa na upepo wa kutosha kuiendesha mashua kwa kasi.
Ilikuwa mida ya alasiri ndipo tuling'oa nanga kuelekea dagoni, na tulifika Mkwaja usiku mwingi na nahodha aliamuru nanga ishushwe 'nje kidogo' kwenye maji mengi kabla ya kufika ufukweni ili tupate kulala kabla hapajakucha tukiwa ndani ya mashua.
Palivyokucha tulisogeza chombo ufukweni, tukashusha mizigo yetu na kuanza kuandaa kambi. Siku nzima siku hiyo ilikuwa ni kujenga vibanda. tulijenga vibanda vitatu ambapo banda kuu lilikuwa la nadhodha na wasaidizi wake wawili, na mizigo yote ilikuwa hapo, mabanda mawili yaliyobaki yalikuwa ya wavuvi ambapo wanne walikaa kwenye kila banda. Mabanda haya ni yale ya kusimikwa kwa miti na kuezekwa kwa makuti juu ambapo msuko wa aina ya 'kumba' na 'pande' ilitumika na pembeni kulizibwa vivyo hivyo kwa makuti ili kukabiliana na upepo kutoka baharini hususani nyakati za usiku.
Kwa kuwa nilikuwa kijana mdogo tena mfupi, sikuruhusiwa kuingia baharini kwa ajili ya kuvua, bali niliachwa kambini pamoja na msaidizi wa nahodha kama walinzi mashahidi wa kambi. siku ya kwanza hadi ya tatu zoezi liliendelea vizuri, na tulifanikiwa kupata kaji wengi sana pamoja na kamba wachache.
Wavuvi wenyewe hujuwa ni wakati gani na sehemu gani waende kuvua. kamba na kaji huvuliwa kwa nyavu moja kushikwa na wavuvi wawili mmoja huku na mwingine kule kisha wakianzia maji mengi na kutembea taratibu kuja maji machache na hatimaye kuwanasa kamba na kaji na mazao mengine ya baharini yaliyonasa kwenye nyavu kisha huja kando kando ya bahari na kuanza kuchambua, kamba na kaji huhifadhiwa kwenye tenga, samaki wengine waliwao huwekwa kwa ajili ya kitoweo na baadhi
ya viumbe wengine wa bahari hurudishwa baharini ama kuachwa tu wakizagaa.
Siku ya nne nilibaki peke yangu kambini na ndiyo nadhani ikawa ni sababu ya maradhi yangu yaliyonisumbua kwa muda mrefu sana.
Kambini kwetu asubuhi wavuvi hunywa supu ya samaki tu na kujiandaa na kazi kwa kuangalia mwenendo wa maji. baada la zoezi la uvuvi asubuhi, wakirudi hupikiwa ugali kwa samaki kisha kusubiri zoezi lingine kulingana na mwendendo wa maji, hivyo kwa siku
huwa kuna mazoezi mawili makuu ya kuvua kamba na kaji.
Sasa siku hiyo mida yao kurudi ili wapate chakula cha mchana ilikuwa majira ya saa sita hivi, hivyo nami katika harakati za kumsaidia mpishi wa zamu (msaidizi wa nahodha) kuwasha moto, nikapatwa na gumbizi (kuzunguzungu) na kuanguka chini. Sikuelewa kilichondelea hadi baadaye nilipopata fahamu nikawaona wavuvi wote wamenizunguka huku nahodha akiniuliza ninajisiaje sasa.
"Najisikia vizuri ila nahisi uchovu tu, kwani kimetokea nini?" nilijibu na kuuliza.
Nahodha akaniambia kuwa nilianguka na kusogezwa kibandani na msaidizi wake na nikawa kama nimezimia na kupoteza fahamu, wao waliitwa kuja kunisaidia haraka kwa kunipepea na kunimwagia maji ndipo nikazinduka.
Nikapewa supu ya Samaki aina ya 'Songolo' nikanywa nikapata nguvu kidogo na ugali ukasongwa
wengine wote walikula lakini mimi nilitosheka na supu ya samaki sikujisikia kula tena. Zoezi la jioni walibaki watu watatu pale kambini pamoja nami, yaani nahodha na wasaidizi wake wawili, wavuvi wengine waliendelea kuvua.
Kwakuwa ilikuwa msimu wa 'bamvua' lenye samaki wengi, haikutuchukua zaidi ya siku kumi kujaza
vyombo vyetu vyote samaki aina ya kamba na kaji. Lilifanyika zoezi la ziada kwa ajili ya uvuvi wa maji mengi ili kupata samaki wakubwa kwa njia ya 'mishipi', basi wiki hiyo iliyofuata tulitumia usiku wa kiza kwenda kuvua Jodari, Sehewa, Papa, Chewa na Nguru. Kambini tulikuwa tunawaacha wavuvi wanne wakilinda samaki na kambi kwa ujumla, mimi hawakutaka kuniacha kwa kuhofia nisije nikaanguka tena wao wakiwa mbali.
Zoezi hili la usiku nilikuwa nikilifurahia kwa kuwa hatuingii ndani ya maji, bali tunawasha tu 'karabai' na kuweka chambo kwenye ndoano na kuanza kuvua huku 'mishoto' ikiwa jirani kwa ajili ya 'kuwatuliza' samaki wasumbufu kabla ya kumtoa kwenye ndoano.
Tulipata Jodari wachache, sehewa wengi, nguru wachache, papa mmoja na chewa mkubwa mmoja kwa zoezi zima la wiki hiyo. Chakula Unga kutoka mjini Bagamoyo tulichukuwa wa kutosha wiki nne, lakini Nahodha aliamuru turudi mjini baada ya wiki tatu na nusu kwa kuwa tulishapata mavuno ya kutosha.
***********
Safari ya kurudi ilianza, lakini kwa upande wangu niliona vituko njiani kadha wa kadha, tulianza safari
jioni sana ili tutembee usiku kucha na asubuhi tuwe tumefika. Ilikuwa ni kawaida ya vyombo vyetu kuja 'kutua' maeneo ya pwani ya msikiti wa Ijumaa Bagamoyo "nchi pana", (siku hizi wanapaita kwa Zakaria / Alfazul).
Kituko cha kwanza ni kuona moto mwekundu ukiwaka baharini pasipo na chombo chochote,
awali nilidhani ni wavuvi wenzetu wakivua lakini nilipo muuliza nahoda alinijibu kuwa hapana,
siyo wavuvi, wale ni "vibwengo"
'Wakati nasoma kizuiani, nimesikia simulizi nyingi za vibwengo, leo hatimaye naaza kushuhudia
mubashara', nilijisemea.
Vimbwengo kwa simulizi ni aina fulani ya viumbe ambavyo aghalabu hupatikana maeneo yenye maji mengi mfano wa mabwawa makubwa, mito, maziwa, bahari. Viumbe hivi husemekana vina uwezo wa kujibadilisha muonekano wao, na wakiwa katika umbo la mfano wa mwanadamu basi huwa wafupi. wana uwezo wa kuonekana na kupotea kwa ghafla. hupenda kuwatisha binadamu lakini inasemekana hawana madhara makubwa kwa binadamu.
Inasemekana pia ni aina fulani ya kabila moja ya jamii (specie) ya majini. Sasa ile mioto ilikuwa inaonekana na tunapoikaribia inapotea na kuonekana umbali mwingine.
************
Inaendelea...
***********
1. ALFA
Nilifahamiana na Mwinyi Mkila katika harakati za kutafuta shamba Bagamoyo na hatimaye kwa msaada wake nilipata shamba kubwa eneo la Sanzale miaka hiyo ya 1980's.
Mwinyi Mkila alikuwa na watoto kadhaa na mmoja wa watoto hao anaitwa Pazi. Kijana Pazi ndiye mzuwanda kwa Mwinyi Mkila kwa bi mdogo maana Mwinyi Mkila alikuwa na wake wawili.
Mwinyi Mkila mpaka mauti yanamkuta alikuwa akijishughulisha na shughuli za uvuvi na uchuuzi
wa mazao ya baharini. Alikuwa na Jahazi, Mashua, Dau, Ngalawa na Mitumbwi ambayo alikuwa akiwapa
wavuvi kwa mikataba maalumu ya kufanya nao kazi na kumuuzia kitakacho patikana.
Mazao hayo ya baharini hususani samaki yalikuwa yakipelekwa Dar es Salaam kwa ajili ya kuuzwa. Sasa huyu kijana Pazi ndiye aliyekuwa akisimamia zoezi zima la uuzwaji samaki hao na mazao mengine ya baharini katika soko la Feri (Dsm)
Miaka ya 1990's nilipokutana naye Feri wakati nimeenda kununua kitoweo, Pazi alikuwa hayupo kama kawaida, alikuwa amekonda na macho yamekuwa angavu zaidi na kama anatumia nguvu nyingi hivi
ili kuangalia.
Nilipo mjulia hali zaidi ndipo akaniambia kuwa amepata na maradhi yasiyo julikana na akasema kuwa hali yake kila siku inazidi kudhoofu.
Familia ya Mwinyi Mkila haikuwa na shida ndogo ndogo za kiuchumi kwani baba yao alikuwa mkwasi
na maarufu sana Bagamoyo na ukanda wa Pwani kwa ujumla na watoto wake karibuni wote wa kiume
walirithi kazi ya baba yao.
Bada ya mazungumzo ya muda mrefu na Pazi tukaagana na kila mmoja akaendelea na shughuli zake.
***********
Miaka kumi na moja hivi baadaye nilikutana tena na Pazi lakini katika hali tofauti sana na akiwa na afya njema na akaniomba nikapajuwe nyumbani kwake alipojenga sasa hivi.
Tulikutana na Pazi Long-room TRA mkabala na kituo cha mabasi Stesheni - Dar es Salaam siku ya Ijumaa. Akaomba niongozane naye hadi kwake 'Mbezi beach'. Kwa kuwa nilikuwa tayari nimeshamaliza shughuli zangu nilizojipangia kwa siku hiyo, nilikubali kuongozana naye na tukafika kwake eneo la Mbezi Juu kama unataka kwenda Salasala.
Baada ya mazungumzo ya awali ndipo akaanza kunihadithia.
"Baba, hujafa hujaumbika!" alisema Pazi.
"Enhe!?", niliitikia kwa shauku ya kutaka kujuwa zaidi na zaidi.
Pazi alianza kunisimulia:-
***********
Tangia nasoma shule ya Msingi Kizuiani Bagamoyo, nimekuwa nikimsaidia Baba kazi zake za uvuvi. Japo wakati huo nilikuwa siendi baharini kuvua, lakini vyombo (mashua nk) vinaporudi huwa nakuwa pwani ufukweni nikisimamia yale niliyopangiwa na wakubwa wangu.
Jahazi letu kazi yake kubwa ilikuwa ni kusafirisha mizigo kutoka huku Bagamoyo kwenda Unguja na mizigo ya Unguja kuileta Bagamoyo. Mashua ilikuwa kwa ajili ya kazi za uvuvi maalum ambapo chombo hukabidhiwa nahodha, yeye ndiye anakuwa na jukumu la kuwatafuta wavuvi atakao shirikiana nao katika zoezi zima la uvuvi. Dau mara zote tumekuwa tukiwakodisha 'Wakojani' kwa ajili ya shughuli zao za uvuvi wa 'juya' kisha wao huwa huru kuuza mavuno popote lakini hukilipia chombo kwa fedha taslimu kila siku warudipo kuvua kwa kadri tulivyo kubalina. Ngalawa na mitumbwi pia huwa wanalipa kwa fedha taslimu na wapo huru kuuza sehemu yoyote ingawaje mara nyingi huja kutuuzia sisi wenyewe.
Jahazi, Dau, Ngalawa wanatumia 'tanga', lakini mtumbwi wanatumia 'makasia' peke yake na kwenye Mashua wanatumia tanga pamoja na injini.
Baada ya kumaliza darasa la saba wavuvi wa mashua walipanga kwenda 'dago' maeneo ya Sadani na Mkwaja kwa ajili ya zoezi la kuvua 'kamba' na 'kaji' (prawns), na Kamba koche (robuster), niliamua kuongozana nao kwa kuwa sasa nilikuwa huru zaidi kuliko wakati nikisoma.
Tulijiandaa vyema kwa ajili ya safari hiyo ya kwenda kupiga kambi (dago) kwa kubeba unga wa ugali, mafuta kidogo ya kupikia na vifaa vya uvuvi kama vile nyavu maalumu kwa ajili ya kuvulia kamba na kaji, Petroli ya kutosha, tofali za barafu za kutosha na vifaa vingine.
Siku ya safari tulisubiri maji yajae kusogea ufukweni ili chombo kiweze kuelea kwa sababu 'yalikupwa'. Muda wa kuanza safari ulipowadia nahodha aliamrisha baharia mmoja ashike 'upondo' na kuanza kukitembeza chombo huku baharia mwingine akivuta kamba ya nanga kurahisisha uelekeo wa kuielekea nanga ili ipandishwe na safari ianze.
Nahodha aliwasha mashine Yamaha Enduro supa 40 (horse power 40), nanga ikang’olewa (ikaingizwa kwenye mashua) na safari ikaanza mdogo mdogo. 'Hatukutweka tanga' kwa kuwa hali ya bahari ilikuwa shwari hivyo hakukuwa na upepo wa kutosha kuiendesha mashua kwa kasi.
Ilikuwa mida ya alasiri ndipo tuling'oa nanga kuelekea dagoni, na tulifika Mkwaja usiku mwingi na nahodha aliamuru nanga ishushwe 'nje kidogo' kwenye maji mengi kabla ya kufika ufukweni ili tupate kulala kabla hapajakucha tukiwa ndani ya mashua.
Palivyokucha tulisogeza chombo ufukweni, tukashusha mizigo yetu na kuanza kuandaa kambi. Siku nzima siku hiyo ilikuwa ni kujenga vibanda. tulijenga vibanda vitatu ambapo banda kuu lilikuwa la nadhodha na wasaidizi wake wawili, na mizigo yote ilikuwa hapo, mabanda mawili yaliyobaki yalikuwa ya wavuvi ambapo wanne walikaa kwenye kila banda. Mabanda haya ni yale ya kusimikwa kwa miti na kuezekwa kwa makuti juu ambapo msuko wa aina ya 'kumba' na 'pande' ilitumika na pembeni kulizibwa vivyo hivyo kwa makuti ili kukabiliana na upepo kutoka baharini hususani nyakati za usiku.
Kwa kuwa nilikuwa kijana mdogo tena mfupi, sikuruhusiwa kuingia baharini kwa ajili ya kuvua, bali niliachwa kambini pamoja na msaidizi wa nahodha kama walinzi mashahidi wa kambi. siku ya kwanza hadi ya tatu zoezi liliendelea vizuri, na tulifanikiwa kupata kaji wengi sana pamoja na kamba wachache.
Wavuvi wenyewe hujuwa ni wakati gani na sehemu gani waende kuvua. kamba na kaji huvuliwa kwa nyavu moja kushikwa na wavuvi wawili mmoja huku na mwingine kule kisha wakianzia maji mengi na kutembea taratibu kuja maji machache na hatimaye kuwanasa kamba na kaji na mazao mengine ya baharini yaliyonasa kwenye nyavu kisha huja kando kando ya bahari na kuanza kuchambua, kamba na kaji huhifadhiwa kwenye tenga, samaki wengine waliwao huwekwa kwa ajili ya kitoweo na baadhi
ya viumbe wengine wa bahari hurudishwa baharini ama kuachwa tu wakizagaa.
Siku ya nne nilibaki peke yangu kambini na ndiyo nadhani ikawa ni sababu ya maradhi yangu yaliyonisumbua kwa muda mrefu sana.
Kambini kwetu asubuhi wavuvi hunywa supu ya samaki tu na kujiandaa na kazi kwa kuangalia mwenendo wa maji. baada la zoezi la uvuvi asubuhi, wakirudi hupikiwa ugali kwa samaki kisha kusubiri zoezi lingine kulingana na mwendendo wa maji, hivyo kwa siku
huwa kuna mazoezi mawili makuu ya kuvua kamba na kaji.
Sasa siku hiyo mida yao kurudi ili wapate chakula cha mchana ilikuwa majira ya saa sita hivi, hivyo nami katika harakati za kumsaidia mpishi wa zamu (msaidizi wa nahodha) kuwasha moto, nikapatwa na gumbizi (kuzunguzungu) na kuanguka chini. Sikuelewa kilichondelea hadi baadaye nilipopata fahamu nikawaona wavuvi wote wamenizunguka huku nahodha akiniuliza ninajisiaje sasa.
"Najisikia vizuri ila nahisi uchovu tu, kwani kimetokea nini?" nilijibu na kuuliza.
Nahodha akaniambia kuwa nilianguka na kusogezwa kibandani na msaidizi wake na nikawa kama nimezimia na kupoteza fahamu, wao waliitwa kuja kunisaidia haraka kwa kunipepea na kunimwagia maji ndipo nikazinduka.
Nikapewa supu ya Samaki aina ya 'Songolo' nikanywa nikapata nguvu kidogo na ugali ukasongwa
wengine wote walikula lakini mimi nilitosheka na supu ya samaki sikujisikia kula tena. Zoezi la jioni walibaki watu watatu pale kambini pamoja nami, yaani nahodha na wasaidizi wake wawili, wavuvi wengine waliendelea kuvua.
Kwakuwa ilikuwa msimu wa 'bamvua' lenye samaki wengi, haikutuchukua zaidi ya siku kumi kujaza
vyombo vyetu vyote samaki aina ya kamba na kaji. Lilifanyika zoezi la ziada kwa ajili ya uvuvi wa maji mengi ili kupata samaki wakubwa kwa njia ya 'mishipi', basi wiki hiyo iliyofuata tulitumia usiku wa kiza kwenda kuvua Jodari, Sehewa, Papa, Chewa na Nguru. Kambini tulikuwa tunawaacha wavuvi wanne wakilinda samaki na kambi kwa ujumla, mimi hawakutaka kuniacha kwa kuhofia nisije nikaanguka tena wao wakiwa mbali.
Zoezi hili la usiku nilikuwa nikilifurahia kwa kuwa hatuingii ndani ya maji, bali tunawasha tu 'karabai' na kuweka chambo kwenye ndoano na kuanza kuvua huku 'mishoto' ikiwa jirani kwa ajili ya 'kuwatuliza' samaki wasumbufu kabla ya kumtoa kwenye ndoano.
Tulipata Jodari wachache, sehewa wengi, nguru wachache, papa mmoja na chewa mkubwa mmoja kwa zoezi zima la wiki hiyo. Chakula Unga kutoka mjini Bagamoyo tulichukuwa wa kutosha wiki nne, lakini Nahodha aliamuru turudi mjini baada ya wiki tatu na nusu kwa kuwa tulishapata mavuno ya kutosha.
***********
Safari ya kurudi ilianza, lakini kwa upande wangu niliona vituko njiani kadha wa kadha, tulianza safari
jioni sana ili tutembee usiku kucha na asubuhi tuwe tumefika. Ilikuwa ni kawaida ya vyombo vyetu kuja 'kutua' maeneo ya pwani ya msikiti wa Ijumaa Bagamoyo "nchi pana", (siku hizi wanapaita kwa Zakaria / Alfazul).
Kituko cha kwanza ni kuona moto mwekundu ukiwaka baharini pasipo na chombo chochote,
awali nilidhani ni wavuvi wenzetu wakivua lakini nilipo muuliza nahoda alinijibu kuwa hapana,
siyo wavuvi, wale ni "vibwengo"
'Wakati nasoma kizuiani, nimesikia simulizi nyingi za vibwengo, leo hatimaye naaza kushuhudia
mubashara', nilijisemea.
Vimbwengo kwa simulizi ni aina fulani ya viumbe ambavyo aghalabu hupatikana maeneo yenye maji mengi mfano wa mabwawa makubwa, mito, maziwa, bahari. Viumbe hivi husemekana vina uwezo wa kujibadilisha muonekano wao, na wakiwa katika umbo la mfano wa mwanadamu basi huwa wafupi. wana uwezo wa kuonekana na kupotea kwa ghafla. hupenda kuwatisha binadamu lakini inasemekana hawana madhara makubwa kwa binadamu.
Inasemekana pia ni aina fulani ya kabila moja ya jamii (specie) ya majini. Sasa ile mioto ilikuwa inaonekana na tunapoikaribia inapotea na kuonekana umbali mwingine.
************
Inaendelea...