Hatimaye Dk. Juma Mwaka ajisalimisha Polisi

Hatimaye Dk. Juma Mwaka ajisalimisha Polisi

Hakuna uhasama Kigwangallah anatimiza wajibu wake.
Sawa asilimia kubwa ya hawa madokta ni wapigaji!Yuko wapi isiack ndondi naye....
Hata hizi tv nazo wanawapa SANA airtime hawa madoktaa.....
Lakini bado Kuna ugomvi ambao ni personnel kati hamis na kigwagala.....na hamis kashapata chanzo cha kumkomoa Dr mwaka
 
Kuibuka kwa watu aina ya kina Dk Mwaka ni viashilia vya udhaifu wa serikali yetu katika kusimamia na kuboresha huduma za afya.....

Wakati serikali kupitia wizara husika wakihangaishana na hao matapeli wa tiba....na

wao hawana budi kujitafakari walipojikwaa il
kuweka mambo sawa.....kinyume na hapo
watakuwa wanatwanga maji kwenye kinu.....
Wanatakiwa wajiulize kwanini wananchi wengi nyakati hizi wanakimbilia tiba mbadala.....!!??




Ukiacha miundombinu mibovu ya huduma za afya vile vile wananchi wanakimbizwa na
huduma mbovu za watendaji kwenye sekta ya afya..........

Baada ya kumalizana na hao matapeli pia
wahusika tuliowapa jukumu la kusimamia afya zetu wajipime wenyewe kuwa wanastahili


kiendelea kuwepo mahali hapo...kulingana na uwajibikaji wao ndio utakuwa mwisho wa hao


matapeli wa tiba wanaochezea kamali afya za waTanzania.........
KWELI KABISA ULICHOSEMA!BAADA YA MWAKA UTAONA ANAIBUKA MTU MWINGINE
 
Sawa asilimia kubwa ya hawa madokta ni wapigaji!Yuko wapi isiack ndondi naye....
Hata hizi tv nazo wanawapa SANA airtime hawa madoktaa.....
Lakini bado Kuna ugomvi ambao ni personnel kati hamis na kigwagala.....na hamis kashapata chanzo cha kumkomoa Dr mwaka
Kwa TV kuwapa airtime si kosa lao maana wao ni wafanya biashara, ili iwepo TV lazima matangazo yawepo hawezi kuyakataa. Cha msingi serikali itoe taratibu na kuwa makini na hawa watu mnaowaita matapeli
 
Nafikiri inabidi nchi hii iendeshwe kwa kutmia sheria na kanuni, kuna wimbi kubwa la watu wanaojiita madaktari wa tiba asili, wameawasaidia watu lakini nje ya taratibu na kanuni za tiba.
 
Mwaka kwa utajiri ulionao sidhani kama Sheria itachukua mkondo wake.!
Mwaka ni ithibati kuwa utapeli unalipa. Manabii feki wanamiliki mali za ajabu, wajanja wajanja kama Lugumi wanapeta kama wapo peponi in short ukitaka kuishi kwa raha kuwa tapeli ndio maana tunayopewa nchi hii.
 
Kama huyo mganga wake huko alipoenda kujificha kamuaminisha hivyo basi ahesabu maumivu
Mganga ni yeye mwenyewe. Haya majanga yote yanakuja baada ya kutosa kaniki na tunguri na kuweka stethoscope shingoni pamoja na kuvaa koti jeupe. Sasa mizimu imenuna. Alitakiwa awe anafanya tiba kwenye kibanda cha makuti.
 
Walianzaga Wakina mama terry,akaja Yule alikuwa na ofisi yake magomeni Jina nmemsahau,akaja baby wa loliondo,ukienda opposite na Hindu mandal Kuna jamaa wana kituo chao nao wanasema wanaponyeshaa watu....Hao dawa zao wanakuambiaa usiweke karibu ya tv ama radio....Haya Kuna Huyu rahabu,akaja Dr Mwaka .......
Mwaka na kigwagala ni uhasama tu....utakuwaa
Ni kweli Mwaka katengeneza hela sanaa kupitia tiba hizi lakini siku zote hawa sijui tuwaite wenye shida ambao wanakwenda huko ndiyo tatizo....
SAHIVI TUNASUBIRIA NANI ATAIBUKAAA BAADA YA DR MWAKA
Mwaka amesaidia wengi sana mimi shuhuda, ajabu sijaona hata mmoja alielalamika kadhurika na tiba za mwaka, chuki ya kipato chake. Mbona babu wa loliondo hakamatwi au kuna ushahidi gani anatibu ukimwi? Kichaa cha serikali ni kushuhulika na mambo ambayo yanweza kujitatua na kuacha mabo ambayo ni lazima wayatatue. Kama dawa za mwaka zingekuwa fake asingepata wagonjwa jamani mbona hesabu rahisi tu?!. Embu washuhulike na mambo ya msingi., ikiwepo kugawa mashamba kwa vijana na si kuwahimiza walime wakati wengi hatuna mashamba, tulime lami?!
 
Sawa asilimia kubwa ya hawa madokta ni wapigaji!Yuko wapi isiack ndondi naye....
Hata hizi tv nazo wanawapa SANA airtime hawa madoktaa.....
Lakini bado Kuna ugomvi ambao ni personnel kati hamis na kigwagala.....na hamis kashapata chanzo cha kumkomoa Dr mwaka
Kweli kabisa kuna uhasama wa kibinafsi, kama kuna shida nilitegemea Ummy mwalim ambae ni waziri na ni mwanamke nae alivalie njuga hili swala la mwaka lakini ni kikwangala tu kwa nini? Hawa wanaojiwekea mabango kwenye miti wametoka sumbawanga mbona ahato agizo nao wachukuliwe hatua?? Nawahakikishia kwa jinsi mwaka alivyosaidia wengi watu wako tayari kwenda kwake kupewa huduma kama wageni, labda wamfunge ila huduma tu ni ngumu kumzuia au wataweka walinzi mtu asiende kwake kumuona?
 
Mwasu@hawa matabibu wana Tibu kwa kubahatisha tu,ni kweli babu wa loliondo,isiack ndondi,mama tery,rahabu na wengineo wote ni fiksi tu.....
Mwaka Sema kapiga hela SANA mpaka hamis kaingiaa jelous na inawezekana Kuna la zaidi ktk beef Lao....
 
View attachment 379395jambazi mwingine huyu hapa anayejiita Dr. Rahabu Lubago, kawaliza wengi na majani ya mipapai eti anatibu vidonda vya tumbo!
Nakumbuka kuna kipindi nilihudhuria kliniki ya Rahabu pale Buguruni, nilimuuliza maswali mengi sana na hakufurahia yale maswali. Hawa watu kwa kweli ni matapeli na wanaumiza sana watu.
 
Back
Top Bottom