Waziri Mkuu Mizengo Pinda akikagua Bajaj ambayo imetengenezwa ili kumudu kazi ya kuzima moto hasa kwenye maeneo yenye barabara nyembamba katika maonesho yaliyoandaliwa na Kampuni ya Spray and Fumigation Services Limited, bungeni Dodoma Alhamisi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
Karne ya 21 tunatumia bajaj kuzima moto! Jameni usanii mwingine haufai, hizi zimamoto zinazobeba zaidi ya lita 30,000 za maji zina shindwa kuzima nyumba moja itakuwaje bajaji ya lita 500 au 1000! Huu si utani jameni?
Nchi hii ni kama haina viongozi mkuu, maana kila siku hatukosi kushangaa, bado bajaji za kubebea kina mama wajawazito. Si mchezo tunaelekea kwenye ujima kwa kasi. Kwa nini barabara ziwe nyembamba kama nyumba zimejengwa kwa kufuata utaratibu. Hii inaonyesha serikali haina mpango wa kuzuia ujenzi wa makazi bila mpangilio.
Mkubwa mzima Pinda anashangaa kitu cha kitoto sijui ninini hicho!...Tangu lini bajaji ikawa zima moto jamani?
Hivi vidudud ni kama vile vya kubebea wajawazito, nadhani aliyewasupply vile ndo huyohuyo kaleta na hivi tena!
Amewashika masikio hawafurukuti!..Ashagundua kuwa ni mazezeta wote!...my hairs!
Wajawazito bajaj, moto bajaj, bado nini sijui... yeye mbona hapandi bajaj, hivi hiyo bajaj ikijaza hicho kitenki chake itatembea kweli, I think these people are trying our patience. kwa hiyo ndio ubunifu huo, kweli kiboko!!! hicho labda wakitumie kuzimia sigara. I wont buy this crap.
Mmepata bei yake ni kiasi gani? serikali imetoa order ya ngapi? inaweza enda kasi kiasi gani? ilikuwa ilishatumika nchi gani? n.k,n.k,n.k. Watu wamepata baraka za mkuu na wamesha tengeneza ulaji, Tanzania bana, naipenda.