Hatimae CHADEMA yafanya kweli katika propaganda ya muda mrefu

Mpangawangu

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2014
Posts
887
Reaction score
965
Chadema yadhihirisha ubaguzi wa kikanda,Sasa
1. Mwenyekiti (Mbowe)-Mkaskazini
2. Katibu mkuu (Slaa)-Mkaskazini
3. Naibu katibu mkuu(Mnyika)-Mk askazini.
4. Mwenyekiti Bawacha (Mdee) -Mkaskazini.
5. Mweka hazina-Mkaskazini

Duuuh,Mwanzo nilijua hoja ya ukanda kwa CHADEMA ni propaganda kumbe ni FACT.

Wale wa kukanusha naombeni mtueleze sifa ya ziada walizonazo watanzania wanaotoka Kaskazini kuliko wanachadema wa kutoka mikoa mingine,la sivyo mnataka tuamini kuwa CHADEMA wenye akili ni watu wa
Kaskazini.
 
Nilikuwa naipenda sana Chadema. Sasa sijui nijiunge na chama gani....!!!!
 
Malizia na akina Prof Safari wa Kaskazini, Said Issa Mohamed ni wa Kaskazini, Salum Mwalimu Juma ni wa Kaskazini, Patrobas ni wa Kaskazini, Hashim ni wa Kaskazini, Hawa Mwaifunga ni wa Kaskazini, Jannet Fussi ni wa Kaskazini, Zeudi ni wa Kaskazini, Rutembeka ni wa Kaskazini.
 
Mtoa mada n saddist! Anawachukia watu wa kaskazini! Mwambie kwenye viongozi wa chama tawala ccm kuna nani kutoka kaskazini hata lowassa walimtoa. Acheni kuhubiri siasa majitaka
 

Mkuu Malova, hiyo ndo dawa ya mapashikuna magamba.
Hayalali bado yanausaka umbea tu.
 
Mkuu Malova, hiyo ndo dawa ya mapashikuna magamba.
Hayalali bado yanausaka umbea tu.
Akili zao ni ndogo sana. Lakini maneno yao hayo ni mikuki ya kuwachoma wenyewe maana watu wa Kaskazini wanahamasishwa zaidi kujiunga na CHADEMA kwa maneno hayo na hivyo kukifanya CHADEMA kitanuke zaidi ma CCM kitakufa zaidi maeneo hayo na popote ambapo wachaga wapo.
 
watu makini sisi kina gogo la shamba tunaoona mbali na kuchambua mambo tunaiona hiyo timu ya chadema list yake ni kali sana kama ni kocha kweli chadema wana kocha mzuri anaejua kupanga list kufuatana na mazoezi uwanjani
 

Wakati mwingine jamani mkiandika vitu hata kama ni vya kishabiki basi angalau muandike kama mna akili. Sasa ili angalau ujaribu kuonesha ulinganifu wa unachotaka kuonesha. Badala ya 'kupick and choose' ungejaribu kuonesha kwa mfano Makamu Mwenyekiti wa pande zote mbili wanatoka wapi; Manaibu wanatoka wapi n.k sasa ukichagua watu wachache tu ni kuabisha kile ambacho Mwenyezi Mungu amekupa - akili.
 
Nilikuwa naipenda sana Chadema. Sasa sijui nijiunge na chama gani....!!!!
nenda na usirudi maana ulitaka vyeo vigawanywe kwa kanda.Kama ime tokea waliokubalika katika uchaguzi wa wanachama wa nchi nzima kwa hiari yao wametoka huko shida iko wapi we zuzu!
 
Mkuu Malova, hiyo ndo dawa ya mapashikuna magamba.
Hayalali bado yanausaka umbea tu.

Prof.Abdallah Jumbe safari amewekwa kama shotu mbele ya gari na kwakuwa Safari anajitambua subilini muone muda simlefu mizengwe itaanza angalia wakaskazini walivyo jipanga yani yule msagaji ndio m/kiti wa akina mama Ukistajabu ya mussa utaona ya firauni
 
Usihangaike na wahuni wa siasa.Mnyika kwa asili yake ni Njombe,mzazi wake alifanyia kazi Mwanza
 
Taifa Stars ivunjwe haraka maana wachezaji wamechaguliwa kutoka mikoa fulani tu (Morogoro, Pwani, Dar na kidogo Zanzibar). Malinzi ondoa huyo kocha kama hamchagui mhaya ktk timu ya taifa. Wanzio hawataki tuangalie uwezo bali ukabila, udini na ukanda. Kama ww jina kuna Mrisho, Ngurumbi, Kawambwa, Simba, Chui, Kabati, Kijiko wewe ni wa kwetu kama sio waziri basi Mkuu Wilaya ya Korogwe. Ukikosa nenda ukawe polisi au uhamiaji.
 

najua hujasoma ila jitahidi kutumia akili katika post zako. watu wa aina yenu ndio mlio shusha hadhi ya JF.nakushauri nenda facebook au instagram ndio kuna watu wa aina yako wengi,JF is meant only for GREAT THINKERS.

CHADEMA wamefanya uchaguzi na wapiga kura wametoka pande zote za Nchi hii, na waliochaguliwa hakuna anae tiliwa shaka kuwa amehonga au kuingia kwa mizengwe iweje wewe zumbukuku unakuja kutuletea upuuzi wako hapa? tumia akili hata kama unalipwa ili USITUMIE AKILI.
 
Nilikuwa naipenda sana Chadema. Sasa sijui nijiunge na chama gani....!!!!

Kwa nini hukugombea ili uone kama wanaopitishwa ni wa kanda hiyo na siyo kwa kujali umahiri wa waliogombea!
 
Ulitaka uchaguliwe wewe!!!!!Pumbav!!!Hii dhana ya ubaguzi mnapeenda sana eeeee!!!!!!!Inawauma sana kusikia Mbowe na Slaa wamerudi uongozini!!!!If you can fight against us then you have to join us
 
Hii single ya ukanda na ukaskazini ilishabugi siku nyingi tu. Kuna manaibu katibu wakuu wawili. Umeamua kuandika mmoja tu.
 
respect..............
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…