Naomba tuwaheshimu single Mums jamani please! Kuna factor nyingi zinazosababisha mtu awe single mother. Mbona single father wapo wengi tu lakini wenzetu hawawapondi single fathers? Sasa iweje mwanaume unaponda single mothers? HESHIMA NI KITU CHA BURE.....huwezi kwenda dukani ukanunua heshima....jiheshimuni WAVULANA tafadhali.
By the way, most of single mothers are best wives.....sababu ni kuwa wanajua uhalisia wa maisha ya mahusiano na mikiki yote ya kutunza mtoto au watoto. Hivyo inapotokea akampata mwanaume mwenye upendo wa kweli daima huwa wanajitoa haswa na huonyesha mapenzi ya dhati. Wapo waliokuwa single mothers na leo wana maisha ya furaha, amani na upendo wa hali ya juu katika ndoa zao na wengine wamekuwa wamama wa mfano katika jamii inayowazunguka.
NB: Mvulana yeyote yule ambaye ana umri wa miaka chini ya 30 (mostly wanachuo/wanafunzi) ndio wanaongoza kuponda single mothers; but atleast Wanaume kuanzia 30 years plus huwa na heshima sana kwa hawa dada zetu single mothers.
Tuelewe ya kwamba mdada au mwanamke kuwa single mother si dhambi....ni MAPITO TU YA MAISHA HAPA DUNIANI (sote tu wasafiri katika hii dunia na tunahitaji ....na wao wanahitaji kupendwa kama wewe unavyotaka kupendwa). Acha dharau.
Mwisho, kama yupo single mother, graduate wa chuo kikuu (bachelor degree holder etc) ambaye hajazidi miaka 30 na anahitaji mwanaume wa maisha yake; naomba ani-PM tafadhali. Naamini ipo siku katika maisha yake atakuja kutoa ushuhuda hapa kwamba kuwa single mother sio DHAMBI.
#RESPECT_TO_ALL_SINGLEMOTHER