GeniusBrain
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 4,315
- 306
Na Waandishi Wetu
Kwa namna ya kipekee, gwiji wa unajimu barani Afrika, marehemu Sheikh Yahya Hussein aliyefariki dunia Ijumaa iliyopita, hatasahaulika kutokana na historia yake.
Umati wa kihistoria uliojitokeza kwenda kumhifadhi kwenye nyumba yake ya dawamu, juzi (Jumamosi) na msisimko wenye hadhi ya kitaifa ni pointi nyingine iliyoacha gumzo la kukumbukwa.
http://api.ning.com/files/cXoyaNxi7...MaXoFJIhoMO5Paj8MoI7PY*sqjHz6G2ZKl1y-*-/2.jpgMwili wa marehemu Sheikh Yahya, ulisaliwa nje nyumbani kwake, Magomeni, baadaye ulipelekwa Msikiti wa Manyema, Kariakoo kwa ajili ya sala nyingine kabla ya kuzikwa kwenye makaburi ya Tambaza, Dar es Salaam.
Idadi kubwa ya watu waliokuwepo, iliizidi nguvu serikali ambayo ilipanga kuwe na msafara wa pikipiki na magari kuelekea Msikiti wa Manyema.
http://api.ning.com/files/6q1gQVNn*...ZzqSPZS4ZDxDXCH4ZTuAm2cbl3aspx2n0TMbmuB/1.jpgAwali, ilipangwa kuwa waombolezaji watembea kwa miguu wangebeba mwili wa marehemu katika jeneza kutoka Magomeni Mikumi hadi Usalama (mataa) ambako ungepakiwa kwenye gari maalumu litakaloongozwa na trafiki mwenye pikipiki ya kingora.
Hata hivyo, watu hao waligoma walipofika Usalama, walikataa kumpandisha kwenye gari na kuubeba kwa miguu mpaka Msikiti wa Manyema na baadaye waliuchukua hadi Tambaza.
Walipokuwa wanagoma, watu hao walipaza sauti kuwa hawawezi kumpandisha Sheikh wao kwenye gari, wakati uwezo wa kumbeba wanao.
http://api.ning.com/files/QdPaIG2cD...dN*PPXM9SmFku5M2baQmuuIX6u**Mjq/IMG_92362.jpgKAULI YA MWISHO
Sheikh Yahya, alifariki dunia Ijumaa iliyopita njiani akipelekwa Hospitali ya Mt. Mkombozi, Morocco, Kinondoni, Dar es Salaam.
Hata hivyo, Sheikh ambaye alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya moyo kwa muda mrefu, siku hiyo aliamka salama na kuanza kazi ya kuwahudumia wateja wake (kuwatibu) kama kawaida.
Gazeti hili limeelezwa kuwa watu wa kwanza kufika ofisini kwake ni 12 ambao aliwahudumia wote.
http://api.ning.com/files/CuiJgph4S...osmyQ06Dh7rTwU6*cRfvmlE5jk6P*Pfs/IMG_9179.jpgImeelezwa kuwa mtu wa mwisho kuhudumiwa na Sheikh ni mwanamke anayeitwa Winnie.
Habari zinasema kuwa baada ya kumtibu Winnie, Sheikh aliwaambia wasaidizi wake kuwa amemaliza kazi na kuwataka wampeleke hospitali ambapo alifariki dunia akiwa kwenye gari njiani.
VIONGOZI SIMANZI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na makamu wake, Dk. Mohamed Gharib Bilal walihudhuria mazishi hayo.
http://api.ning.com/files/lsFTYHebH...YWTdwCAMzg5su01AoDX9856I2DgN1*i/IMG_91852.jpgDk. Bilal alikuwa wa kanza kufika, kwani aliwasili nyumbani kwa marehemu saa 4:00 asubuhi na baada ya kutoa salamu za rambirambi aliondoka.
Aidha, Rais Kikwete alikuwa wa kwanza kufika makaburini, kwani umati ukiwa na mwili wa marehemu ulipofika, ulikuta ameshatangulia.
Viongozi wengine waliohudhuria mazishi ya mnajimu huyo ni Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa UPD, John Cheyo na Mchungaji wa Kanisa la GRC, Anthony Lusekelo Mzee wa Upako.
http://api.ning.com/files/HmgmWdOeo...Q-saQ9*GffZF*5os1nmG7c6GpEKcJB7t/IMG_9196.jpgViongozi hao kwa nyakati tofauti walisema Sheikh Yahya alikuwa mtu wa watu, mpenda amani na aliyekuwa akihimiza mshikamano wa kitaifa bila kujali itikadi za kisiasa.
Wengine waliokuwepo ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa kipolisi wa Kinondoni, Charles Kenyela, Afisa wa ngazi ya juu wa polisi makao makuu, Jamal Rwambow, Mbunge wa Ilala, Musa Zungu, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, Mbunge wa Namtumbo, Vita Kawawa, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika na Mbunge wa Wawi (CUF), Hamadi Rashid.
http://api.ning.com/files/wY*r8ECsV...aYEid8dHbq04DWuhgKuloLxqmH6O8R9/IMG_92002.jpgVURUGU
Vurugu zilizotokea ni zile ambazo ziliifanya serikali izidiwe nguvu na wananchi ambao walishindwa kufuata utaratibu uliowekwa wa kumsindikiza kaburini kiongozi huyo wa dini.
Mwili wa marehemu Sheikh Yahya ulipofika eneo la Usalama karibu Hoteli ya Travertine, kulitokea mabishano kati ya waombolezaji watembea kwa miguu na mwenyekiti wa mazishi, Sheikh Alhaj Musa Salum ambaye ni Sheikh Mkuu wa Dar es Salaam.
http://api.ning.com/files/hL1O-vOJ3...hmhZgRS9F930MrcDpHq3FIfW*3nyf8b/IMG_92122.jpgSheikh Salum aliwataka waombolezaji kufuata utaratibu uliopangwa lakini waligoma, hivyo kuibua mabishano makubwa ikiwemo kunyanganyana mwili wa marehemu.
Mabishano hayo yalichukua dakika tano, baadaye watembea kwa miguu walishinda na kuufikisha mwili wa marehemu kwenye Msikiti wa Manyema na kupokewa na Imamu wake, Sheikh Ahmed Jongo.
Baada ya sala ya marehemu, ilitakiwa mwili uwekwe kwenye gari lakini wananchi waligoma, hivyo waliubeba hadi Tambaza.
http://api.ning.com/files/Rve-*h*i*...P6gZZNqV0zQHAxnqnahCRfUqVC62Zmt/IMG_92232.jpgKAULI YA SHEIKH SALUM
Katika kumuweka sawa Rais Kikwete, mara tu mwili wa marehemu ulipofikishwa makaburini, Sheikh Salum alisema kwa kutumia kipaza sauti huku akimwangalia kiongozi huyo wa nchi:
Mheshimiwa Rais, Sheikh Yahya Hussein alikuwa mtu wa vijana, anapokaa alikuwa akizungukwa na vijana japokuwa alikuwa mtu mzima. Ndiyo maana vijana hawa wamelibeba jeneza hili kutoka nyumbani kwake hadi hapa makaburini licha ya kuwa kulikuwa na gari maalumu la kubeba mwili wa sheikh wetu.
http://api.ning.com/files/-rtCHQZ-j...B8-eH5GMCwnnT8uMA1w7u1LIUcFwWfq/IMG_92292.jpgMATUKIO YA KUKUMBUKWA
Katibu wa Halmashauri Kuu CCM (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alipopata nafasi ya kuzungumza kwenye mazishi hayo, alisema, Sheikh Yahya hatasahaulika kutokana na utabiri wake uliokuwa ukihimiza amani na mshikamano.
Alisema, Sheikh Yahya alitabiri CCM na CUF kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na baadaye ikawa hivyo.
http://api.ning.com/files/QdPaIG2cD...Um04PcRo2tg-fv-aH7dpz1yFBYETaRk/IMG_92152.jpgUtabiri mwingine wa Sheikh Yahya ni ule ambao alisema Rais Benjamin Mkapa angeongezewa muda wa kutawala mwaka 2005 na kweli ilitokea hivyo. Hii ilisababisha wanasiasa wengi kukiri kuwa hakuwa mtu wa kawaida.
Aidha, Sheikh Yahya Hussein aliwahi kutabiri kuwa uchaguzi wa Zanzibar wa mwaka 2000 utarudiwa na ikawa hivyo.
http://api.ning.com/files/-maJWYYGq...u9KqLy4ZBIFJnYD7QqX9IYbTU27EalFAPgnxpzO/a.JPGMnajimu huyo aliwahi kutabiri kesi ya mwanamuziki Nguza Viking Babu Seya na watoto wake watatu waliofungwa jela maisha wataachiwa huru.
Walipokata rufaa, watoto wawili wa Babu Seya, Nguza Mbangu na Francis Nguza waliachiwa huru na kuacha mkongwe huyo wa muziki wa dansi akiendelea kutumikia kifungo cha maisha jela na mwanaye mmoja, Johnson Nguza Papii Kocha.
http://api.ning.com/files/2BgXwufyD...5hvfFw4LOhL6-ovcFZKiCzpa0Ysi-2IaQfNIuY8/b.JPGBaada ya hukumu hiyo, sheikh Yahya alisema: Utabiri wangu haukukosea kabisa, nimepata nusu na nimefeli nusu, lakini naona kinyota Nguza yupo huru, tusubiri mbele ya safari.
Mnajimu huyo aliwahi pia kumtabiria aliyekuwa Rais wa Uganda Dikteta Iddi Amini kupinduliwa baada ya miezi sita alipokutana naye jijini Kampala na ikawa hivyo baada ya kupigwa na majeshi ya Tanzania.
http://api.ning.com/files/CuiJgph4S...VWMxeLcLRl3qK-JqAHA3K0nGjXfRqcllO-c3lbF/c.JPGSheikh Yahya, anakumbukwa na Wakenya baada kutabiri kuwa waziri mmoja wa nchi hiyo angepigwa risasi akiwa karibu na duka la dawa na ikawa hivyo baada ya Tom Mboya kuuawa kama alivyosema.
Mwaka 2002, alitabiri kuwa atakayeshinda urais Kenya atakuwa na sauti mbuzi na ataapishwa akiwa kwenye kiti cha magurudumu (wheel chair) na ikawa kweli, kwani alishinda Rais Mwai Kibaki na kula kiapo siku chache baada ya ajali ya gari.
http://api.ning.com/files/d1j3CHeta...WJwnq6IDODXuXQDLs8MtN9qW3e9qnNfcG5582Z*/d.JPGAidha, aliwatabiria Rais Kikwete kushinda urais, Dk. Ali Mohamed Shein kuwa Makamu wa Rais, akatabiri vifo vya aliyekuwa Makamu wa Rais, Dk. Omar Ali Juma na Waziri Mkuu Mstaafu, Rashid Mfaume
Kwa namna ya kipekee, gwiji wa unajimu barani Afrika, marehemu Sheikh Yahya Hussein aliyefariki dunia Ijumaa iliyopita, hatasahaulika kutokana na historia yake.
Umati wa kihistoria uliojitokeza kwenda kumhifadhi kwenye nyumba yake ya dawamu, juzi (Jumamosi) na msisimko wenye hadhi ya kitaifa ni pointi nyingine iliyoacha gumzo la kukumbukwa.
http://api.ning.com/files/cXoyaNxi7...MaXoFJIhoMO5Paj8MoI7PY*sqjHz6G2ZKl1y-*-/2.jpgMwili wa marehemu Sheikh Yahya, ulisaliwa nje nyumbani kwake, Magomeni, baadaye ulipelekwa Msikiti wa Manyema, Kariakoo kwa ajili ya sala nyingine kabla ya kuzikwa kwenye makaburi ya Tambaza, Dar es Salaam.
Idadi kubwa ya watu waliokuwepo, iliizidi nguvu serikali ambayo ilipanga kuwe na msafara wa pikipiki na magari kuelekea Msikiti wa Manyema.
http://api.ning.com/files/6q1gQVNn*...ZzqSPZS4ZDxDXCH4ZTuAm2cbl3aspx2n0TMbmuB/1.jpgAwali, ilipangwa kuwa waombolezaji watembea kwa miguu wangebeba mwili wa marehemu katika jeneza kutoka Magomeni Mikumi hadi Usalama (mataa) ambako ungepakiwa kwenye gari maalumu litakaloongozwa na trafiki mwenye pikipiki ya kingora.
Hata hivyo, watu hao waligoma walipofika Usalama, walikataa kumpandisha kwenye gari na kuubeba kwa miguu mpaka Msikiti wa Manyema na baadaye waliuchukua hadi Tambaza.
Walipokuwa wanagoma, watu hao walipaza sauti kuwa hawawezi kumpandisha Sheikh wao kwenye gari, wakati uwezo wa kumbeba wanao.
http://api.ning.com/files/QdPaIG2cD...dN*PPXM9SmFku5M2baQmuuIX6u**Mjq/IMG_92362.jpgKAULI YA MWISHO
Sheikh Yahya, alifariki dunia Ijumaa iliyopita njiani akipelekwa Hospitali ya Mt. Mkombozi, Morocco, Kinondoni, Dar es Salaam.
Hata hivyo, Sheikh ambaye alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya moyo kwa muda mrefu, siku hiyo aliamka salama na kuanza kazi ya kuwahudumia wateja wake (kuwatibu) kama kawaida.
Gazeti hili limeelezwa kuwa watu wa kwanza kufika ofisini kwake ni 12 ambao aliwahudumia wote.
http://api.ning.com/files/CuiJgph4S...osmyQ06Dh7rTwU6*cRfvmlE5jk6P*Pfs/IMG_9179.jpgImeelezwa kuwa mtu wa mwisho kuhudumiwa na Sheikh ni mwanamke anayeitwa Winnie.
Habari zinasema kuwa baada ya kumtibu Winnie, Sheikh aliwaambia wasaidizi wake kuwa amemaliza kazi na kuwataka wampeleke hospitali ambapo alifariki dunia akiwa kwenye gari njiani.
VIONGOZI SIMANZI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na makamu wake, Dk. Mohamed Gharib Bilal walihudhuria mazishi hayo.
http://api.ning.com/files/lsFTYHebH...YWTdwCAMzg5su01AoDX9856I2DgN1*i/IMG_91852.jpgDk. Bilal alikuwa wa kanza kufika, kwani aliwasili nyumbani kwa marehemu saa 4:00 asubuhi na baada ya kutoa salamu za rambirambi aliondoka.
Aidha, Rais Kikwete alikuwa wa kwanza kufika makaburini, kwani umati ukiwa na mwili wa marehemu ulipofika, ulikuta ameshatangulia.
Viongozi wengine waliohudhuria mazishi ya mnajimu huyo ni Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa UPD, John Cheyo na Mchungaji wa Kanisa la GRC, Anthony Lusekelo Mzee wa Upako.
http://api.ning.com/files/HmgmWdOeo...Q-saQ9*GffZF*5os1nmG7c6GpEKcJB7t/IMG_9196.jpgViongozi hao kwa nyakati tofauti walisema Sheikh Yahya alikuwa mtu wa watu, mpenda amani na aliyekuwa akihimiza mshikamano wa kitaifa bila kujali itikadi za kisiasa.
Wengine waliokuwepo ni Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa kipolisi wa Kinondoni, Charles Kenyela, Afisa wa ngazi ya juu wa polisi makao makuu, Jamal Rwambow, Mbunge wa Ilala, Musa Zungu, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, Mbunge wa Namtumbo, Vita Kawawa, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika na Mbunge wa Wawi (CUF), Hamadi Rashid.
http://api.ning.com/files/wY*r8ECsV...aYEid8dHbq04DWuhgKuloLxqmH6O8R9/IMG_92002.jpgVURUGU
Vurugu zilizotokea ni zile ambazo ziliifanya serikali izidiwe nguvu na wananchi ambao walishindwa kufuata utaratibu uliowekwa wa kumsindikiza kaburini kiongozi huyo wa dini.
Mwili wa marehemu Sheikh Yahya ulipofika eneo la Usalama karibu Hoteli ya Travertine, kulitokea mabishano kati ya waombolezaji watembea kwa miguu na mwenyekiti wa mazishi, Sheikh Alhaj Musa Salum ambaye ni Sheikh Mkuu wa Dar es Salaam.
http://api.ning.com/files/hL1O-vOJ3...hmhZgRS9F930MrcDpHq3FIfW*3nyf8b/IMG_92122.jpgSheikh Salum aliwataka waombolezaji kufuata utaratibu uliopangwa lakini waligoma, hivyo kuibua mabishano makubwa ikiwemo kunyanganyana mwili wa marehemu.
Mabishano hayo yalichukua dakika tano, baadaye watembea kwa miguu walishinda na kuufikisha mwili wa marehemu kwenye Msikiti wa Manyema na kupokewa na Imamu wake, Sheikh Ahmed Jongo.
Baada ya sala ya marehemu, ilitakiwa mwili uwekwe kwenye gari lakini wananchi waligoma, hivyo waliubeba hadi Tambaza.
http://api.ning.com/files/Rve-*h*i*...P6gZZNqV0zQHAxnqnahCRfUqVC62Zmt/IMG_92232.jpgKAULI YA SHEIKH SALUM
Katika kumuweka sawa Rais Kikwete, mara tu mwili wa marehemu ulipofikishwa makaburini, Sheikh Salum alisema kwa kutumia kipaza sauti huku akimwangalia kiongozi huyo wa nchi:
Mheshimiwa Rais, Sheikh Yahya Hussein alikuwa mtu wa vijana, anapokaa alikuwa akizungukwa na vijana japokuwa alikuwa mtu mzima. Ndiyo maana vijana hawa wamelibeba jeneza hili kutoka nyumbani kwake hadi hapa makaburini licha ya kuwa kulikuwa na gari maalumu la kubeba mwili wa sheikh wetu.
http://api.ning.com/files/-rtCHQZ-j...B8-eH5GMCwnnT8uMA1w7u1LIUcFwWfq/IMG_92292.jpgMATUKIO YA KUKUMBUKWA
Katibu wa Halmashauri Kuu CCM (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alipopata nafasi ya kuzungumza kwenye mazishi hayo, alisema, Sheikh Yahya hatasahaulika kutokana na utabiri wake uliokuwa ukihimiza amani na mshikamano.
Alisema, Sheikh Yahya alitabiri CCM na CUF kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na baadaye ikawa hivyo.
http://api.ning.com/files/QdPaIG2cD...Um04PcRo2tg-fv-aH7dpz1yFBYETaRk/IMG_92152.jpgUtabiri mwingine wa Sheikh Yahya ni ule ambao alisema Rais Benjamin Mkapa angeongezewa muda wa kutawala mwaka 2005 na kweli ilitokea hivyo. Hii ilisababisha wanasiasa wengi kukiri kuwa hakuwa mtu wa kawaida.
Aidha, Sheikh Yahya Hussein aliwahi kutabiri kuwa uchaguzi wa Zanzibar wa mwaka 2000 utarudiwa na ikawa hivyo.
http://api.ning.com/files/-maJWYYGq...u9KqLy4ZBIFJnYD7QqX9IYbTU27EalFAPgnxpzO/a.JPGMnajimu huyo aliwahi kutabiri kesi ya mwanamuziki Nguza Viking Babu Seya na watoto wake watatu waliofungwa jela maisha wataachiwa huru.
Walipokata rufaa, watoto wawili wa Babu Seya, Nguza Mbangu na Francis Nguza waliachiwa huru na kuacha mkongwe huyo wa muziki wa dansi akiendelea kutumikia kifungo cha maisha jela na mwanaye mmoja, Johnson Nguza Papii Kocha.
http://api.ning.com/files/2BgXwufyD...5hvfFw4LOhL6-ovcFZKiCzpa0Ysi-2IaQfNIuY8/b.JPGBaada ya hukumu hiyo, sheikh Yahya alisema: Utabiri wangu haukukosea kabisa, nimepata nusu na nimefeli nusu, lakini naona kinyota Nguza yupo huru, tusubiri mbele ya safari.
Mnajimu huyo aliwahi pia kumtabiria aliyekuwa Rais wa Uganda Dikteta Iddi Amini kupinduliwa baada ya miezi sita alipokutana naye jijini Kampala na ikawa hivyo baada ya kupigwa na majeshi ya Tanzania.
http://api.ning.com/files/CuiJgph4S...VWMxeLcLRl3qK-JqAHA3K0nGjXfRqcllO-c3lbF/c.JPGSheikh Yahya, anakumbukwa na Wakenya baada kutabiri kuwa waziri mmoja wa nchi hiyo angepigwa risasi akiwa karibu na duka la dawa na ikawa hivyo baada ya Tom Mboya kuuawa kama alivyosema.
Mwaka 2002, alitabiri kuwa atakayeshinda urais Kenya atakuwa na sauti mbuzi na ataapishwa akiwa kwenye kiti cha magurudumu (wheel chair) na ikawa kweli, kwani alishinda Rais Mwai Kibaki na kula kiapo siku chache baada ya ajali ya gari.
http://api.ning.com/files/d1j3CHeta...WJwnq6IDODXuXQDLs8MtN9qW3e9qnNfcG5582Z*/d.JPGAidha, aliwatabiria Rais Kikwete kushinda urais, Dk. Ali Mohamed Shein kuwa Makamu wa Rais, akatabiri vifo vya aliyekuwa Makamu wa Rais, Dk. Omar Ali Juma na Waziri Mkuu Mstaafu, Rashid Mfaume