Hata nikiongea kawaida wanasema nafoka

Hata nikiongea kawaida wanasema nafoka

zee_latown

JF-Expert Member
Joined
Feb 21, 2026
Posts
523
Reaction score
927
Habarini ndugu Wanabodi wa JF!

Naenda kwenye kiini cha mada moja kwa moja.

Nina changamoto... hata nikiongea kwa upole na kawaida, wasikilizaji wangu wanadai kuwa nimechukia na nafoka,, yaani nikiongea seriously mfano kwenye jambo nyeti na la msingi, naonekana kama nafoka. Hali hii inanitatiza sana, ukizingatia mimi kiasili ni mtu muungwana na ninayependa watu.

Kuna wakati huko zamani, nilikuwa naongea na bosi wangu... sasa wafanyakazi wenzangu wa pemebni walikuwa wanasikiliza maongezi yetu.. nilipomaliza wakaja wakanishangaa sana wakisema hivi siogopi kumfokea bosi? hili liliniuma sana na ukizingatia mimi nilikuwa naongea kwa upole mno ila in a serious way,kwa sababu jambo lenyewe lilikuwa serious pia

Sasa ninahofia sana hii hali... huenda ikanieletea shida mbeleni hasa ukizingatia kuna nyakati huwa naongea na baadhi ya viongozi wakubwa wa serikali... isije kuonekana nafoka na nimepandisha sauti, ilhali mimi naona naongea kawaida.

Nafahamu humu kuna wenye uwezo wa kunisaidia utatuzi wa hili. naomba msaada wa hali na mali tafadhali.
natanguliza shukrani zangu.
 
mkuu
mimi pia nipo kama wewe.
nimechumguza nimegundua nimerithi kwa baba yangu.

mzee wangu ana tone ya ukali hata kama
jambo ni la kawaida, nilikua nachukia sana
zamani the way alivyokua anaongea na mimi.

sasa nimekuja kugundua mimi pia
nina ile tone yake baada ya kuambiwa na watu.

najitahidi sana nisiwe naongea kwa namna hiyo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom