Hassan Abas Msemaji wa Serikali na mwanamkakati wa kujipatia shibe kwa nafasi aliyopewa

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Tunamshuhudia msemaji wa serikali akizunguka mikoa ya nchi hii kila mkoa akiingia kwenye redio za eneo hilo na kuinadi serikali.

Anatumia gharama kubwa za safari hizo na kujilipa posho zisizo za lazima. Per diem yake ni kubwa na wale wanaofuatana nae wanalipwa pia, madereva na watu kadhaa anaoongozana nao kwenye msurulu wake.

Tunajiuliza kwanini Abbas anazunguka kila kona kufanya kampeni za kipropaganda kunadi maendeleo anayoyaita yaliyofanywa na JPM kwa miaka mitatu?

Anajaribu kuhubiri mno JPM anachokifanya, anaweka ushawishi kwenye maendeleo, yaani kuwaambia wananchi ni nini JPM kafanya.

Hivi maendeleo ya kweli yanahitaji airtime ili tuyaone? Kwani maendeleo yanataka mtu akae studio aanze kuyataja moja mpaka la mwisho ndio tuelewe? Maendeleo ni kitu hai na halisi, hayahitaji hesabu za kikokotoo ni swala la udhihiriko halisi.

Serikali ya awamu hii imefanya vitu vibaya mpaka imeamua kujikita kua serikali Ongo kuwahitokea nchini.

Kwani kama lengo ni kuongea na redio, kwanini asingeenda kwenye redio kama Clouds na nyinginezo zenye coverage kubwa na kusemea huko huko alipo na nchi nzima ikajua.

Cha ajabu kaomba fungu la kuzunguka nchi nzima akaongee na redio za mikoani ambazo hata coverage zake ni hafifu. Kikubwa alipwe mamilioni ya safari.

Abbas hakuna cha maana kimefanywa na serikali hii hasa kwa kuyagusa maisha ya mtu masikini moja kwa moja. Zaidi ya kuzindua majengo na madaraja, ile hali watu wanakosa kula wanakosa kusomesha watoto wao elimu za juu na elimu za uhakika.

Watu wanakosa kazi na haki kua ngumu, watu wanakandamizwa na kodi za TRA mpaka wanaamua kufunga biashara kila siku.

Hebu achaneni na siasa za North Korea za kipuuzi, mje na akili za kuiendeleza nchi sio kujiendeleza nyie na chama chenu. Mnaingia maofisi ya umma mkiwa masikini mnatoka mkiwa matajiri wakubwa na masikini wamezidi kua kapuku wakutupwa.

Serikali inapofanya maendeleo haihitaji kupayuka payuka, kwakua maendeleo hai hayajifichi yanaonekana wazi wazi, kuanzia kwa watu mpaka kwa miji yao.
 
Hii ni aibu kwa taifa.
Yaani watu hawaoni alichokifanya Rais?
Njaa mbaya sana inakufanya ufiche ukweli ili tu ulizishe tumbo
 
Toka hii serikali ya awamu ya tano ianza kukwapua pesa za wawanya biashara kwa nguvu sina hamu nayo. Tumerudishwa nyuma miaka 40. Kama una pesa bank za ndani ya nchi kuanzia mil 50 na kuendelea jiandae kisaikologia kunyang'anywa 18% hadi 25% ya hizo pesa bila hiari yako.
Acha sote tosome namba!
 
Leo nilikuwa namsikiliza hapa kili Fm anaongea pumba pumba tu kama za bosi wake kichaa jiwe mtukufu. Leo kaulizwa kwa nini kahawa Kilimanjaro ilikufa na KNCU yeye akabaki anabung'aa bung'aa kama amefumaniwa mara wanaenda kuifufua mara kilimo cha KOKOA mbeya mazao yameuzwa kwa shilingi 3000. Yaani unaulizwa Moshi unajibu Mbeya.

Kaulizwa swala la serikali inunue nayo kahawa kulikwepa hilo swali, bado dawa hospitalini hakuna kaulizwa eti akampigia mtu wa bima on air. Yaani hawa jamaa ni mapoyoyo. Ni kama vile jiwe alivyofanya pale UDSM eti anaingia kama sio mtoa mada kumbe ni mpango wake.

Hawa jamaa waseme kwamba nchi imewashinda maana mmejaa kipropaganda tu. Mara mseme kwamba Michikichi walikuja kuchukuwa hapa tz alafu ndio nchi ya mwisho kuzalisha Michikichi. nchi hii ccm ndo shida
 
Mbona Mwenyekiti wenu anatumia ruzuku kunywa juisi Dubai hadi mnashindwa kuwalipa mawakili
Mkuu ni lini utakuwa na akiri? Unataka kusema Mwenyekiti wa upande ule akinya njia na wakwenu atakunya njiani?
Ni aibu sana serikali ya Tanzania kutetewa na watu wajinga kama wewe
 
Dawa imeingia... wacha watu waelezwe... jaman Zitoo Ester Bulaya Mnyika na wengine mnaowaita viongozi kila siku kwenda kwenye media na kufanya mikutano na waandishi wa habari kuongea wanayoona ni mabaya haya nyie mbona hamsemi? Ila mtu akienda kueleza utekelezaji na makubwa yaliyofanyika inakuwa ni shida.... hebu muda mwingine watanzania tuweke uwanja sawa.... #WACHADAWAIINGIE...ACHENI AWAMU YA TANO IFANYE KAZI... Tuliokosa tujipange 2020 kama tutaweza
 
Mbona Mwenyekiti wenu anatumia ruzuku kunywa juisi Dubai hadi mnashindwa kuwalipa mawakili
Wakili gani aliyelalamika kuwa hajalipwa?? Useme tu kwamba watumishi wa umma wamezurumiwa na liccm .hii hapa list ya viongozi makatili na wauaji: 1.rais. 2.makamu wa rais.
3.waziri mkuu.
4.mawaziri wote.
5.wabunge wote wa ccm.
6.katibu mkuu wa chama.
7.katibu mwenezi wa ccm.
8.uviccm.
9.jumuiya ya wazazi ccm.
10.rais wa awamu ya pili.
11.rais wa awamu ya tatu.
12.rasi wa awamu ya nne.
13.jeshi la polisi.
14.bashite.
15.spika wa bunge.
 
9 Dec 2018
Msemaji wa Serikali, Dkt. Hassan Abasi amefunguka kuhusiana na kitendo kinachodaiwa kufanywa na Mwanaharakati huru Cyprian Musiba cha kuwatuhumu viongozi na wanasiasa katika masakata mbalimbali na kusema kuwa sio msaidizi wake na hatumwi na mtu yeyote kuzungumza

Hapa Dr. Hassan Abbasi anaonekana analiogopa gazeti la Tanzanite maana anajua linatumiwa na serikali ya awamu ya tano kufanya kampeni chafu
 
Bnafc Raisi wetu amefanya mambo mengi makubwa na mazr ila kiukweli hayaaksi maisha yetu watu wa chini hapo ndo kuna shida mfno unaponunua ndege ni kitu kizr ila cc watu wa chini haitunufaishi ni wale wazito tu, cc tukisikia bohari ya dawa inataka kuctisha huduma kwa kuidai serikali ni hatari maana cc hatuwezi enda India.
 
Acheni mbwembwe jamani. . . Msemaji wa serikali anaboss wake bana, lazima amemueleza na amejustify ni kitu gani anataka kufanya katika ziara hizo za mikoani na boss wake akaapprove. Haya wewe kinachokuuma ni nini hasa? Ni yeye kufanya hiyo kazi yake au kuna kingine?

Hivi kazi ya msemaji wa serikali unaifahamu kweli au unahisi? Hichi anachokifanya saiv ni kazi yake 100%, wacha aendelee kufanya. . . .anayoyatangaza yanaweza yakawa yanafahamika ila sio kila mtu anayafahamu undani wake ambapo ndio patamu mtu akijua. Wanasema "najua wajua lakini nataka kukujuza zaidi"
 
Back
Top Bottom