Kwa watu ambao ni very matured
Ndio inayovunjika mwanzo kabla ya kukaa muda mwingi, kupata watoto na kuchuma mali ina afadhali kuliko kinyume chake.
Imagine unapanda bus la kwenda umbali mrefu then linaharibika katikati ya safari au linaharibika mwanzoni mwa safari ungechakua kipi?
Tatizo la sisi ambao hatufurahii ndoa zetu na sisi ambao hatujapata wenza na sisi tuliokosa pesa za harusi na sisi ambao harusi zetu hazikufana ndio tunajifanya kushangaa huku tukifurahia haya mambo ya ndoa kuvunjika mwanzoni. Ila kiuhalisia ni ndoa nyingi sana zinavunjika zikiwa zimedumu na wanandoa wakiwa wameshapata watoto na kuchuma mali nyingi na hili linasababisha hadi kuondoa uhai wa baadhi yetu.
N.B Ukiona au ukijipata hujaolewa au kuoa na umri umeenda usianze kusingizia ndoa zinavunjika na kutolea mifano huku ukijua huwezi hata kufanya ya kwako na kuivunja.
Mifano ya watu waliooana na ndoa zao zikadumu kwa furaha zipo nyingi sana na zipo pia ndoa chache zilizofungwa na kuvunjika mwanzoni au mbele ya safari. Tuliza akili yako uolewe achana kurukaruka uolewe. Usitumie mifano ya walioshindwa. Ni sawa na kupata pesa sio kitu rahisi ila kuna watu wanachukua risk na wanafanikiwa.
Sent using
Jamii Forums mobile app