Harry Belafonte na Hamza Aziz

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,922
30,271
HARRY BELAFONTE NA HAMZA AZIZ
Hamza Aziz kazaliwa Mtaa wa Kipata mtaa ambao mimi nimezaliwa.

Babu yangu Salum Abdalah alikuwa na nyumba Mtaa wa Mbaruku jirani na nyumba ya Aziz Ali baba yake Hamza na Dossa Aziz.

Kwa ajili hii Hamza Aziz wamejuana na baba yangu toka udogoni kwao.

Hamza Aziz kwangu alikuwa baba na rafiki na tukizungumza mengi sana hadi alipotangulia mbele ya haki tulikuwa hivi.

Jana niliweka picha ya Harry Belafonte na Sidney Poitier na nikasema kuwa watu hawa maarufu walikuwa nyumbani kwa Ally Sykes.

Rose Aziz bint ya Hamza Aziz jana usiku kaniletea ujumbe baada ya kuona picha ile na kunifahamisha kuwa pale ni nyumbani kwao Msasani na baba yake ndiye siku hiyo aliyewaalika Harry Belafonte na Sidney Poitier nyumbani kwao pamoja na Ally Sykes na John Malecela.

Kwenye picha ya kwanza John Malecela amekaa pembeni ya Sidney Poitier.

Naweka hapa picha za siku hiyo adhimu wakati Harry Belafonte na Sidney Poitier walipokuwa wageni wa Hamza Aziz nyumbani kwake Msasani.

Rose amenieleza kuwa Hamza Aziz alikutana tena na Harry Belafonte Canada na Sidney Poitier Marekani na wakabakia kuwa marafiki wa karibu.

Mzee Hamza Aziz mimi na yeye tukimpenda Nat King Cole na akanieleza kuwa katika ujana wake akiziimba nyimbo zake.

Siku moja aliniimbia nyimbo ya Nat King Cole, ''I Love You For Sentimental Reasons.''

Abbas Sykes na Hamza walikuwa marafiki wakubwa sana.

Balozi Sykes alikuwa akimtania Hamza Aziz kwa kumwita jina lake la utani ''Nat King Cole'' akilifupisha kwa kumwita ''Nat.''

Hamza Aziz na yeye akimwita Balozi Sykes ''Spencer Tracey'' jina la muigizaji maarufu katika miaka ya 1950 hadi 1960.

Mwenyezi Mungu awarehemu wazee wetu hawa.

Picha tatu za chini kulia ni Hamza Aziz, Sidney Poitier na Harry Belafonte.

334253340_1591260591338564_7935049236424629549_n.jpg

Walio simama kulia Hamza Aziz na Harry Belafonte chini kulia Sidney Poitier na John Malecela
334250373_215298824368113_429058690959339409_n.jpg

Kulia Harry Belafonte, Sidney Poitier na Hamza Aziz
334432642_1408908219912914_2639556758103707209_n.jpg

Harry Balafonte
334536017_1659622031124556_2238274698262417544_n.jpg

Sidney Poitier

334747253_1371063180356265_5181412606881759616_n.jpg

Hamza Aziz​
 
Mzee Mohamed .S
Kama itakupendeza naongezea taarifa...

Hao magwiji wa Harakati za Kiraia Marekani na Harakati za Ukombozi wa Afrika, waliweza kuisaidia Tanzania wakati wa Magwiji wawili wa masuala ya Kimataifa yaani the Late Amb. Salim Ahmed pamoja na Mh. John Malecela walipokuwa katika nafasi zao mbalimbali za uwakilishi wa Tanzania Umoja wa Mataifa na nchini Marekani. Marekani.

Hao magwiji, Sidney na mwenzie Bellafonte ni moja ya watu walioweza kunichagiza kupenda Siasa na misimamo yao ya maridhiano bila vurugu nyingi! Happy birthday Bellafonte. R.I.P Sidney
 
Mzee Mohamed .S
Kama itakupendeza naongezea taarifa...

Hao magwiji wa Harakati za Kiraia Marekani na Harakati za Ukombozi wa Afrika, waliweza kuisaidia Tanzania wakati wa Magwiji wawili wa masuala ya Kimataifa yaani the Late Amb. Salim Ahmed pamoja na Mh. John Malecela walipokuwa katika nafasi zao mbalimbali za uwakilishi wa Tanzania Umoja wa Mataifa na nchini Marekani. Marekani.

Hao magwiji, Sidney na mwenzie Bellafonte ni moja ya watu walioweza kunichagiza kupenda Siasa na misimamo yao ya maridhiano bila vurugu nyingi! Happy birthday Bellafonte. R.I.P Sidney
Salim is alive.
 
Mzee Mohamed .S
Kama itakupendeza naongezea taarifa...

Hao magwiji wa Harakati za Kiraia Marekani na Harakati za Ukombozi wa Afrika, waliweza kuisaidia Tanzania wakati wa Magwiji wawili wa masuala ya Kimataifa yaani the Late Amb. Salim Ahmed pamoja na Mh. John Malecela walipokuwa katika nafasi zao mbalimbali za uwakilishi wa Tanzania Umoja wa Mataifa na nchini Marekani. Marekani.

Hao magwiji, Sidney na mwenzie Bellafonte ni moja ya watu walioweza kunichagiza kupenda Siasa na misimamo yao ya maridhiano bila vurugu nyingi! Happy birthday Bellafonte. R.I.P Sidney

Wasanii wa Marekani hawawezi kiisaidia Tanzania, much less Tanzania ya Nyerere. Labda hii ya sasa ambayo Rais Mstaafu JK alisema the greatest day of his life ni alipokutana na Michael Jackson.
 
Wasanii wa Marekani hawawezi kiisaidia Tanzania, much less Tanzania ya Nyerere. Labda hii ya sasa ambayo Rais Mstaafu JK alisema the greatest day of his life ni alipokutana na Michael Jackson.
Sijui ulikuwa na mpango gani.
Hakika haujasoma mada wala maudhui ya Mzee Mohamed.
Yaani umekurupuka.

Badala ya kutafuta na Taarifa zako uchanganye na za hapa, unakuja na kejeli kwa sababu za kipuuzi kabisa. Hawa wapigania haki na uhuru, ndio waliokupa uhuru huo. Tumia vizuri.
 
Mzee Mohammed naomba uwaulize hao watu wa Zamani ...kuhusu wasanii wakubwa waliokuja kuimba bure pale mnazi mmoja....hasa kutoka USA
 
Mzee Mohammed naomba uwaulize hao watu wa Zamani ...kuhusu wasanii wakubwa waliokuja kuimba bure pale mnazi mmoja....hasa kutoka USA
The Boss,
Buddy Guy alifanya onyesho Mnazi Mmoja nadhani 1968/69.

Vijana wengi tulihudhuria.

Alifungua na nyimbo instrumental: "Watermelon Man."
 
Sijui ulikuwa na mpango gani.
Hakika haujasoma mada wala maudhui ya Mzee Mohamed.
Yaani umekurupuka.

Badala ya kutafuta na Taarifa zako uchanganye na za hapa, unakuja na kejeli kwa sababu za kipuuzi kabisa. Hawa wapigania haki na uhuru, ndio waliokupa uhuru huo. Tumia vizuri.
Mwafrika usiyeelewa historia na usiyejielewa, unadhani kila kitu umepewa na mgeni, mpaka uhuru wako.

Tanzania tumetafuta uhuru na ukombozi wa nusu ya Afrika, kivita na kidiplomasia, singlehandedly, hakuna mwanamuziki na mcheza filamu aliyetusaidia.

Belafonte na Pottier wamekimbia kwao visiwani, watawezaje kunipatia mimi uhuru ??? Acha ulimbukeni na uwe proud of our own bootstrap struggles.

Na usome hotuba za Malcolm X alivyokuwa anawaasa wa Negro wenzie wajifunze Afrika tulivyogangamala kutafuta uhuru wetu.
 
Mwafrika usiyeelewa historia na usiyejielewa, unadhani kila kitu umepewa na mgeni, mpaka uhuru wako.
Unavimba nini sasa? Unajitutumua kwa vile nina taarifa kukushinda?.
Mpuuzi tu wewe.

Tanzania tumetafuta uhuru na ukombozi wa nusu ya Afrika, kivita na kidiplomasia, singlehandedly, hakuna mwanamuziki na mcheza filamu aliyetusaidia.
Wacha hadaa na upotoshaji....kama isingekuwa network ya hao magwiji Marekani, isingelikuwa rahisi kuishwawishi Serikali ya Marekani kubadilisha msimamo kupitia congress yao kuitaka Serikali ya South Afrika kuacha sera zao za kibaguzi Bisha mpuuzi we
Belafonte na Pottier wamekimbia kwao visiwani, watawezaje kunipatia mimi uhuru ??? Acha ulimbukeni na uwe proud of our own bootstrap struggles.

Kukimbia kwao visiwani ndio inifanye niwapuuzie? una akili ww? Usinipandikize ulimbukeni uliokuwa nao wewe. Najitambua vilivyo.
Na usome hotuba za Malcolm X alivyokuwa anawaasa wa Negro wenzie wajifunze Afrika tulivyogangamala kutafuta uhuru wetu.
Nimsome wa nini? Atakuwa ana tofauti gani na hao magwiji uliowabeza hapa shwain wewe. Unajishaushau tu.

Nimekusoma toka mwanzo, umeacha vyote vilivyokuwa ndani ya mada, ukaja kuniparamia mimi, ukiwa umeona kabisa nimeomba hata ruhusa ya kuweka taarifa zingine, ukaja na yako Ati hawakuweza kuja saidia! Kwa mantiki gani hiyo unayodai hawakuweza kuja kusaidia 'Tanzania ya Nyerere" kwani hao niliowataja walikuwa kwenye serikali ya nani....


Una yako, tafuta wengine huko wa kuwasengenya huko.
 
Mzee Mohamed .S
Kama itakupendeza naongezea taarifa...

Hao magwiji wa Harakati za Kiraia Marekani na Harakati za Ukombozi wa Afrika, waliweza kuisaidia Tanzania wakati wa Magwiji wawili wa masuala ya Kimataifa yaani the Late Amb. Salim Ahmed pamoja na Mh. John Malecela walipokuwa katika nafasi zao mbalimbali za uwakilishi wa Tanzania Umoja wa Mataifa na nchini Marekani. Marekani.

Hao magwiji, Sidney na mwenzie Bellafonte ni moja ya watu walioweza kunichagiza kupenda Siasa na misimamo yao ya maridhiano bila vurugu nyingi! Happy birthday Bellafonte. R.I.P Sidney

Asante kwa hii taarifa.
Unahisi tunakosea wapi?Mbona hata msimamo wa nchi ktk tasnianya kimataifa sasa haujulikani?Mfano kura ya uvamizi wa Russia kule Ukraine sisi TZ tumepiga kura ya ‘absenteeism’
Wapi tunakosea Mzee wangu MO?
 
Asante kwa hii taarifa.
Unahisi tunakosea wapi?Mbona hata msimamo wa nchi ktk tasnianya kimataifa sasa haujulikani?Mfano kura ya uvamizi wa Russia kule Ukraine sisi TZ tumepiga kura ya ‘absenteeism’
Wapi tunakosea Mzee wangu MO?
Mal...
Sitakupa jibu la moja kwa moja bali nitakuwekea hapa sehemu za mhadhara niliotoa State University of Zanzibar (SUZA) iwe muongozo wa kutuangazia tulikotoka hadi kufikia hali hii:

‘’Sheikh Ali Saleh alikuwa alikuwa Imam wa Msikiti wa Kitumbini wakati ule wa ukoloni bila woga wowote alikuwa akitoa khutba za hamasa katika sala ya Ijumaa akiunga mkono harakati za Waarabu wa Palestine dhidi ya uonevu wa Uingereza katika mgogoro wa Mashariki ya Kati.

Mgogoro huu ingawa ulikuwa mbali sana na Tanganyika lakini ulikuwa mmoja wa migogoro iliyokuwa ikiitatanisha serikali ya kikoloni kwa kuwa Waislam wa Tanganyika tayari walikuwa wakipamba Waingereza nchini na waliona shida ya Waislam Palestine ni shida yao pia.

Hali hii ikatoa picha kuwa ni tatizo lililowahusu zaidi Waislam kuliko watu wengine.

Lakini huu ulikuwa wakati wa Waingereza wanaitawala Tanganyika.
Uhuru ulipopatikana sera ya Tanganyika na baadae Tanzania ilikuwa kuwaunga mkono wote wanaodhulumiwa duniani pamoja na Wapelestina.

Katika kupinga dhulma kokote duniani Mwalimu Nyerere akawa ameacha historia kubwa sana.

Baada ya kifo cha Mwalimu Nyerere mwaka wa 1999, pametokea ndani ya Tanzania mabadiliko makubwa yaliyogusa sehemu nyingi katika misingi ambayo ndiyo ilikuwa utambulisho wa nchi.

Mojawapo ya mabadiliko haya makubwa ni msimamo wa Tanzania kwa Israel na tatizo la Wapelestina.

Tanzania imefungua ubalozi Israel baada ya kukata uhusiano na nchi hiyo mwaka wa 1967 baada ya Vita Vya Siku Sita kati ya Israel, Misri, Iraq, Syria, Jordan and Lebanon.

iFum1slRr8u-x6Y1BDvt3fxyDp4Pc1MpI2d2fBz5xe4ORnDV2pzW3EWOBmgxWaOG9VFBCl5LrHshVLeRMKu5C3FswkqSFI2v0pKNwnXVTMOfCeobN7-gXNenrnaGs0s1hPdXymbpCB7XUpR-L7FZzeJzS5V6bXor9QgfUsbE3wS7u5Wr-VeemlbJm6818FOb_Ptal0UqGBwomfUob_NEg9HMilkyzdEaksBGKXU9xnr1Amfo1UEisVilHVcSv208pJGC0JHR3egHhIP0IA_4gI3Q75vIvy9AjYHA9R52P-CuYXB9NOJCsALbizFs1xOEApwS3frtQtOjg7CKOFaasOu9qKz3dEV6dJCUfX_5rN4tEIF_oQYyL9QBIKiHZAGTbNcDXyJxBKls1UbyJEbf477yK24BECbBvONqlIC3EqyPccpab4ehA05wecF4fSlpuFtkAndlMxwergONTdly4p29JkZ5YyjasOvHOephfPp_t9Z-4Zzdi9Ir_KnCNFje7YxlSH16iMmjosmxK0m1TbSUpqwzbgDNHyQIRk3bnjdZTjCB0TZWnUkJ21-XurBoCBEXZG3kcqCtHcd1XouPxU6LSNuM31SI3PEO2wDFELg76FaJV3HALA=w238-h300-no

Sheikh Ali Saleh

IMG-20170623-WA0283.jpg

IMG-20170623-WA0284.jpg

Tanzania imerudisha uhusiano na Wayahudi.

Amerika ni taifa la Kikristo na ni rafiki mkubwa wa Israel lau kama Wayahudi ndiyo waliomuua Yesu, ambae wao kama Wakristo wote duniani wanamuitikadi ni ‘’Mtoto wa Mungu.’’

Kwa Wamarekani Israel ni rafiki na mshirika wake si adui abadan.

Waamerika wana marafiki katika mataifa ya Kiislam kama vile walivyokuwa pia wana maadui wengi katika mataifa ya Kiislam.

Tanzania Ukristo umedhibiti vyema serikali na una nguvu sana katika nyanja zote kuanzia serikalini kwenyewe hadi ndani ya Bunge la Jamhuri ya Tanzania.

Idadi ya Waislam ndani ya Bunge la Tanzania ni ndogo kiasi inaogopwa hata kuelezwa.

Hii nguvu na ushawishi wa Ukristo ndani ya Bunge la Tanzania unaweza kuwa moja ya sababu ya kuona Tanzania imerudisha uhusiano na Israel na balozi wake kujifaharisha na kibandiko cha Kiyahudi pale alipokwenda kujitambulisha Israel.

Zitto Kabwe alipata kusema ndani ya Bunge kuwa:

''Hatuwashi tena mwenge na kuuweka mlimani Kilimanjaro, hatumuliki tena nje ya mipaka yetu, hatuleti tena matumaini pale pasipo na matumaini, hatupeleki tena upendo kule kuliko na chuki, na hatuleti heshima pale palipojaa dharau.

Sisi si Tanzania ya Mwalimu Nyerere, sisi sasa ni Tanzania mpya, Tanzania mbaya, Taifa lililokiuka misingi yake, Taifa linalowaacha Wapelestina wakiuawa kinyama, na sasa linalosapoti waonevu.''

(Sehemu ya Kwanza na ya Hotuba ya ndugu Kabwe Z. Ruyagwa Zitto (MB) Juu ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mwaka 2018/19).


Zitto Kabwa hakurudi Bungeni katika Uchaguzi Mkuu wa 2020.
Hiki ni kisa kingine kwa siku nyingine.

Kwa kuhitimisha napenda kusema kuwa katika historia ya Tanzania kuwaunga mkono Palestine siku zote anatajwa Julius Nyerere hakuna mwandishi yeyote aliyepata kumtaja Sheik Ali Saleh na kusema kuwa harakati hizi zilianza zamani sana na mtu aliyezisimamia alikuwa Sheikh Ali Saleh Imam wa Msikiti wa Kitumbini.

 
Unavimba nini sasa? Unajitutumua kwa vile nina taarifa kukushinda?.
Mpuuzi tu wewe.


Wacha hadaa na upotoshaji....kama isingekuwa network ya hao magwiji Marekani, isingelikuwa rahisi kuishwawishi Serikali ya Marekani kubadilisha msimamo kupitia congress yao kuitaka Serikali ya South Afrika kuacha sera zao za kibaguzi Bisha mpuuzi we


Kukimbia kwao visiwani ndio inifanye niwapuuzie? una akili ww? Usinipandikize ulimbukeni uliokuwa nao wewe. Najitambua vilivyo.

Nimsome wa nini? Atakuwa ana tofauti gani na hao magwiji uliowabeza hapa shwain wewe. Unajishaushau tu.

Nimekusoma toka mwanzo, umeacha vyote vilivyokuwa ndani ya mada, ukaja kuniparamia mimi, ukiwa umeona kabisa nimeomba hata ruhusa ya kuweka taarifa zingine, ukaja na yako Ati hawakuweza kuja saidia! Kwa mantiki gani hiyo unayodai hawakuweza kuja kusaidia 'Tanzania ya Nyerere" kwani hao niliowataja walikuwa kwenye serikali ya nani....


Una yako, tafuta wengine huko wa kuwasengenya huko.

Ni lini, wapi na nini Harry Belafonte na Sidney Pottier walitamka au kufanya kupigania uhuru wa Tanganyika ??????
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom