Kusema kweli Rasimu ya Katiba mpya ina mapungufu mengi ukiacha kosa la msingi la kuleta serikali Tatu lakini kuna hili ambalo limefichwa ndani ya hizo kurasa 240.Watanganyika na Wazanzibari wanatakiwa kupitia kipengele moja baada ya nyingine.
Tunarudishwa kule kule kupitia mlango wa Nyuma.
Updates;
Maoni binafsi ndani ya Rasimu kadri muda utakavyoruhu.
9.-(1) Mtu au kikundi cha watu hakitachukua au kushikilia mamlaka ya nchi (Serikali, Bunge na Mahakama) isipokuwa kwa mujibu wa Katiba hii.
(2) Kitendo chochote kinachokiuka masharti ya Ibara ndogo ya (1) ni batili na ni kitendo cha uhaini isipokuwa Maandamano yoyote ya Amani ya Umma ya kudai haki au kuondoka madarakani kwa maamlaka ya Nchi hayatachukuliwa kuwa ni Uhaini.
10.-(1) Malengo ya Taifa yaliyoainishwa ndani ya Katiba hii yatakuwa ni mwongozo kwa Serikali, Bunge, Mahakama, vyama vya siasa, taasisi, asasi na mamlaka nyingine na kwa kila mwananchi katika matumizi au kutafsiri masharti ya Katiba hii au sheria nyingine
yoyote na katika utekelezaji wa uamuzi wa kisera kwa madhumuni ya kujenga jamii huru, makini na iliyo bora.
(2) Serikali itatoa taarifa Bungeni si chini ya mara moja katika kila mwaka, kuhusu hatua zilizochukuliwa na mamlaka ya nchi ili kuhakikisha utekelezaji wa malengo ya Taifa yaliyoainishwa katika Katiba hii na Bunge litapewa nafasi ya kuijadili na kupiga kura ya kuikubali au kuikataa taarifa husika kwa kutumia Kanuni ya Bunge katika kufikia maamuzi .
11.-(1) Lengo Kuu la Katiba hii ni kulinda, kuimarisha na kudumisha udugu, amani, umoja na utengamano wa wananchi wa Jamhuri ya Muungano kwa kuzingatia ustawi wa wananchi na kujenga Taifa huru lenye demokrasia, utawala bora na kujitegemea.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), lengo hilo kuu litaendelezwa na kuimarishwa katika nyanja zote kuu,ikijumuisha nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na
kimazingira.
(3) Katika kutekeleza malengo ya Taifa ya:
(c) kiuchumi, Serikali inachukua hatua zinazofaa ili:
(i) kuwaletea wananchi maisha bora kwa kuondoa umaskini;
(ii) kuhakikisha kwamba shughuli za Serikali zinatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha
kuwa utajiri wa Taifa unaendelezwa,unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine;
(iii) kuweka mazingira bora kwa ajili ya kuanzisha na kuendeleza vyombo vya uwakilishi wa vikundi vya shughuli za Kiuchumi na kuwashirikisha katika hatua za kuandaa sera na Kanuni za shughuli husika.
(iv) kuweka mazingira bora ya kufanya biashara na kukuza fursa za uwekezaji;
(v) Kupitia Serikali za Washirika wa Muungano Serikali itaweka mazingira bora kwa ajili ya kukuza kilimo, ufugaji na uvuvi kwa kuhakikisha kuwa wakulima, wafugaji na wavuvi wanakuwa na ardhi na nyenzo kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao;
(vi) kuweka mazingira bora ya uzalishaji wa mazao kwa wakulima, wafugaji na wavuvi, utafutaji na uendelezaji wa masoko ya mazao yao;
(vii) kuweka utaratibu mzuri wa upangaji na usimamiaji wa mizania ya bei za mazao zitokanazo na shughuli za uchumi hasa kilimo,Ufugaji na Uvuvi .
(viii) kuimarisha na kuendeleza uwekezaji wa ndani kwa kuhakikisha ,upatikanaji wa Mitaji kwa ajili ya pembejeo za kilimo, madawa na majasho ya Mifugo na vifaa vya uvuvi;
(ix) kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa fursa na nafasi za wazi kwa kila mmoja kuanzisha shughuli za kiuchumi kwa kukuza mazingira yaliyo bora kwa ajili ya kuhamasisha sekta binafsi katika uchumi;
(x) kuhakikisha kuwa kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anapata fursa ya kufanya kazi, kwa maana ya kufanya shughuli yoyote halali inayompatia kipato;
(xi) kuweka utaratibu unaofaa kwa ajili ya kufanikisha utekelezaji wa haki ya mtu kujipatia
elimu na kuwa huru kupata fursa sawa ya kutafuta elimu katika fani anayoipenda hadi
kufikia upeo wowote kulingana na stahili na uwezo wake;
(xii) Serikali itahakikisha mkataba wowote utakaoingiwa na Serikali au taasisi zake na Serikali zingine au Makampuni binafsi unakuwa wa wazi kwa kuweka nakala ya mkataba husika kwenye magazeti na Tovuti ya Wizara/taasisi husika isipokuwa mikataba ya Ulinzi ambao Kamati ya Bunge ya Ulinzi ndiyo itakayo kuwa na Mamlaka ya kukagua kabla Mkataba wenyewe hauja sainiwa kuona kama masilahi ya Taifa yamezingatiwa au lah na kama Mkataba haukuzingatia masilahi ya Taifa Kamati itatoa mapendekezo ya kuzingatiwa na Wizara husika na Nakala kupewa Spika wa Bunge.
16.-(1) Kiongozi wa Umma atalazimika kutangaza, ndani ya siku thelathini baada ya kupata uongozi na baada ya kuacha uongozi,mali na thamani zake na madeni yake katika Tume ya Maadili na Uwajibikaji.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), Kiongozi wa Umma atalazimika kutangaza mali zake na madeni:
(a) yake binafsi;
(b) ya mwenza wake wa ndoa; na
(c) watoto wake walio chini ya umri wa miaka kumi na nane,mara moja kila mwaka, au kadri itakavyoamuliwa na sheria.
(d) Utangazaji wa Mali za kiongozi kupitia kifungu cha 16(2); a na b ya Katiba hii utafanywa chini ya Kiapo na itakuwa Kosa la jinai kusema uongo.
(e) Bunge litatunga sheria itakayo simamia na kuwezesha Umma kuweza kuhakiki ukweli wa mali zilizotangazwa na Kiongozi wa Umma.
19. Masharti yaliyoainishwa katika Ibara za 13, 18 na 20 ya Katiba hii yatatumika pia kwa watumishi wa umma na Bunge kupitia Sheria ya Tume ya Maadili ya Uongozi wa Umma itatunga Kanuni itakayosimamia Masharti ya Katiba hii.
20.-(1) Bila ya kuathiri masharti yoyote ya Katiba hii, kiongozi yeyote wa Umma atapaswa kuheshimu na kutii maadili ya viongozi wa umma, ikiwemo Miiko ya Uongozi.
(2) Miiko ya Uongozi inayorejewa katika Ibara ndogo (1),itakuwa kama ifuatavyo:
(a) Kiongozi wa umma hatopaswa:
(i) kuvunja au kukiuka masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano;
(ii) kutoa au kupokea rushwa;
(iii) kujilimbikizia mali kinyume cha sheria;
(iv) kusema uongo au kutoa taarifa zisizo za ukweli;
(v) kutoa siri za Serikali kinyume na sheria isipokuwa zilizokinyume na Masilahi ya Umma kadri katiba hii ilivyoelekeza;
(vi) kutumia wadhifa, nafasi au cheo chake kwa manufaa yake binafsi, familia yake, ndugu, jamaa au marafiki zake au mtu yeyote aliye na uhusiano naye wa karibu;
(vii) kufanya vitendo vya uzembe, uvivu, ubaguzi,kiburi, dharau au unyanyasaji wa kijinsia.
21.-(1) Mtumishi wa umma aliye katika ajira ya kudumu hataruhusiwa kuingia katika ajira nyingine yoyote yenye malipo ya mshahara.
(2) Mtumishi wa umma haruhusiwi kuchaguliwa au kuteuliwa kushika madaraka katika chama cha siasa .
(3) Mtumishi wa umma aliyestaafu na anayepokea malipo ya pensheni kutokana na fedha za umma anaruhusiwa tu kuwa Mwenyekiti na si kwa zaidi ya vipindi viwili vya jumla ya miaka kumi katika;
(a) shirika au kampuni inayomilikiwa au kuendeshwa kwa fedha za umma; au
(b) chombo chochote cha umma.
(4) Mtumishi wa Umma aliyestaafu na kuwa Mwenyekiti kwa mujibu wa Ibara hii baada ya kumaliza vipindi vyake vya kuwa Mwenyekiti hatabadilishiwa aina ya Pensheni badala yake atabaki na kuendelea kupokea Pensheni yake ya utumishi wa awali.
Updates;
24.-(7) Kwa madhumuni ya kuhakikisha usawa mbele ya sheria,mamlaka ya nchi itaweka utaratibu unaofaa na unaozingatia misingi kwamba -
(a) wakati haki na wajibu kwa mtu yeyote vinapohitajika kufanyiwa uamuzi na mahakama au mamlaka nyingine inayohusika, basi mtu huyo atakuwa na haki ya kupewa fursa ya kusikilizwa kwa ukamilifu, na pia atakuwa na haki ya kukata rufani au kupata nafuu nyingine ya kisheria
kutokana na uamuzi wa mahakama au mamlaka nyingine inayohusika;
(b) ni marufuku kwa mtu aliyeshtakiwa kwa kosa la jinai kutendewa kama mtu aliyehukumiwa kwa kutenda kosa hilo hadi itakapothibitika mahakamani kuwa anayo hatia ya kutenda kosa hilo;
(c) ni marufuku kwa mtu kuadhibiwa kwa sababu ya kitendo chochote ambacho wakati alipotenda kitendo hicho hakikuwa ni kosa chini ya sheria;
(d) ni marufuku kwa mtu kupewa adhabu ambayo ni kubwa kuliko adhabu iliyokuwapo kisheria wakati kosa linalohusika lilipotendeka;
(e) haki ya usawa wa binadamu,heshima ya mtu na faragha itahifadhiwa katika shughuli zote zinazohusu upelelezi wa tuhuma na uendeshaji wa masharti ya jinai na katika shughuli nyingine ambazo mtu anakuwa katika kizuizi cha mamlaka ya nchi au katika kuhakikisha utekelezaji wa adhabu; na
(f) ni marufuku kwa mtu kuteswa, kuadhibiwa kinyama au kupewa adhabu zinazotweza au kudhalilisha.
29.-(1) Kila mtu:
(a) anao uhuru wa-
(i) kuwa na maoni na kueleza fikra zake;
(ii) kufanya mawasiliano na vile vile anayo haki ya kutoingiliwa katika mawasiliano yake;
(iii) ubunifu na sanaa;
(iv) kitaaluma na tafiti za kisayansi; na
(b) anayo haki ya kupewa taarifa wakati wowote kuhusu:
(i) matukio mbalimbali muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi; na
(ii) utekelezaji wa mamlaka ya nchi kuhusu sera za kitaifa na shughuli ya maendeleo ya jamii; na
(iii) masuala mengine muhimu kwa jamii.
(2) Utekelezaji wa haki zilizoainishwa katika Ibara ndogo ya (1), utajumuisha wajibu muhimu kwa mwananchi na wajibu huo unaweza kupunguza haki hizo kutokana na:
(a) vita au machafuko ya kisiasa; au
(b) propaganda kuhusu vita, ushawishi wa chuki kwa misingi ya rangi, ukabila, ubaguzi wa kijinsia, dini ,propaganda kuhusu shughuli za Uchumi yenye mlengo wa ubaguzi au masuala yoyote yanayoelekea kuleta madhara kwa Taifa.
(c) kabla au baada ya mamlaka husika kuchukua hatua kupunguza/kusitisha uhuru wa mtu kwa mujibu wa Ibara 29;2(b) ya katiba hii basi mamlaka husika italiarifu Bunge katika kikao kijacho baada ya tukio husika kuhusu sababu na hatua za kisheria ambazo zimechukuliwa/ inatarajia kuchukuliwa ilikuliepusha Taifa na madhara.
30.-(1) Kila mtu anao uhuru wa-
(a) kutafuta, kupata na kutumia habari na taarifa na kusambaza taarifa hizo; na
(b) kuanzisha vyombo vya habari na njia nyingine za upashanaji wa habari bila kujali mipaka ya nchi.
(2) Vyombo vya habari vitakuwa huru na vile vile vitakuwa na:
(a) haki ya kupata, kutumia na kusambaza habari na taarifa wanazopata;
(b) wajibu wa:
(i) kusambaza habari na taarifa kwa wananchi; na
(ii) kuheshimu na kulinda utu, heshima, uhuru na staha ya wananchi dhidi ya habari na taarifa
wanazozitumia, wanazozitayarisha na kuzisambaza.
(3) Serikali na taasisi zake, asasi za kiraia na watu binafsi watakuwa na wajibu wa kutoa habari kwa umma juu ya shughuli na utekelezaji wa shughuli zao.
(4) Bunge litatunga sheria ya Habari yenye kulinda Usalama wa Taifa, Amani, Maadili ya Umma, haki, staha na uhuru wa watu wengine bila kuathiri masharti yoyote ya ibara ya Katiba hii.
32.(1)Kila mtu anastahili kuwa huru, bila ya kuathiri sheria za nchi,kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kujumuika na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo hadharani, na hasa zaidi kuanzisha au kujiunga na vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo.
(2)Katika kutumia uhuru binafsi kwa mujibu wa ibara ndogo ya 32(1) ya Katiba hii itakuwa marufuku kwa Mtumishi wa Umma kutumia cheo au nafasi yake kwenye utumishi wa Umma kuinufaisha Jumuiya/taasisi ya Imani kwa namna ambayo italeta taswira ya upendeleo au ubaguzi kwa kuwa naye ni mshirika wa Jumuiya hiyo au lah! lakini ananufaika/atanufaika yeye binafsi au taasisi anayoitumikia kupitia Jumuiya hiyo ya Kiimani kwa namna yoyote ile .
Tunarudishwa kule kule kupitia mlango wa Nyuma.
Kupitishwa
kwa hoja
za SerikaliKupitishwa
kwa hoja
za Serikali
115.-(1) Endapo Bunge halitaridhishwa na mchanganuo au
mgawanyo wa hoja ya Bajeti iliyowasilishwa na serikali, Bunge linaweza
‐ 47 ‐
kurudisha hoja kuhusu Bajeti ya Serikali pamoja na mapendekezomahsusi
kuhusiana na upungufuuliobainika.
(2) Serikali itawajibika kuyafanyia kazi mapendekezo ya Bunge kwa
kadri itakavyowezekana na kisha kuwasilisha tena Bungeni hoja husika
pamoja na maelezo ya utekelezaji wa maelekezo ya Bunge na endapo Bunge
litakataa kwa mara ya pili hoja kuhusu Bajeti ya Serikali, basi hoja hiyo
itahesabika kuwa imepitishwa na Bunge.
Updates;
Maoni binafsi ndani ya Rasimu kadri muda utakavyoruhu.
2. Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanganyika ikijumuisha sehemu yake ya bahari na eneo lote la Zanzibar ikijumuisha sehemu yake ya bahari.2. Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara ikijumuisha sehemu yake ya bahari na eneo lote la Zanzibar ikijumuisha sehemu yake ya bahari.
9.-(1) Mtu au kikundi cha watu hakitachukua au kushikilia mamlaka ya nchi isipokuwa kwa mujibu wa Katiba hii.
(2) Kitendo chochote kinachokiuka masharti ya Ibara ndogo ya (1) ni batili na ni kitendo cha uhaini kama itakavyoelezwa katika sheria za nchi.
9.-(1) Mtu au kikundi cha watu hakitachukua au kushikilia mamlaka ya nchi (Serikali, Bunge na Mahakama) isipokuwa kwa mujibu wa Katiba hii.
(2) Kitendo chochote kinachokiuka masharti ya Ibara ndogo ya (1) ni batili na ni kitendo cha uhaini isipokuwa Maandamano yoyote ya Amani ya Umma ya kudai haki au kuondoka madarakani kwa maamlaka ya Nchi hayatachukuliwa kuwa ni Uhaini.
10.-(1) Malengo ya Taifa yaliyoainishwa ndani ya Katiba hii yatakuwa ni mwongozo kwa Serikali, Bunge, Mahakama, vyama vya siasa, taasisi, asasi na mamlaka nyingine na kwa kila mwananchi katika matumizi au kutafsiri masharti ya Katiba hii au sheria nyingine yoyote na katika utekelezaji wa uamuzi wa kisera kwa madhumuni ya kujenga jamii huru, makini na iliyo bora.
(2) Serikali itatoa taarifa Bungeni si chini ya mara moja katika kila mwaka, kuhusu hatua zilizochukuliwa na mamlaka ya nchi ili kuhakikisha utekelezaji wa malengo ya Taifa yaliyoainishwa katika Katiba hii.
10.-(1) Malengo ya Taifa yaliyoainishwa ndani ya Katiba hii yatakuwa ni mwongozo kwa Serikali, Bunge, Mahakama, vyama vya siasa, taasisi, asasi na mamlaka nyingine na kwa kila mwananchi katika matumizi au kutafsiri masharti ya Katiba hii au sheria nyingine
yoyote na katika utekelezaji wa uamuzi wa kisera kwa madhumuni ya kujenga jamii huru, makini na iliyo bora.
(2) Serikali itatoa taarifa Bungeni si chini ya mara moja katika kila mwaka, kuhusu hatua zilizochukuliwa na mamlaka ya nchi ili kuhakikisha utekelezaji wa malengo ya Taifa yaliyoainishwa katika Katiba hii na Bunge litapewa nafasi ya kuijadili na kupiga kura ya kuikubali au kuikataa taarifa husika kwa kutumia Kanuni ya Bunge katika kufikia maamuzi .
11.-(1) Lengo Kuu la Katiba hii ni kulinda, kuimarisha na kudumisha udugu, amani, umoja na utengamanowa wananchi wa Jamhuri ya Muungano kwa kuzingatia ustawi wa wananchi na kujenga Taifa huru lenye demokrasia, utawala bora na kujitegemea.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), lengo hilo kuu litaendelezwa na kuimarishwa katika nyanja zote kuu,ikijumuisha nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na
kimazingira.
(3) Katika kutekeleza malengo ya Taifa ya:
(c) kiuchumi, Serikali inachukua hatua zinazofaa ili:
(i) kuwaletea wananchi maisha bora kwa kuondoa umaskini;
(ii) kuhakikisha kwamba shughuli za Serikali zinatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha
kuwa utajiri wa Taifa unaendelezwa,unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine;
(iii) kuweka mazingira bora kwa ajili ya kuanzisha na kuendeleza vyombo vya uwakilishi wa wakulima,wafugaji na wavuvi;
(iv) kuweka mazingira bora ya kufanya biashara na kukuza fursa za uwekezaji;
(v) kuweka mazingira bora kwa ajili ya kukuza kilimo, ufugaji na uvuvi kwa kuhakikisha kuwa wakulima, wafugaji na wavuvi wanakuwa na ardhi na nyenzo kwa ajili ya kuendeleza shughuli
zao;
(vi) kuweka mazingira bora ya uzalishaji wa mazao kwa wakulima, wafugaji na wavuvi, utafutaji na uendelezaji wa masoko ya mazao yao;
(vii) kuweka utaratibu mzuri wa upangaji na usimamiaji wa mizania ya bei za mazao na
pembejeo;
(viii) kuimarisha na kuendeleza uwekezaji wa ndani,upatikanaji wa pembejeo za kilimo, maeneo ya ufugaji na vifaa vya uvuvi;
(ix) kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa fursa na nafasi za wazi kwa watu wote na kuanzisha shughuli za kiuchumi na kukuza mazingira yaliyobora kwa ajili ya kuhamasisha sekta binafsi katika uchumi;
(x) kuhakikisha kuwa kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anapata fursa ya kufanya kazi, kwa maana ya kufanya shughuli yoyote halali inayompatia kipato;
(xi) kuweka utaratibu unaofaa kwa ajili ya kufanikisha utekelezaji wa haki ya mtu kujipatia elimu na kuwa huru kupata fursa sawa ya kutafuta elimu katika fani anayoipenda hadi kufikia upeo wowote kulingana na stahili na uwezo wake;
11.-(1) Lengo Kuu la Katiba hii ni kulinda, kuimarisha na kudumisha udugu, amani, umoja na utengamano wa wananchi wa Jamhuri ya Muungano kwa kuzingatia ustawi wa wananchi na kujenga Taifa huru lenye demokrasia, utawala bora na kujitegemea.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), lengo hilo kuu litaendelezwa na kuimarishwa katika nyanja zote kuu,ikijumuisha nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na
kimazingira.
(3) Katika kutekeleza malengo ya Taifa ya:
(c) kiuchumi, Serikali inachukua hatua zinazofaa ili:
(i) kuwaletea wananchi maisha bora kwa kuondoa umaskini;
(ii) kuhakikisha kwamba shughuli za Serikali zinatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha
kuwa utajiri wa Taifa unaendelezwa,unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine;
(iii) kuweka mazingira bora kwa ajili ya kuanzisha na kuendeleza vyombo vya uwakilishi wa vikundi vya shughuli za Kiuchumi na kuwashirikisha katika hatua za kuandaa sera na Kanuni za shughuli husika.
(iv) kuweka mazingira bora ya kufanya biashara na kukuza fursa za uwekezaji;
(v) Kupitia Serikali za Washirika wa Muungano Serikali itaweka mazingira bora kwa ajili ya kukuza kilimo, ufugaji na uvuvi kwa kuhakikisha kuwa wakulima, wafugaji na wavuvi wanakuwa na ardhi na nyenzo kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao;
(vi) kuweka mazingira bora ya uzalishaji wa mazao kwa wakulima, wafugaji na wavuvi, utafutaji na uendelezaji wa masoko ya mazao yao;
(vii) kuweka utaratibu mzuri wa upangaji na usimamiaji wa mizania ya bei za mazao zitokanazo na shughuli za uchumi hasa kilimo,Ufugaji na Uvuvi .
(viii) kuimarisha na kuendeleza uwekezaji wa ndani kwa kuhakikisha ,upatikanaji wa Mitaji kwa ajili ya pembejeo za kilimo, madawa na majasho ya Mifugo na vifaa vya uvuvi;
(ix) kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa fursa na nafasi za wazi kwa kila mmoja kuanzisha shughuli za kiuchumi kwa kukuza mazingira yaliyo bora kwa ajili ya kuhamasisha sekta binafsi katika uchumi;
(x) kuhakikisha kuwa kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anapata fursa ya kufanya kazi, kwa maana ya kufanya shughuli yoyote halali inayompatia kipato;
(xi) kuweka utaratibu unaofaa kwa ajili ya kufanikisha utekelezaji wa haki ya mtu kujipatia
elimu na kuwa huru kupata fursa sawa ya kutafuta elimu katika fani anayoipenda hadi
kufikia upeo wowote kulingana na stahili na uwezo wake;
(xii) Serikali itahakikisha mkataba wowote utakaoingiwa na Serikali au taasisi zake na Serikali zingine au Makampuni binafsi unakuwa wa wazi kwa kuweka nakala ya mkataba husika kwenye magazeti na Tovuti ya Wizara/taasisi husika isipokuwa mikataba ya Ulinzi ambao Kamati ya Bunge ya Ulinzi ndiyo itakayo kuwa na Mamlaka ya kukagua kabla Mkataba wenyewe hauja sainiwa kuona kama masilahi ya Taifa yamezingatiwa au lah na kama Mkataba haukuzingatia masilahi ya Taifa Kamati itatoa mapendekezo ya kuzingatiwa na Wizara husika na Nakala kupewa Spika wa Bunge.
16.-(1) Kiongozi wa Umma atalazimika kutangaza, ndani ya siku thelathini baada ya kupata uongozi na baada ya kuacha uongozi,mali na thamani zake na madeni yake katika Tume ya Maadili na Uwajibikaji.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), Kiongozi wa Umma atalazimika kutangaza mali zake na madeni:
(a) yake binafsi;
(b) ya mwenza wake wa ndoa; na
(c) watoto wake walio chini ya umri wa miaka kumi na nane,mara moja kila mwaka, au kadri itakavyoamuliwa na sheria.
16.-(1) Kiongozi wa Umma atalazimika kutangaza, ndani ya siku thelathini baada ya kupata uongozi na baada ya kuacha uongozi,mali na thamani zake na madeni yake katika Tume ya Maadili na Uwajibikaji.
(2) Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1), Kiongozi wa Umma atalazimika kutangaza mali zake na madeni:
(a) yake binafsi;
(b) ya mwenza wake wa ndoa; na
(c) watoto wake walio chini ya umri wa miaka kumi na nane,mara moja kila mwaka, au kadri itakavyoamuliwa na sheria.
(d) Utangazaji wa Mali za kiongozi kupitia kifungu cha 16(2); a na b ya Katiba hii utafanywa chini ya Kiapo na itakuwa Kosa la jinai kusema uongo.
(e) Bunge litatunga sheria itakayo simamia na kuwezesha Umma kuweza kuhakiki ukweli wa mali zilizotangazwa na Kiongozi wa Umma.
19. Masharti yaliyoainishwa katika Ibara za 13 mpaka 18 yatatumika pia kwa watumishi wa umma baada ya kufanyiwa marekebisho stahiki.
19. Masharti yaliyoainishwa katika Ibara za 13, 18 na 20 ya Katiba hii yatatumika pia kwa watumishi wa umma na Bunge kupitia Sheria ya Tume ya Maadili ya Uongozi wa Umma itatunga Kanuni itakayosimamia Masharti ya Katiba hii.
20.-(1) Bila ya kuathiri masharti yoyote ya Katiba hii, kiongozi yeyote wa Umma atapaswa kuheshimu na kutii maadili ya viongozi
wa umma, ikiwemo Miiko ya Uongozi.
(2) Miiko ya Uongozi inayorejewa katika Ibara ndogo (1),itakuwa kama ifuatavyo:
(a) Kiongozi wa umma hatopaswa:
(i) kuvunja au kukiuka masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano;
(ii) kutoa au kupokea rushwa;
(iii) kujilimbikizia mali kinyume cha sheria;
(iv) kusema uongo au kutoa taarifa zisizo za ukweli;
(v) kutoa siri za Serikali kinyume na sheria;
(vi) kutumia wadhifa, nafasi au cheo chake kwa manufaa yake binafsi, familia yake, ndugu, jamaa
au marafiki zake au mtu yeyote aliye na uhusiano naye wa karibu;
(vii) kufanya vitendo vya uzembe, uvivu, ubaguzi,kiburi, dharau au unyanyasaji wa kijinsia.
20.-(1) Bila ya kuathiri masharti yoyote ya Katiba hii, kiongozi yeyote wa Umma atapaswa kuheshimu na kutii maadili ya viongozi wa umma, ikiwemo Miiko ya Uongozi.
(2) Miiko ya Uongozi inayorejewa katika Ibara ndogo (1),itakuwa kama ifuatavyo:
(a) Kiongozi wa umma hatopaswa:
(i) kuvunja au kukiuka masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano;
(ii) kutoa au kupokea rushwa;
(iii) kujilimbikizia mali kinyume cha sheria;
(iv) kusema uongo au kutoa taarifa zisizo za ukweli;
(v) kutoa siri za Serikali kinyume na sheria isipokuwa zilizokinyume na Masilahi ya Umma kadri katiba hii ilivyoelekeza;
(vi) kutumia wadhifa, nafasi au cheo chake kwa manufaa yake binafsi, familia yake, ndugu, jamaa au marafiki zake au mtu yeyote aliye na uhusiano naye wa karibu;
(vii) kufanya vitendo vya uzembe, uvivu, ubaguzi,kiburi, dharau au unyanyasaji wa kijinsia.
21.-(1) Mtumishi wa umma aliye katika ajira ya kudumu hataruhusiwa kuingia katika ajira nyingine yoyote yenye malipo ya
mshahara.
(2) Mtumishi wa umma haruhusiwi kuchaguliwa au kuteuliwa kushika madaraka katika chama cha siasa.
(3) Mtumishi wa umma aliyestaafu na anayepokea malipo ya pensheni kutokana na fedha za umma haruhusiwi kuwa mwenyekiti,
mkurugenzi au mtumishi zaidi ya vipindi viwili katika:
(a) shirika au kampuni inayomilikiwa au kuendeshwa kwa fedha za umma; au
(b) chombo chochote cha umma.
21.-(1) Mtumishi wa umma aliye katika ajira ya kudumu hataruhusiwa kuingia katika ajira nyingine yoyote yenye malipo ya mshahara.
(2) Mtumishi wa umma haruhusiwi kuchaguliwa au kuteuliwa kushika madaraka katika chama cha siasa .
(3) Mtumishi wa umma aliyestaafu na anayepokea malipo ya pensheni kutokana na fedha za umma anaruhusiwa tu kuwa Mwenyekiti na si kwa zaidi ya vipindi viwili vya jumla ya miaka kumi katika;
(a) shirika au kampuni inayomilikiwa au kuendeshwa kwa fedha za umma; au
(b) chombo chochote cha umma.
(4) Mtumishi wa Umma aliyestaafu na kuwa Mwenyekiti kwa mujibu wa Ibara hii baada ya kumaliza vipindi vyake vya kuwa Mwenyekiti hatabadilishiwa aina ya Pensheni badala yake atabaki na kuendelea kupokea Pensheni yake ya utumishi wa awali.
Updates;
24.- (7) Kwa madhumuni ya kuhakikisha usawa mbele ya sheria,mamlaka ya nchi itaweka utaratibu unaofaa na unaozingatia misingi kwamba -
(a) wakati haki na wajibu kwa mtu yeyote vinapohitajika kufanyiwa uamuzi na mahakama au mamlaka nyingine inayohusika, basi mtu huyo atakuwa na haki ya kupewa fursa ya kusikilizwa kwa ukamilifu, na pia atakuwa na haki ya kukata rufani au kupata nafuu nyingine ya kisheria
kutokana na uamuzi wa mahakama au mamlaka nyingine inayohusika;
(b) ni marufuku kwa mtu aliyeshtakiwa kwa kosa la jinai kutendewa kama mtu aliyehukumiwa kwa kutenda kosa hilo hadi itakapothibitika mahakamani kuwa anayo hatia ya kutenda kosa hilo;
(c) ni marufuku kwa mtu kuadhibiwa kwa sababu ya kitendo chochote ambacho wakati alipotenda kitendo hicho hakikuwa ni kosa chini ya sheria;
(d) ni marufuku kwa mtu kupewa adhabu ambayo ni kubwa kuliko adhabu iliyokuwapo wakati kosa linalohusika lilipotendeka;
(e) kwa ajili ya kuhifadhi haki ya usawa wa binadamu,heshima ya mtu na faragha itahifadhiwa katika shughuli zote zinazohusu upelelezi wa tuhuma na uendeshaji wa masharti ya jinai na katika shughuli nyingine ambazo mtu anakuwa katika kizuizi cha mamlaka ya nchi au katika
kuhakikisha utekelezaji wa adhabu; na
(f) ni marufuku kwa mtu kuteswa, kuadhibiwa kinyama au kupewa adhabu zinazotweza au kudhalilisha.
24.-(7) Kwa madhumuni ya kuhakikisha usawa mbele ya sheria,mamlaka ya nchi itaweka utaratibu unaofaa na unaozingatia misingi kwamba -
(a) wakati haki na wajibu kwa mtu yeyote vinapohitajika kufanyiwa uamuzi na mahakama au mamlaka nyingine inayohusika, basi mtu huyo atakuwa na haki ya kupewa fursa ya kusikilizwa kwa ukamilifu, na pia atakuwa na haki ya kukata rufani au kupata nafuu nyingine ya kisheria
kutokana na uamuzi wa mahakama au mamlaka nyingine inayohusika;
(b) ni marufuku kwa mtu aliyeshtakiwa kwa kosa la jinai kutendewa kama mtu aliyehukumiwa kwa kutenda kosa hilo hadi itakapothibitika mahakamani kuwa anayo hatia ya kutenda kosa hilo;
(c) ni marufuku kwa mtu kuadhibiwa kwa sababu ya kitendo chochote ambacho wakati alipotenda kitendo hicho hakikuwa ni kosa chini ya sheria;
(d) ni marufuku kwa mtu kupewa adhabu ambayo ni kubwa kuliko adhabu iliyokuwapo kisheria wakati kosa linalohusika lilipotendeka;
(e) haki ya usawa wa binadamu,heshima ya mtu na faragha itahifadhiwa katika shughuli zote zinazohusu upelelezi wa tuhuma na uendeshaji wa masharti ya jinai na katika shughuli nyingine ambazo mtu anakuwa katika kizuizi cha mamlaka ya nchi au katika kuhakikisha utekelezaji wa adhabu; na
(f) ni marufuku kwa mtu kuteswa, kuadhibiwa kinyama au kupewa adhabu zinazotweza au kudhalilisha.
29.-(1) Kila mtu:
(a) anao uhuru wa-
(i) kuwa na maoni na kueleza fikra zake;
(ii) kufanya mawasiliano na vile vile anayo haki ya kutoingiliwa katika mawasiliano yake;
(iii) ubunifu na sanaa;
(iv) kitaaluma na tafiti za kisayansi; na
(b) anayo haki ya kupewa taarifa wakati wowote kuhusu:
(i) matukio mbalimbali muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi; na
(ii) utekelezaji wa mamlaka ya nchi kuhusu sera za kitaifa na shughuli ya maendeleo ya jamii; na
(iii) masuala mengine muhimu kwa jamii.
(2) Utekelezaji wa haki zilizoainishwa katika Ibara ndogo ya (1), utajumuisha wajibu muhimu kwa mwananchi na wajibu huo unaweza kupunguza haki hizo kutokana na:
(a) vita au machafuko ya kisiasa; au
(b) propaganda kuhusu vita, ushawishi wa chuki kwa misingi ya rangi, ukabila, ubaguzi wa kijinsia, dini au masuala yoyote yanayoweza kuleta madhara kwa Taifa.
29.-(1) Kila mtu:
(a) anao uhuru wa-
(i) kuwa na maoni na kueleza fikra zake;
(ii) kufanya mawasiliano na vile vile anayo haki ya kutoingiliwa katika mawasiliano yake;
(iii) ubunifu na sanaa;
(iv) kitaaluma na tafiti za kisayansi; na
(b) anayo haki ya kupewa taarifa wakati wowote kuhusu:
(i) matukio mbalimbali muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi; na
(ii) utekelezaji wa mamlaka ya nchi kuhusu sera za kitaifa na shughuli ya maendeleo ya jamii; na
(iii) masuala mengine muhimu kwa jamii.
(2) Utekelezaji wa haki zilizoainishwa katika Ibara ndogo ya (1), utajumuisha wajibu muhimu kwa mwananchi na wajibu huo unaweza kupunguza haki hizo kutokana na:
(a) vita au machafuko ya kisiasa; au
(b) propaganda kuhusu vita, ushawishi wa chuki kwa misingi ya rangi, ukabila, ubaguzi wa kijinsia, dini ,propaganda kuhusu shughuli za Uchumi yenye mlengo wa ubaguzi au masuala yoyote yanayoelekea kuleta madhara kwa Taifa.
(c) kabla au baada ya mamlaka husika kuchukua hatua kupunguza/kusitisha uhuru wa mtu kwa mujibu wa Ibara 29;2(b) ya katiba hii basi mamlaka husika italiarifu Bunge katika kikao kijacho baada ya tukio husika kuhusu sababu na hatua za kisheria ambazo zimechukuliwa/ inatarajia kuchukuliwa ilikuliepusha Taifa na madhara.
30.-(1) Kila mtu anao uhuru wa-
(a) kutafuta, kupata na kutumia habari na taarifa na kusambaza taarifa hizo; na
(b) kuanzisha vyombo vya habari na njia nyingine za upashanaji wa habari bila kujali mipaka ya nchi.
(2) Vyombo vya habari vitakuwa huru na vile vile vitakuwa na:
(a) haki ya kupata, kutumia na kusambaza habari na taarifa wanazopata;
(b) wajibu wa:
(i) kusambaza habari na taarifa kwa wananchi; na
(ii) kuheshimu na kulinda utu, heshima, uhuru na staha ya wananchi dhidi ya habari na taarifa
wanazozitumia, wanazozitayarisha na kuzisambaza.
(3) Serikali na taasisi zake, asasi za kiraia na watu binafsi watakuwa na wajibu wa kutoa habari kwa umma juu ya shughuli na utekelezaji wa shughuli zao.
(4) Masharti ya Ibara hii yatalazimika kuzingatia masharti ya sheria ya nchi itakayotungwa kwa ajili hiyo na kwa madhumuni ya kulinda usalama wa Taifa, amani, maadili ya umma, haki, staha na uhuru wa watu wengine.
30.-(1) Kila mtu anao uhuru wa-
(a) kutafuta, kupata na kutumia habari na taarifa na kusambaza taarifa hizo; na
(b) kuanzisha vyombo vya habari na njia nyingine za upashanaji wa habari bila kujali mipaka ya nchi.
(2) Vyombo vya habari vitakuwa huru na vile vile vitakuwa na:
(a) haki ya kupata, kutumia na kusambaza habari na taarifa wanazopata;
(b) wajibu wa:
(i) kusambaza habari na taarifa kwa wananchi; na
(ii) kuheshimu na kulinda utu, heshima, uhuru na staha ya wananchi dhidi ya habari na taarifa
wanazozitumia, wanazozitayarisha na kuzisambaza.
(3) Serikali na taasisi zake, asasi za kiraia na watu binafsi watakuwa na wajibu wa kutoa habari kwa umma juu ya shughuli na utekelezaji wa shughuli zao.
(4) Bunge litatunga sheria ya Habari yenye kulinda Usalama wa Taifa, Amani, Maadili ya Umma, haki, staha na uhuru wa watu wengine bila kuathiri masharti yoyote ya ibara ya Katiba hii.
32.Kila mtu anastahili kuwa huru, bila ya kuathiri sheria za nchi,kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kujumuika na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo hadharani, na hasa zaidi kuanzisha au kujiunga na vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo.
32.(1)Kila mtu anastahili kuwa huru, bila ya kuathiri sheria za nchi,kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kujumuika na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo hadharani, na hasa zaidi kuanzisha au kujiunga na vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo.
(2)Katika kutumia uhuru binafsi kwa mujibu wa ibara ndogo ya 32(1) ya Katiba hii itakuwa marufuku kwa Mtumishi wa Umma kutumia cheo au nafasi yake kwenye utumishi wa Umma kuinufaisha Jumuiya/taasisi ya Imani kwa namna ambayo italeta taswira ya upendeleo au ubaguzi kwa kuwa naye ni mshirika wa Jumuiya hiyo au lah! lakini ananufaika/atanufaika yeye binafsi au taasisi anayoitumikia kupitia Jumuiya hiyo ya Kiimani kwa namna yoyote ile .