KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 35,772
- 86,460
Hivi sasa kumekuwa na jopo la wanawake kurudia wapenzi wao wa zamani baada ya kuona kule walipoenda mambo si mambo. Si kwa wote lakini.
Moja kati ya kiu kinachowasumbua viumbe hawa ni ile ndoto yao ya kuwa na mpenzi wa aina fulani. Kuwa na ndoto si kosa ila ndoto na uhalisia wa maisha ni vitu viwili tofauti.
Ambacho kinawaponza ni kutokujua usahihi, kila atakayempata humuona bado hajakidhi vigezohivyo huamua kutafuta njia nyingine na hapa huwa hana hakika ya kujua uamuzi alioufanya ni sahihi au si sahihi.
Usahihi ni upi?
Usahihi katika mapenzi ni kile kimfaacho mtu katika nyanja zake. Wanawake wa leo ni wale wanaotaka utimilifu wa mwanaume kimwili na kiuchumi. Kitu ambacho wamesahau viumbe hawa ni tabia,a mbapo hichi baadae ndio huwa majuto na husahihisha kile alichokiona hakifai.
Mwanamke ni heri kujua ni usahihi upi unauhitaji kwa mwenzi wako ili unapoingia kwenye huba ujue kile ulichokichagua ni sahihi. Moja kati ya kosa ni hili wanaume huweza kuingia kwenye mahusiano hata kama hajakupenda lakini huweza kukupenda akiwa ndani ya mahusiano. Mwanamke ukiipata nafasi hii itumie, ukimuacha muda utaongea nawe kama mambo yakikuendea kombo.
Ni heri kujenga maisha na yule uliyempenda na yeye akakupenda na kwenye mapenzi kila aliyependwa ni lazima aelewe kuwa kupendwa huko si sehemu ya kumuadhibu aliyekupenda.
Muda si kitu cha kutalii bali kutumia katika usahihi.
Mwambie unayempenda kuwa unampenda kwa usahihi.