Habari zenu wana MMU?
Mimi ni dada ambaye nimepata mpenzi kama miezi mitatu hivi imepita. Kitu kinachonifanya niombe ushauri wenu ni kwamba, huyu kaka kwanza mawasiliano yake sio mazuri ni mpaka nimuanze na hata nikimtext anachukua kama masaa mawili ndio anajibu meseji.. Anajitetea kwamba yuko bize sana. Anapafahamu ninapoishi na huwa anakuja kunitembelea lakini ninapomwambia anipeleke kwake anasema atanipeleka kwa sasa ni mapema mno kufanya hivyo.
Kitu kingine nilipomueleza kwamba mimi niko serious na huu uhusiano, akaniambia kwa nini tusichukulie kama tuu tunastareheshana isitoshe tuna muda mfupi tangu tumeanza hivyo tusiji commit mapema! Na akanieleza nisipende sana mambo ya kuolewa kama vipi tuzae tu.
Napata wasiwasi na huyu kaka kama kweli ana mpango na mimi. Naombeni ushauri wenu maana nimeshaanza kukata tamaa..
Mimi ni dada ambaye nimepata mpenzi kama miezi mitatu hivi imepita. Kitu kinachonifanya niombe ushauri wenu ni kwamba, huyu kaka kwanza mawasiliano yake sio mazuri ni mpaka nimuanze na hata nikimtext anachukua kama masaa mawili ndio anajibu meseji.. Anajitetea kwamba yuko bize sana. Anapafahamu ninapoishi na huwa anakuja kunitembelea lakini ninapomwambia anipeleke kwake anasema atanipeleka kwa sasa ni mapema mno kufanya hivyo.
Kitu kingine nilipomueleza kwamba mimi niko serious na huu uhusiano, akaniambia kwa nini tusichukulie kama tuu tunastareheshana isitoshe tuna muda mfupi tangu tumeanza hivyo tusiji commit mapema! Na akanieleza nisipende sana mambo ya kuolewa kama vipi tuzae tu.
Napata wasiwasi na huyu kaka kama kweli ana mpango na mimi. Naombeni ushauri wenu maana nimeshaanza kukata tamaa..