Mkaruka
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 19,617
- 34,062
Kuwa na fikra huru kisha urudi hapa tuzungumze.Hiyo Support hatukatai lkn nina uhakika yeye alitoa zaidi ya nusu,je msanii gani unaye mjua ww ndani ya miaka minne akawa na hela kama Kondeboy.
Yy aliuza nyumba mbili na kutoa mil 200,jembe ni jembe akaongeza mili 100.
Show zilikuwa juu,sh ngapi?
Mgao ulukuwa juu kwa % ngapi?
Alafu umemzungumzia Qboy WCB wamemnyonya,sasa mbona kila siku anamwomba msamaha Diamond arudi WCB,manake kama kungekuwa kubaya asinge omba kurudi.
Kifesi WCB ndani ya miaka mitatu WCB ana nyumba mwanza na gari.Kifesi kaondoka WCB sababu ya imani yake ya kisabato,anaona anakosea kufanya kazi siku ya sabato na kaondoka sasa hivi ana kampuni yake ya kupiga picha kwenye masherehe na huwezi mzuia mtu ambaye kwa imani yake anaona anachofanya ni haram.
Mavoko kaingia WCB,alitoa nyimbo ngapi na hit songs zilikuwa ngapi,alikaa kwa miaka mingapi?Mavoko alikuwa chini ya Papaa alipata kiasi gani?,Kaenda Kenya kwa King Kaka alikuwa na kiasi gani?
Alafu useme leo hii WCB wamemnyonya?Kwa mujibu ya intvw aliyoifanya Papa Misifa na Soudy mpaka sasa hivi mavoko andaiwa mil 50 na Papaa,baada ya kuvunja mkataba na kwenda kwa Papa Misifa.
Mavoko kaondoka WCB 2018,je mpaka hivi sasa ana kiasi gani?