Lord Diplock MR
JF-Expert Member
- Mar 16, 2015
- 1,393
- 3,234
Huyu kijana wa Banza Stone Hanstone ninaamini ana kipaji kikubwa sana. Ameonesha uwezo mkubwa sana kwenye wimbo wa Iokote alioshirikishwa na Maua Sama, na hatimaye nyimbo zake mbili ailizozitoa hapo baadaye za acha lipite na I miss you mama. Pamoja na kwamba hizo nyimbo mbili alisema hazikuwa rasmi lakini zilituvutia wengi na kuona ni kijana mwenye bright future kwenye muziki.
Basi mambo yakawa mambo akajitoa kwenye management aliyokuwepo ya kina Abbah na Hanscana na kutokomea kusikojulikana. Ni zaidi ya mwaka sasa hajulikani yupo management gani, wapo waliosema yupo kwa S2kizzy na wengine wakasema anaandaliwa kuingia wasafi, wapo pia waliosema yupo chini ya Harmonize. Siku zinakwenda hakuna lililothibitika yeye mwenyewe hasemi yupo wapi amekuwa Kama Yahaya.
Lakini ni nini kilimtoa kwa Abbah na Hanscana ambako mwenzake Marioo ametulia na anafanya vizuri? Ni kiburi? Abbah process anasema Hanstone aliondoka bila kuaga ni pale alipomkemea baada ya kuiba wimbo walioufanya studio na kuuvujisha, baada ya kumsema akanuna akaondoka. Walipomwita kushoot video ya wimbo wa Chibonge akagoma kutokea hali iliyopelekea wakaondoa verse yake na kumweka gnako.
Akihojiwa na media bila kusema kilichomtoa kwa Abbah anawakana kwamba hakuwa ameingia nao mkataba wowote wa maandishi. Sasa mbona walimpora akaunti yake ya Instagram Kama ndiyo hivyo? Yaani bila mkataba wowote wakamshirikisha kwenye Iokote, Chibonge na kumrekodia nyimbo zingine? Mkataba ni lazima uwe umeandikwa?. Kisheria mkataba ambao ni lazima uandikwe ni wa ajira na kuuziana ardhi tu mingine inaweza isiandikwe na ikawa halali ili mradi kukiwa na ushahidi tu. Kwa hapa Kuna ushahidi wa kimazingira kuwa dogo alikuwa chini ya kina Abbah process na Hanscana na ameondoka kwa jeuri na kiburi.
Hanstone unapaswa ujirekebishe maana kwa staili hii hata labels kubwa unazozitegemea Kama Wasafi na Konde gang zitaogopa kukusaini maana jina lako limeshakuwa labelled kuwa ni kijana mwenye kiburi na dharau na asiye ambilika
Basi mambo yakawa mambo akajitoa kwenye management aliyokuwepo ya kina Abbah na Hanscana na kutokomea kusikojulikana. Ni zaidi ya mwaka sasa hajulikani yupo management gani, wapo waliosema yupo kwa S2kizzy na wengine wakasema anaandaliwa kuingia wasafi, wapo pia waliosema yupo chini ya Harmonize. Siku zinakwenda hakuna lililothibitika yeye mwenyewe hasemi yupo wapi amekuwa Kama Yahaya.
Lakini ni nini kilimtoa kwa Abbah na Hanscana ambako mwenzake Marioo ametulia na anafanya vizuri? Ni kiburi? Abbah process anasema Hanstone aliondoka bila kuaga ni pale alipomkemea baada ya kuiba wimbo walioufanya studio na kuuvujisha, baada ya kumsema akanuna akaondoka. Walipomwita kushoot video ya wimbo wa Chibonge akagoma kutokea hali iliyopelekea wakaondoa verse yake na kumweka gnako.
Akihojiwa na media bila kusema kilichomtoa kwa Abbah anawakana kwamba hakuwa ameingia nao mkataba wowote wa maandishi. Sasa mbona walimpora akaunti yake ya Instagram Kama ndiyo hivyo? Yaani bila mkataba wowote wakamshirikisha kwenye Iokote, Chibonge na kumrekodia nyimbo zingine? Mkataba ni lazima uwe umeandikwa?. Kisheria mkataba ambao ni lazima uandikwe ni wa ajira na kuuziana ardhi tu mingine inaweza isiandikwe na ikawa halali ili mradi kukiwa na ushahidi tu. Kwa hapa Kuna ushahidi wa kimazingira kuwa dogo alikuwa chini ya kina Abbah process na Hanscana na ameondoka kwa jeuri na kiburi.
Hanstone unapaswa ujirekebishe maana kwa staili hii hata labels kubwa unazozitegemea Kama Wasafi na Konde gang zitaogopa kukusaini maana jina lako limeshakuwa labelled kuwa ni kijana mwenye kiburi na dharau na asiye ambilika