kapistrano
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 1,244
- 453
kila binadamu na hulka yake hivyo basi busara inaitajika ktk swala hili na wala siyo kukurupuka
khaaaaaaaaaaaaaaaaaa wanaume wengine wakoje jamani? au anasilika ya udokozi?
sasa wewe wala usijali sometimes wanaume wa namna hiyo inabidi na wewe uwe bandidu...
akirudi tu mpige search, kwenye gari, wallet yake simu yake mkague mifukoni, nakwambia mara 3 tu ataacha mwenyewe
Hamna tatizo kukagua chochote cha mkeo na yeye ni ruksa kukagua chochote cha kwako, kwanini uogope na hakuna magendo humo ndani? Kila atakachokiona akiuliza atapata jibu lake tu. Tatizo hapo ni kwanini anakagua kwa siri? Kwanini hakagui mbele yako tu.
Jiamini Naima, mwache akague tu au kuna kitu hupendi akione?
Kwa hoja yako Kambaku hapo kuna kaukweli
Umeona eeenh? Haina haja kujisikia vibaya kama mwenzio akikagua pochi yako, mfukoni kwako au handbag yako, akiona kitu haelewi si anakuuliza na unamwambia tu? Sioni ubaya wowote kukagua, hata kama anakuamini au hakuamini ni haki yake kukagua tu. Kwanza tusiite kukagua ni kuangalia
Nadhani hapa Naima anazungumzia kukagua kwa siri na si kukagua maana hata password za emial na FB kampa.......swala ni kwanini anakagua kwa siri????
HAKUNA TATIZO LOLOTE NDIO HOBBY YAO JAMANI , ACHENI WAPEKUE ROHO ZAO ZI RIDHIKE. Nina uhakika wakishajificha akipekua akamaliza na wewe hujamuona anajiona bingwaaaa, raha mustarehe, muache mmeo afurahie bana. Si umeona ulivyomsema amenuna?Habari zenu wapendwa, Jamani naomba mnisaidie nina tatizo dogo tu ambalo kadri siku zinavoenda naona linanikwaza, mume wangu kila nikirudi home kutoka job au popote tu lazima atavizia handbag yangu ataipekua, nimeshamkutia karibia mara 15 sikumuuliza wala sikuchukia, juzi nimemkutia tena na hafanyi hivo mbele yangu anapekua kwa usiri hivo ata kumkutia inakuwa ni bahati tu, hiyo ya juzi nilikuwa nimetoka chuo nikaenda kuweka handbag room, nimerudi sitting room nimekaa kama dakika 5 tu akaja nayeye alikuwa chumbani, akachungulia pale sitting room kaniona niko busy na mtoto akarudi tena chumbani, namie hapohapo nikaingia chumbani nikamkuta tena busy anachambua handbag yangu, jamani ata kama kuna kitu anatafuta kwa mara hizo zote angekuwa ameshakipata, mimi binafsi nachukia na nilishawai kumwambia karibuni tu kama mara ya 13 hivi kuwa kwanini unapenda kufungua handbag yangu, unatafuta nin nikamuuliza vipi mimi nikiwa nakagua mifuko yako ya suruali kila ukirudi utajisikiaje maana wanaume hawabebi handbag, nikamwambia naomba uwe na imani na mimi hili jambo kwakweli linanikwaza, tangia nimemwambia hiyo juzi kaninunia mpaka leo hii eid imepita kimyakimya tu, jamani nisaidieni nifanye nini ili huyu mtu awe na imani namm au anatafuta sababu?
Amsterdam nimecheka sana hapo red daaah!anajua umekuja na mwanamme kwenye poch yako !!!!!
mtegee mavi ya mtoto au mtego wa panya akiingiza tu mkono atanasa thenunamwambia kuna panya huwa anaingia ndani ya pochi kukagua kila siku leo ndio 16 yake pale pale mwambie ulikuwa unatafuta nini? alafu kila siku mpe mwambie kagua basi ili nipeleke ndani au unaiweka juu ya laptop yake au mahali ambapi lazima ataigusa!
anajua umekuja na mwanamme kwenye poch yako !!!!!
mtegee mavi ya mtoto au mtego wa panya akiingiza tu mkono atanasa thenunamwambia kuna panya huwa anaingia ndani ya pochi kukagua kila siku leo ndio 16 yake pale pale mwambie ulikuwa unatafuta nini? alafu kila siku mpe mwambie kagua basi ili nipeleke ndani au unaiweka juu ya laptop yake au mahali ambapi lazima ataigusa!
Unajua nivigumu sana kushauri au kutoa hukumu,endapo kama umesikiliza upande mmoja tu!unajua huyo bwana anahofu fulani juu yako kukagua hbag yako kama mkewe sio mbaya chamsingi hunabudi kumuuliza huwaana tafiti nn? Ushauri wangu achana na mitandao ya vijana fb kwani yaweza kuvunja ndoa yako kama unayo jmf haina shida.kumbuka hakuna dwanaume asie na wivu naasiena hofu juu ya mwenza wake hasa kama anampenda kwa dhati.jaribu kujua nn tatizo hofu yake lake.pia inaekana wewe unakwenda na wakati kuzidi mmewako. Pia umri wake na wako kama ana 50yrs na wewe 28 to 30yrs mvumilie huo ndio wivu wa kizee.