Hamna kitu kirahisi, Mimba sio mchezo

Hamna kitu kirahisi, Mimba sio mchezo

mandunda,
Hahahahaha unafanana na baba k wangu tatizo yeye ni mlalaji sana sijui Hiyo kazi ya kuamka usiku kunipepea kama ataweza ila ya kuongea anaiweza tunaongea video call hadi napata usingizi
 
Aurora,
Thanks so much dear najitahidi sana nisiwe nahuzuni nikiona picha za kutisha naogopa now nimefuta ig kwanza maana unaingia unakutana na vitu hata hukuvitarajia
 
Jmn kulea mimba hapana, usiku nikiamka kukojoa mwili unauma utafikir ulikuwa unapigwa, njoo kiuno au mgongo mchana yesu ndo anayejua. Miguu kuvimba Hapo bado ukisikia stor za leba.. Mungu nisaidie April sio mbali

Sent using Jamii Forums mobile app

Nakutamania hongera mwaya mimi safari ndio kwanza mbichi basi hapa viugonjwa vya hapa na pale kila siku, naambiwa mpaka ikomae miezi minne huko ndio nitakua sawa
 
Hongera ukiona mwanamke kaitwa mama sio mchezo.
Hiyo ni mimba ,bado kujifungua,bado kulea kachanga,na kukalinda mda wotee .

bado kakifikisha 6. monrth na kuendelea ...plus kukosa usingizi na kuwa Kama teja mchana..
Ngoja niishie hapa.
 
Kule ndo baba lao...ohooo..MUNGU awasaidie wanawake wooteee wapate watoto ili wajue heshima ya kuitwa Mumy....

Amiin in sha allah Yani nachoomba tutoke salama tu wote ila uoga wa kwenda huko sina kabisa Au kwavile sijui bado muda
 
Madame S, Haya mambo ya kuweka mambo hadharan jamen wadada muache

Maana siri ni nying sana skuhiz sis wanaume tunazijua sabab mnaongea sana

Sasa mfano hyo ishu ya mikojo kutoka.mara mwengne aseme kule leba huwa mnakata gogo kabisa.kujamba etc

Mara mkiwa period sjui hata kucheka huwa mnajizuia sabab unaweza achia mambo ukicheka sana,mara ukipiga chafya sjui nini.

Sasa sis wanaume hzi detail hatutak kuskia jamen daaah...mambo ni meng mda ni mchache
 
Back
Top Bottom