Hamna kitu kirahisi, Mimba sio mchezo

Hamna kitu kirahisi, Mimba sio mchezo

Pisi kali

JF-Expert Member
Joined
Dec 31, 2019
Posts
1,235
Reaction score
2,545
Habarini wanaJF

Aisee kweli hamna kitu kirahisi hapa duniani, almost 2weeks ago nilikuwa naumwa siwezi kula yaani nakuwa na hamu na kitu then nikila kidogo tu najisikia vibaya +kichefuchefu, joto sasa hadi kizunguzungu naweza kuoga hata mara nane, na usiku nikishtuka ndio silali tena.

Namshukuru Mungu kuanzia juzi hali imebadilika ila sasa natamani vitu vizuri tu, maji nayaona mabaya hadi niyakamulie ndimu ndio napata taste hivi, kama hapa sasa hivi natamani burger.

Tatizo ambalo bado niko nalo ni usingizi, Yaani usiku mimi sina usingizi kabisa nitaangalia movie wee nitaperuzi mitandaoni hadi saa10/11 alfajiri ndio kausingizi kanakuja na saa1 asubuhi nakuwa macho.

Pia vijambo, yaani tumbo nahisi gesi muda wote na vijambo vinanuka, kila siku lazima niende haja kubwa sio chini ya mara 3.

Kingine nikiwa na stress tumbo linaniuma vibaya mno hasa nikiwaza vitu vibaya.

Kwa hali hii tuwaheshimu wa mama wote duniani jamani, najiliuza wale wenye watoto 5/6 ilikuaje? Maana ambao wametangulia uzazi wanasema mambo bado.

Wanaosemaga mimba si kazi, kazi kulea kumbe waongo vyote naona ni kazi

Pamoja na mapungufu yote MAMA YANGU NAKUPENDA SANA.
 
yataisha kukosa usingizi n kawaida ukiwa mjamzito

mimi niliuchukia wali, bamia na samaki nilichokua napenda ni chai na mkate tu

mimba ilipokomaa nilikua nikikosa wali maharage nachanganyikiwa, na mfano nikija kwako nikaskia harufu tu utanipakulia unataka hutaki

Nilipokaribia miezi ya mwisho mikojo inatoka kitone usiku silali miguu ilikua inajaa had inaniuma na nilikua natembea kama sina akili vizur lakini bado uchungu ukanitimba siku nne ndio nikajifungua kabebi gal kazuri zuri jaman Mungu akusimamie ujifungue salama, ufike mwisho wa safari yako salama upakate mwanao kupakata kitoto ulichokibeba ni raha kunakua na hisia ambayo haielezeki
 
Mimba ya kwanza hiyo ndio maana. Zingine itakuwa kawaida tu. Halafu wanawake wa siku hizi tunawadekeza mno.😀
 
Hongera mama kijacho,,, kitumbua kikianza kuvimbavimba unishtue maana napenda vitumbua vya wamama wajawazt
 
Madame S,
Mimi dagaa tu Yani sitaki kuziona wala kuzisikia nitatapika hatari nikiona hata maji yake

AMEEN M/mungu anisaidie tu nivuke salama ila imenipendeza nimekua mzuri ila nimepata chunusi kidogo usoni

Ni mimba ya kwanza ila hata siwazi leba nafikiria mtoto wangu tuvuke wote salama, nashukuru Mungu baba ake ananisapoti sana hata usiku nikikosa usingizi tunaongea weee hadi basi
 
Mimba ya kwanza hiyo ndio maana.
Zingine itakuwa kawaida tu.
Halafu wanawake wa siku hizi tunawadekeza mno.

Hahahahaha mmh kazi ipo yani kila kitu naona cha utofauti sio kudeka jamani mimba za sikuhizi zina vituko sana
 
harder king,
Hata itokee nini bado nitaendelea kumuheshimu tumepitia mengi sana pia kwa hali hii tu namshukuru Mungu na ye akifatiwa
 
Hahahahaha mmh kazi ipo yani kila kitu naona cha utofauti sio kudeka jamani mimba za sikuhizi zina vituko sana
hakuna cha mimba za siku hizi ni kujiendekeza, hayo mbona hatuyaonagi kwa mabeki tatu wakipata mimba?
 
Pisi kali, hahahhaa na raha ya mimba mwenye ujauzito wake awe karibu na wewe

me nilikua hivohivo siwazii leba nawaza mtoto wangu atakuaje? na jinsia nikawa naomba sana Mungu anipe jinsia nayotaka baba akealitaka yake me yangu lakini miezi ya mwisho ilivokaribia hasa wa saba wanasema mtoto anajigeuza kichwa kuwa chini nilijua nitajifungua nilikua namuomba sana msamaha Mungu yan natubu 😂😂😂

Baba yake naye alichanganyikiwa akajua nakufa kweli sim tulizipiga kama zote nikawahishwa hospital mana nilikua naumwa havielezek kulala siwez kukaa siwez kuinama siwez yan vurugu ni mwanangu wa kwanza amenipa experience ambayo sikuwahi kuifikiria hasa pale ndio napoambiwa umemuona mwanao ni wa kike hongera jaman nilitaman kumrukia yule mama nimbebejuu juu,

deka mwaya niwakat wako mwenzio nilinunua had nguo mama akawa ananambia ninunue tu baby shawl na kofia na soks miena vinguo kibao vya jinsia ya kike na akaja huyo huyo

lakini kulea mimbasio kaz kaz ni kulea mwana shughuli naiona 🙌 mikesha na vilio wewe.
 
Madame S,

Tatizo kazi sasa zinatutenganisha tunakua mikoa tofauti

Ajabu sisi wote tunapendelea mtoto wa kiume japokua tumesema mtoto ni mtoto huyo huyo Mungu atakayetuleteA amenambia nisiende kumuangalia ila nakiherehere sidhani kama nitaweza

Raha jamani kua na mtoto haswa hizo kelele ila mtoto wa kulia usiku ni kazi nyingine jamani

Kwahiyo hapa akifikia kugeuka nitaumwa?‍♀‍♀ mamaamaaaa weeee na hivi sijawahi kuumwa hata tumbo la period sipatii picha maana hivi vimaumivu kidogo tu nakua hoi (mimi ni muoga kuumwa)
 
ina mtu na mtu, wengine mtoto akigeuka na uchungu hapo hapo unapush, wengine ndio kina mimi unaumwa as if unataka kujifungua yan hata kuvieleza sjui nielezeaje, me nilipelekwa leba two times wakijua mwanzo ni uchungu na wala skujifungua mpaka ilipotim miezi tisa

uoga utaondoka wenyewe mimihad kumeza dawa skua naweza nilikua napenda syrup au vidawa vidogo kama piriton ndio nimeze ukinipa panadol sinywi naona yanisakama kooni lakini uchungu ulinifanya nijue kuitwa mama sio lelemama

mimi sikuangalia hata io jinsia na skuuliza na ultra sound nilipiga na nikapewa zawad ya mtoto wa jinsia nimtakae

kuhusu kulia n miez mitatu tu ya mwanzo ndiokanakua kanalia lia akifika minne kanapunguza aumitatu raha ya mtoto usiku alalemchana ndio asumbue nakumbukaniliwah kukesha mara mojatu nambembeleza had kunakucha kulea s mchezo

Pisi kali
 
Madame S,

Mimi dawa naogopa sana tangu nijijue nina ujauzito sijameza dawa yoyote nikiumwa nakunywa maji mengi sana basi na kulala.

Dah kweli kuitwa mama ni shughuri pevu jamani ndio maana watu huumiaga watoto wao wakipigwa na watubaki kwa shida kama hizi.,

Hongera dear wengine watoto hua walizi usiku tu mchana analala kama wa jirani yangu hapa
 
Pisi kali, asante mwaya

me nashukuru sasa hivi mchana halali usiku kinalala na akilia sana ujue nimikojo aunjaa

umeona eh mtoto anauma mtu ajeampige tu bure bure wakatniliteseka sikuya kumleta dunian lazima uumie

hata hivo haishauriw unapokua na hali hio kujinyewa midawa tu bila ushaur wa daktar usiache kuhudhuria clinic
 
Back
Top Bottom