Hamasa ya sensa ikoje hapo ulipo?

Makala Jr

JF-Expert Member
Aug 25, 2011
3,395
1,110
Zimebaki siku chache sana kabla ya zoezi la sensa kuanzia usiku wa tarehe 25-26,August 2012. Kwa utafiti mdogo niliufanya Dar es salaam wiki iliyopita...elimu ya uraia ilikuwa bado inahitajika sana.Katika kuwahoji watu kuna uelewa mdogo sana. Kuna watu wameaminishwa kwamba SENSA ni mpango wa freemasons wa kujua idadi ya watu ili wajipange vizuri namna ya kuitawala dunia. Pia kuna wananchi wabishi sana...kuna watu wanadai sensa ya nini kama hawaletewi maendeleo kwa miaka yote waliyowahi kuhesabiwa? Inasikitisha kuona hamasa za kampeni za kisiasa zinakuwa na nguvu kuliko zoezi hili la kitaifa.Kumekuwa na malalamiko ya awali kwamba baadhi ya wale waliochaguliwa kuendesha sensa hawana uwezo wa kutosha kwani rushwa ilitumika. Kuna ujinga ulioenezwa ili kukwamisha sensa ikiwemo misimamo ya kidini,imani potofu na vitisho vya kugomea sensa.Saizi nipo Mbeya mjini kuna matumaini ya zoezi kufanikiwa.Je hapo ulipo hamasa kwa wananchi ikoje?
 
Katika wale ninaokutana nao kwa siku nzima sijasikia hata mmoja akigusia sensa. Naona tu matangazo kwa TV. Bila shaka kila mmoja anajua na sana ni wale wakuu wa familia ndio wajibu maswali. Hakuna kupangwa foleni hivyo that is not an issue to most people. Watu wanahangaika na kula yao.
 
Kuna tetesi kwamba baadhi ya mawakala mkoani Geita wamegoma kutokana na kutolipwa posho, je ni kweli? Naomba taarifa kwa wadau waliopo huko.
 
hapa nilipo wengi hatushiriki, mpaka kipengele cha dini kiwepo.. tena kma wooote u.
 
Leo nilikuwa Madanga/Pangani nikaulizia hamasa ikoje jamaa akasema mkuu wa wilaya alishafika kuhamasisha na watu wakampotezea akaondoka bila kuwahamasisha mashaka makubwa maeneo ya waislam sensa haitofanikiwa
 
Mjini Iringa...madiwani wameagiza watendaji wa vijiji na Kata kusimamisha zoezi la kukusanya michango ya ujenzi wa shule ili kuwafanya wananchi wakae kwa amani katika makazi yao wakisubiri kuhesabiwa!
 
mkoani geita Wilayani mbogwe uhuni,ukatili na usanii vnaendelea kufanyika.Jana wamewatimua wanasemina eti kisa ni warund,kwa vgezo wamezaliwa tz,wamesomea tz na wanaish tz,vyet walikaguliwa na maafisa usalama na jopo la viongoz ngaz ya wilaya na waka qualify mafunzo.Jana siku ya 8 kwa dodoso refu wanatimuliwa!Cha kushanganza jana et tukapewa ka elfu 70 but hbq ndo hyo!
 
hamasa iko chini, mi sihesabiwi mpaka kipengele cha dini kiwekwe.
 
Back
Top Bottom