Tanganyika yetu mbona ipo? Hakuna sababu za kuidai. Kama mwungano hauwezekani kilichobaki ni kuwafukuza tu Wazanzibari warudi kwao.Heko Afande Luten,
Kifupi tu nikuwa ingekuwa jambo labusara sana kama watanganyika mukadai Tanganyika yenu ambayo Mwalim aliipoteza kuliko kudai katiba mpya? Hili lina umuhimu sana kwa historia ya nchi yenu na kwa vile mulipigania uhuru wa nchi yenu Tanganyika sio Tanzania? 11 december 1961 sasa kuna faida gani yakudai katiba wakati hamuna nchi? Wzanzibar akina Hamad Rashid na wenzake wao wana nchi yao yenye Rais wao,katiba yao,Bendera yao,wimbo wataifa wao,mahkama zao,na mipaka ya nchi yao. Sasa kikulacho kiko nguoni mwenu, Mwenye akili timamu anajuwa hakuna mwendazimu hata moja Zanzibar anae ipenda ccm na kila siku Wzanzibar wanomba ifee foroho au mushukuwe wenyenu Wabara ss tumechoka na vitimbi vyao. Na huo Muungano unaishi Zanzibar kwa nguvu ya kijeshi tu lakini wazanzibar imekuwa kero.
Mimi hushangazwa na Chadema kusema watakwenda mahakamani kuishtaki Cuf ktk mabadiliko ya 10 ya katiba ya Zanzibar, Kwa nini musimshtaki Mh Kikwete? au kulishtaki Baraza la Uwakilishi kama muna ubavu? muna juwa kwa nini katiba ccm hawataki kubadilisha? nikuwa haki zote za Zanzibar zitarudi Zanzibar na ukoloni wa kutawaliwa Wzanzibar basi. Wzanzibar tunasubiri kwa hamu kuiona Tanganyika yenu munaifufua na kusimamia haki zenu za Tanganyika zisizo za Muungano, hii niaibu kukataa nchi yenu mulio ipigania uhuru na kupenda ubatizo wa Tanzania.
Case closed.