Hamad Rashid: Mtu mzima hatishiwi nyau!

Dr Matola PhD

JF-Expert Member
Oct 18, 2010
56,395
92,720
Hamad Rashid: Nitapambana na Seif hadi kieleweke

Joseph Zablon

MBUNGE wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohamed amesema anasubiri kwa hamu barua ya kuitwa na Kamati ya Maadili ya chama hicho, akijinasibu kwamba, “mtu mzima hatishiwi nyau.”

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Hamad Rashid alisema anasikia tu katika vyombo vya habari kuhusu suala hilo, lakini binafsi hajaelezwa chochote na Naibu Katibu Mkuu wa CUF Bara, Julius Mtatiro jambo alilosema ni ukiukwaji wa katiba ya chama hicho.

“Kilichofanyika ni ukiukwaji mkubwa wa katiba, kwani kimsingi nilipaswa kuitwa katika vikao vya chama na sio kuhukumiwa na kushutumiwa kupitia vyombo vya habari. Nasema na uandike kwa wino mweusi kabisa kuwa, mtu mzima hatishiwa nyau,” alisema.

Mbunge huyo aliyekuwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni alisema pamoja na kuisubiri barua ya kuitwa katika kikao hicho cha baraza la maadili, atapambana na Maalim Seif kuwania ukatibu mkuu CUF hadi kieleweke.

Kauli ya mbunge huyo, imekuja siku moja baada ya Naibu Katibu Mkuu Bara, Julius Mtatiro kutoa kauli kwenye mkutano na wanahabari akidai kuwa kuwa kitendo cha Hamad Rashid kufanya mkutano na wanachama wa Tawi la Chechnya, Manzese bila kutoa taarifa ofisi za chama makao makuu ni kwenda kinyume na taratibu za chama.

Mtatiro alisema kuwa katika mkutano huo ambao ulivamiwa na walinzi wa chama hicho wa ‘Blue guard’, Hamad Rashid aliungana na wajumbe wengine wa baraza kuu la chama hicho kuendesha mikutano hiyo kinyume na utaratibu wa CUF na kudai kwamba anachofanya Hamad Rashid ni ‘umafia’ kwa kuwa ukatibu mkuu hautafutwi kwa njia hiyo.

Lakini, jana Hamad Rashid alisema kuwa CUF ina utaratibu wake katika kushughulikia mambo ikiwa ni pamoja na vikao kwa kujibu wa katiba ya chama hicho na siyo kupitia vyombo vya habari.

Alisisitiza kuwa atawania nafasi hiyo na kwamba nia yake hiyo aliieleza katika mkutano wa hadhara na wapiga kura wake katika Jimbo la Wawi aliosema wamemuunga mkono.

“Hakuna mjadala ni lazima niwanie nafasi hiyo ya ukatibu mkuu wa chama kwani ni haki yangu ya kikatiba na sifa ninazo za kufanya hivyo,” alisema.

Katika hatua nyingine, Mjumbe wa Baraza Kuu la CUF ambaye pia ni Mbunge wa Gando, Khalifa Suleiman Khalifa alisema kinachotokea ndani ya chama hicho anakisikia tu katika vyombo vya habari na hajaelezwa kitu gani kinachoendelea.

“Sijui chochote, nasikia tu katika vyombo vya habari licha ya kuwa mimi ni mjumbe wa baraza kuu taifa,” alisema.Sakata hilo linatokana na vurugu zilisababisha watu kadhaa kujeruhiwa kwa kukatwa mapanga zilizozuka wakati Hamad Rashid alipokwenda kufanya mkutano na wanachama wa Tawi la Chechnya lililopo Manzese jijini Dar es Salaam.
 
Ngoma inogile!HAMAD RASHID usirudi nyuma tena uko right hakuna katibu mkuu wala mwenyekiti wa maisha ni lazima wawe tested kila baada ya muda fulani,pigania haki najua wako wengi nyuma yako sema wewe umekua jasiri tu kumkabili swahiba wako seif ambae anaonekana kama mungu wa wapemba na cuf kiujumla!
 
CUF imekuwa na usingizi wa kwa kuvishwa kilemba cha ndoa ya mkeka na huku ikijua kuwa bwana mwenyewe haaminiki na kwa hakika

hata hiyo ndoa imefungwa kwa staili ya funika kombe mwanaharamu apite na mme mwenyewe mzee kabakia tu na sauti inayoonesha ni

mume. Mwanasiasa mahiri hakubali kuwa katika ndoa hii ya CHICHIEMU na CUF. Wakikusumbua hamia kwa wanaume ili upambane kiume.:bange:
 
huyu mpemba HR anahangaika nini huku bara, si aende kugombania huko visiwani, kumbe Tanganyika ni tamu
 



Hamad-Kikao(1).jpg

Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohammed


Kikao cha Kamati Tendaji ya Taifa ya Chama cha Wananchi (CUF) kimekwama kutoa adhabu dhidi ya viongozi wake 14 wanaotuhumiwa kula njama ya kukivuruga chama hicho akiwemo mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohammed.
Kikao hicho cha siku mbili kilianza kufanyika Desemba 30, katika hoteli ya Mazson kikiwa chini ya Mwenyekiti wake Katibu Mkuu wa Chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad, huko Shangani mjini Zanzibar.
Akizungumza na Waandishi wa habari baada ya kikao hicho Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Julius Mtatiro, alisema kikao hicho kilipata nafasi ya kupokea taarifa ya hali ya kisiasa ndani ya chama kutoka kamati ndogo ya Ulinzi na Usalama ya chama hicho.
Alisema Taarifa ya kamati hiyo iliwasilishwa katika kikao hicho ambapo ilijikita zaidi katika njama zinazodaiwa kufanywa na viongozi 14 wakiongozwa na Muasisi wa chama hicho, Hamad Rashid Mohammed.
Naibu Katibu huyo alisema kamati hiyo baada ya kupokea taarifa na kujadiliwa kwa kina kimeamua kuitisha kikao cha dharura cha Baraza kuu la uongozi ambalo litawajadili viongozi hao kabla ya kutoa maamuzi yake.
Hata hivyo alisema kwa kuzingatia kifungu cha 63 Baraza Kuu la Uongozi ndiyo limepewa mamlaka ya kikatiba ya kulinda na kuendesha heshima ya chama ya chama hicho.
Aidha, alisema Kamati hiyo imeamua kuitisha kikao cha Baraza Kuu cha dharura kwa vile chombo hicho ndicho chenye mamlaka ya kuwachukulia hatua za kinidhamu viongozi na wanachama wanaotuhumiwa kwa makosa mbali mbali kwa kuzingatia masharti ya Katiba na kanuni za chama hicho.
Alisema kwamba Baraza Kuu la uongozi limepewa mamalaka hiyo kupitia kifungu cha 63 (1)(j) na kwamba viongozi wote 14 watajadiliwa na Baraza hilo katika kikao kilichopangwa kufanyika Zanzibar Januari 4, mwaka 2012.
Mtatiro alisema kikao hicho kitasikiliza tuhuma zinazowakabili viongozi hao na kuwapa nafasi ya kuwasikiliza na kujitetea kabla ya kuchukua hatua yoyote dhidi yao.
Aliwataja viongozi wanaotuhumiwa kula njama ya kuivuruga CUF ambao pia wajumbe wa Baraza Kuu la uongozi kuwa ni Hamad Rashid Mohammed, Doyo Hassan Doyo, Shoka Khamis Juma, Juma Said Sanani na Yasin Mrotwa.
Wengine Mwenyekiti wa CUF Wilaya ya Temeke, Mohammed Albadawi, Katibu wa CUF, Wilaya ya Ilala, Mohammed Masaga, na Yusufu Mungiro, ambaye ni kiongozi mwanadamizi pia katika Wilaya hiyo.
Aliwataja wanachama wengine watakaojadiliwa na baraza hilo kuwa ni Ahmed Issa Tamim Omar, Amir Kirungi, Ayubu Kimangale na Nanjase.
Kikao hicho kimefanyika chini ya uangalizi mkali wa askari wa Blue Guard ambapo juzi kililazimika kumalizika usiku huku baadhi ya wanachama wa CUF katika manispaa ya mji wa Zanzibar wakitaka Hamad Rashidi na wenzake wafukuzwe uongozi kutokana na kwenda kinyume na maadili ya chama hicho.
Kwa mujibu wa Idara ya Nidhamu na Maadili ya CUF, Hamad alikuwa anakabiliwa na tuhuma 11 za ukiukwaji wa Katiba ya chama hicho.
Hata hivyo, Rashid alitangaza kutokuwa na imani na Mwenyekiti wa kamati tendaji ya Taifa ya chama hicho, Maalim Seif Sharif hamad, baada ya kunasa kile alichokiita waraka wa siri wa kiongozi huyo unaoeleza namna ya kumfukuza uanachama bila ya kuzingatia misingi ya katiba ya chama hicho na Demokrasia.
Awali Kamati ya Nidhamu na Maadili ya chama hicho ilikaririwa ikisema iwapo Hamad na wenzake hao watapatikana na hatia, kamati hiyo inaweza kutoa mapendekezo kwa Baraza Kuu la uongozi kutoa onyo la karipio au kuwafukuza uanachama.
Mgogoro wa CUF umeibuka baada ya viongozi waandamizi wa chama hicho wakiongozwa na Hamad Rashid kulalamika kuwa chama hicho kimepoteza nguvu na mwelekeo wa kisiasa kwa kasi, matumizi mabaya ya fedha na kutaka baadhi ya viongozi wake kuondolewa katika nyadhifa zao kutokana na kukabiliwa na majukumu mengi ya kitaifa akiwemo Makamu wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad.



CHANZO: NIPASHE JUMAPILI


 
Demokrasia ianzie kwenye vyama, tuondokane na miungu watu 'untouchables' hongera hr kwa uthubutu!
 
Hamuwezi kuivuruga CUF. Tuko imara kabisa. Hamad Rashid na wenzake wana haki ya kukaa au kuondoka. Nobody is invincible in CUF,.

Chama kipo Imara kabisa na tunaendelea kuwatumikia wananchi wetu.
 
CUF kama mnataka chama kife mfukuzeni Hamad Rashid,acheni fitna na majungu.viongozi wa juu wa CUF nawaomba myafanyie kazi hoja na maoni ya Hamad na wenzake msiwajadiji wao kama wanachama.mnachokifanya ni woga na ni ujinga mkubwa.mimi si mwanachama wa cuf na wala sitarajii kujiunga nanyi lakini nawapa tu mtazamo wangu na pengine ni mtazamo wa watanzania wengine pia.
 
cuf onyesheni kuwa mmekomaa kisiasa kwa kumaliza mambo yenu kistaarabu.msifukuzane
 
tatizo la cuf ninini? kipi hakizungumziki? kinachoitwa mgogoro nini? mawazo na maoni ni dhambi? je kuhoji jambo ndani ya cuf haramu? Sefu na Hamadi wote ni muhimu kwa cuf tusiwatumie kuivuruga cuf tofauti zao za mitizamo ya kuimalisha cuf wapambe wanazitumia kutengeneza mgogoro bandia kwa kuhofia kupoteza maslahi
 
Nashukuru sana Mtatiro amekuja hapa JF na kutujuza mapema kabla ya habari hiii kutoka. Na alitueleza utaratibu wa chama chake mapema kabla ya kikao laa sivyo tungeamini habari ulokolezwa na chunvi kibao..
 
Huyo HR na aunde chama chake maana kwa mara hii hatumpi Mpemba ukatibu mkuu. Tunataka angalau awe mtu wa Unguja au Bara.

Hata akiambiwa abaki kwenye chama lakini ataota kuupata u KM.
 
Back
Top Bottom