Halotel wana chuma ulete saa hii. Nihamie wapi wakuu?

Halotel wana chuma ulete saa hii. Nihamie wapi wakuu?

Dah
Mimi nimehangaika na line zote (airtel, halotel, tigo, ttcl, vodacom) lakini sasa nimeamua kurudi njia kuu. Vodacom ni baba lao.
Mpaka nimepitisha maamuzi ya kila mwezi najiunga kifurushi cha 40,000 napata gb 40. Nikirudi mjini ntaanza kutest ttcl maana ipo mjini tu.
bora tu ubakie huko huko voda ni gharama ila uhakika unainjoy sio huku kwa halotel bei nafuu ila wizi mtupu kuuziwa data bundle feki ama airtel speed ya kobe. Hawa ttcl sitopoteza muda wangu kuhangaika nao maana vocha yenyewe tu kuipata ni lazma niisafirie mpaka majengo.
 
Nimenunua kifurushi cha wiki chenye mb 1200 lakini zimeisha ndani ya nusu saa tena nimeingia jamii forums tu basi. Halafu huduma kwa wateja kuwapata ni ishu kweli kweli.
Inategemea,inawezekana unatumia device ambayo ina "autoupdate" na ukute ilikuwa haijaupdate kitambo!
Nenda kwenye Settings tafuta eneo la Update then badilisha ili isifanye Update automatically!
Kwa hiyo kabla ya kuhitimisha kwamba jamaa wanatatizo angalia device yako kwanza!
Unaweza kumaliza hata Gb10 kwa nusu saa tu
 
nilikuwa na MB 260 mikawa na,download movie ya MB 190 cha kushangaza mb ziliisha kabla sijamaliza kushusha huu ni wizi.
 
Dah wanakula bando kama hawana akili nzuri.
Nishaurini laini nyingine
Mkuu, mm najuta kununua modem ya halotel na hivi sasa hakuna mtu wa kumuuzia tena....kila mtu ameshtukia wizi.

Wizi wa hawa jamaa ni pale wanapokupa bundle ya 450 MB halafu wanakuambia eti 100 itakuwa ya usiku bila kusema ni usiku wa kuanzia saa ngapi hadi saa ngapi na ikifika huo usiku ukiwasha modem hupati kitu.

Halotel ni qumer sana jamani tuhamie voda.
 
Nimenunua kifurushi cha wiki chenye mb 1200 lakini zimeisha ndani ya nusu saa tena nimeingia jamii forums tu basi. Halafu huduma kwa wateja kuwapata ni ishu kweli kweli.
Mkuu Halotel sio tu kuwa ni wezi lakini pia ni qumer wa kutupwa! Achana nao, hamia voda.
 
Inategemea,inawezekana unatumia device ambayo ina "autoupdate" na ukute ilikuwa haijaupdate kitambo!
Nenda kwenye Settings tafuta eneo la Update then badilisha ili isifanye Update automatically!
Kwa hiyo kabla ya kuhitimisha kwamba jamaa wanatatizo angalia device yako kwanza!
Unaweza kumaliza hata Gb10 kwa nusu saa tu
Simu yangu nilisha set iwe ina update kwa wifi only. Auto update ipo off tokea kitambo. Toa sababu nyingine labda ila sio auto update. Na sikuingia site yoyote ya ku stream video zaidi ya jamii forum tu. Na nimeingia kwa nusu saa tu wananitumia sms kuwa nimebakiwa na mb 5 wakati nilijiunga kifurushi cha 1.2gb
 
Back
Top Bottom