Halotel baada ya kusifiwa kua na huduma nzuri lakini saizi ni tofauti kabisa spidi yao ya intanet imepungua sana afu wanakula Mb unaweza sema simu imetoboka znavujia chini mwanzo Mb 600 nilikua natumia hata kwa siku 3 lakini saizi hata masaa 24 hazimalizi muda sio mrefu natupa line lenu maana nilinunua kwa ajili ya Mb
Nilidhani ni mimi pekeangu, mb sikuhizi hazikai pamoja na kwamba wamezipunguza kiasi flani ila nina imani hata nikiweka data manager ikawa inanipa records za data kiasi gani nimetumia toka nimejiunga bando lao, ita detect wizi wanaoufanya!
Hawa jamaa watapoteza wateja maana walivyoanza walikuwa safi sana lakini sasa huwezi amini mb zinavyokimbia. Unatumiwa msg zimebaki mb 5 lakini chini ya dakika moja unaambiwa salio lako ni mb 0. Soon nitawakimbia.
Washenzi af sasa wanachokifanya yani, siku hizi nikiingia youtube tu hata kuangalia nyimbo moja tu, kama nilijiunga nusu saa iliopita basi masaa 24 hayafiki mb zinakata. Ila usipotumia youtube bando linavumilia hata siku mbili.
Hili nakubaliana na ww kabisa lakin sasa airtel kwa maeneo ambayo wengine tunaishi ni tatizo ktk internet tunalazimika kutumia halotel ....mwisho tunapata maumivu na vifurushi vya chuo wamepunguza mb yaani tafrani tupu