Halotel internet mnakera sana, mwogopeni Mungu

Halotel internet mnakera sana, mwogopeni Mungu

jaman inategemea na mahali ulipo ,mimi natumia kwa pc iko vzuri toka mwaka jana baada kuipiga chini airtel
 
Halotel iko njema sema sio kama ilivyokuwaga huko awali.
Imeanza shida flaani yani kama yale yale ya tigo inashika kwenye mpera ukisogelea mnazi haishiki ama ipo slow mpaka inakera at times!
 
Tena bora hata halotela kuliko 071 hawa ndo balaa zaidi insure ni kuhamia TTCL
 
nimebishana sana na watu humu ndani

mimi nilihama voda sababu ya gharama zao zipo juu.
nilivyoenda halotel siku hiyo hiyo line ya halotel nikaiweka dirishani huku 2000 yangu ikienda bure.Halotel net yao ipo slow mno ase

mitandao yenye kasi Tanzania

1.voda hii inaongoza ila tatizo lao ni gharama
2.Airtel
3.Tigo ila hawa wanazingua kimtindo nimewakimbia sababu wanakera mara wasipatikane mara wapatikane

nimerudi voda ila majamaa ni mafascist ''mabepari'' wanatukamua vibaya sana ila net yao ina kasi ya ajabu
 
Tutawakimbia mtabaki na net yenu mtumie wenyewe icho ki 3G chenu. kwa wale wanaotumia computer, unanunua bandle tufanye ya siku, wiki au mwezi, unachokutana nacho hata kinyonga hana mwendo wa polepole kama huu, na inakata kila wakati, ukidownload kidogo tu video haifiki popote, tafadhali, TTCL na makampuni mengine yenye faida kwa watz pigeni mbio muwafunike hawa jamaa, wanaudhi kupita maelezo.ni kama mnatuibia pesa zetu tu sasa.
wew na wengine shtuka AIRTEL ndyo kila kitu kuna sim kad mpya za vyuo zinauzwa kimya kimya bila promo kama mwitaji nichek +255687620807 tena unajiunga popote na kingine wana vocha kama vocha special za chuo kama unataka kudownload kuna vocha ya.buku unapata GB10 ndani ya siku tatu na kuchonga bure sema inakuwa inatumika usiku kuanzia saa nne......umewah ona wap kwenye kuongea sasa hebu check
jinsi unavyopata dakika za mitandao yote hafu linganisha na mtandao unaoutumia

1=sh.500 dk 20
2=sh.650 dk 35
3=sh.1009. dk 60

,wap umeona hyo....
 
Hivi Airtel leo ni kwangu tu jamani au?
Actually ni tokea jana usiku saa 4 hadi sasa.
Network inakatakata taabu tupu.
netwok kidogo imeyumba nasikia kuna marekebisho....airtel ni nowma hao wengine wanaiga tu sis ni wazee wa promo za kimya kimya
 
Kuhusu speed ni eneo na eneo wanachoniboa mb zao hazikai GB moja ya halotel nainigia jamii forum na instagram kidogo inakata wakati airtel natumia had wiki
umeona eeh na bado mpya huo ngoja uzeeke mtakiona cha moto
 
nimebishana sana na watu humu ndani

mimi nilihama voda sababu ya gharama zao zipo juu.
nilivyoenda halotel siku hiyo hiyo line ya halotel nikaiweka dirishani huku 2000 yangu ikienda bure.Halotel net yao ipo slow mno ase

mitandao yenye kasi Tanzania

1.voda hii inaongoza ila tatizo lao ni gharama
2.Airtel
3.Tigo ila hawa wanazingua kimtindo nimewakimbia sababu wanakera mara wasipatikane mara wapatikane

nimerudi voda ila majamaa ni mafascist ''mabepari'' wanatukamua vibaya sana ila net yao ina kasi ya ajabu
Mkuu mimi nilichogundua kasi ya internet ya mtandao inategemea na mahali,.
mfano ipo sehemu voda ina kasi kuliko mitandao yote,

Na ipo mahali Tigo iko fresh na mitandao mingine inazingua,

Niliwahi kaa mahali,hapo aitel iko vzuri yaan hapo si tigo si voda,nilipo hama kwenda mahali pengine ikaanza kusumbua

kwahiyo inategemea na mahali ulipo
 
Hili linaweza kuwa kweli kabisa,
Sjajua labda watumiaji wamekuwa wengi,manaake kipindi cha nyuma ilikuwa vizuri mno,saizi ni taabu kasi imekuwa ndogo sana! Nimewavumilia kwa mda sana hawa halotel.

Sasa itabidi nirudishe Majeshi nyuma-Vodacom.
 
Ila tuwe wakweli, katika mitandao ya simu yote ni hovyo ila Halotel kuna uafadhari kidogo.

Ninatumia laini yao ya Chuo, Tsh 500 unapata Mb 600 kwa wiki, Tsh 1500 unapata MB 1220 dk 15 kupiga mitandao yote na dakika za kutosha kupiga Halotel kwa wiki.

Na kasi yao ipo vizuri hata kama itasoma 2G lakini bado utadownload vizuri tu bila shida.

Tofauti na mitandao mingine, Kasi ya 3/4G ni ya konokono ikibadili 2G ndio hudownload chochote na pengine isifunguke kabisa itabakia Loading....

Wengine wanasema Bundle zao zina wahi kuyeyuka, hii ni kwasababu ya kasi yao kubwa.

Sasa chagua uende ambako bundle haliwahi kuyeyuka na kasi yake ni ndogo na si ajabu mpaka muda wake unaisha haujatumia hata Mb 100 kati ya 500 ulizojiunga au uende ambako bundle linawahi kuyeyuka ila linaisha kihalali.
Mm nilisharudi voda. Halotel walikula gb 2 kwa masaa mawil na kuangalia kinachokula gb hzo ilikuwa ni google plus ambayo hata sikuifungua . Nikaona isiwe tabu. Halotel ni wez kupindukia
 
Labda Dar ndo inawasumbua kwa kweli, mi huniambii kitu kwa halotel, speed kama 4G naunganisha WiFi katika TV kutokea katika simu naangalia YouTube inakwenda kama nimeweka Deck haikwami hata nukta.

Mitandao kongwe kwangu ni kwa ajili ya kupokelea na kupiga tu, Data ni Halotel baaasi.
Kama mimi kwa Halotel huniambii kitu
 
Mkuu mimi nilichogundua kasi ya internet ya mtandao inategemea na mahali,.
mfano ipo sehemu voda ina kasi kuliko mitandao yote,

Na ipo mahali Tigo iko fresh na mitandao mingine inazingua,

Niliwahi kaa mahali,hapo aitel iko vzuri yaan hapo si tigo si voda,nilipo hama kwenda mahali pengine ikaanza kusumbua

kwahiyo inategemea na mahali ulipo

Uko sahihi kabisa,maeneo ya posta kwa hapa Dsm,tigo na voda wako vizuri sana lakini ukitoka nje ya posta ni shida tupu. Mimi natumia halotel kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.
 
Uko sahihi kabisa,maeneo ya posta kwa hapa Dsm,tigo na voda wako vizuri sana lakini ukitoka nje ya posta ni shida tupu. Mimi natumia halotel kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa.
umeona eee ilo mie nimeligundua ,yaa ww unaweza ulalamikia mtandao kwa maeneo yako ,mwingine mtandao huo huo akawa anapeta
 
Tcra fuatilieni hawa jama wa halotel walianza vizuri sana.Ila kwa sasa ni wezi kuliko hata tigo.Wanatuibia sana kwenye bundle za internet.
 
Back
Top Bottom