SIsi watumishi walimu tuliwasilisha fomu zetu za likizo tangia mwezi wa 11 mwanzoni, ila mpaka tarehe ya leo hatujalipwa wakati likizo imeshafikia nusu. Tunaomba mkurugenzi atueleze likizo tunaendaje? Kwanini amekalia pesa zetu na hataki kutulipa. Mh. Mchengerewa wewe ni jembe tegemeo la mh. Rais wetu Dr. Samia Suluhu Hassan, tunaomba msaada wako tupate haki zetu. Tunaomba ummulike huyu mkurugenzi wetu, wanajiona wako mbali na Dodoma wanajifanyia wanavyotaka.