Halima Mdee aomba radhi Bungeni kwa kutoa matusi

Halima Mdee aomba radhi Bungeni kwa kutoa matusi

18157268_1626691130705052_3397560189958886604_n.jpg
 
Binadamu ni wa ajabu kweli, alipo rudi toka India alikuja na maneno ya kutia moyo sana kuwa amebadili tabia. Kumbe pale alikuwa bado anakumbukumbu ya hospitali,sasa kasahau na kiburi juu. Mdee alistahili kumwita vile

Ametumia vyema nafasi aliyoomba,najiuliza upande wa pili ukiwatukana Upinzani wataomba radhi??Je Spika kwa lugha ya kifedhuli aliyoanza kuitumia je,ataomba radhi??

Je akina Musukuma na Kibajaji ambao huwa wanatukana sana upinzani wataomba radhi??Ni kuweka record sawa,kuna watu watakuwa wamefurahia lakini nyuma yake waanze kujiangalia kama wanastahili radhi hiyo.
 

Mbunge Halima Mdee kaomba radhi kwa kauli aliyomtolea Spika Ndugai bungeni kwenye uchaguzi wa EALA.

Huo ni mtego mkubwa sana kwa Ndugai kwani kama tabia alizoonyesha kwenye uchaguzi hataziacha matusi yale atatukanwa tena na wabunge wengine.

Ni wakati sasa naye kujiangalia jee anatenda haki au anafanya mambo yanayo stahili kuitwa tena "fala'?

Spika na naibu wake hata na wenyeviti wa Bunge wanapaswa kutenda kwa kufuata kanuni na kuondoa upendeleo ili kujiepusha na lugha za kuwadhalilisha.

Aiseee umenena point mkuu" zipo tabia zinazopelekea kutukanwa!!!
 
Mimi binafsi sishabikii matusi lakini pia siungi mkono vitendo vya viongozi wa Bunge vyakuwadhalilisha Watanzania asa wawakilishi wetu,kumbuka Bunge sio chombo cha ccm nimali ya Watanzania.Hongera Halima kwakuomba radhi ila tunamtaka na Ndugai awatake radhi wapinzani.
 
Ndugai ana masifa kama wakuja vile ... mara faru Ndugai " hammjui faru ndugai" anauliza.... mara Bashite ndo nani.... mara ngoja tuone kama wagombea wa cdm wanajua ki english kama hawa wa ccm..... utani wa kijinga unafanya kiti cha spika kidhalaurike..... hasa mtoa utani wa kishamba anapo kuwa ndo mwenye Nyumba... sawa na baba home akiwa na mambo ka kijinga jinga na kutoa utani usio na maana......
 
Tabia za Ndugai ni za ki K, K tu.

Kupiga wenzie fimbo kisogoni
Kuipendelea CCM
Kukandamiza demokrasia etc
Nakubaliana na wewe bujibuji, ingawa siungi mkono hiyo k, k. Kwakuwa Sijui maanayake.

Nadhani huyu Ndugai hakustahili kuwa spika kwa kitendo alicho fanyaga katika mchakato wa uchaguzi kwa kumpiga mtu na fimbo.

Alionyesha udhaifu mkubwa sana hakufaa kuwa spika.
 
Mimi si mpenzi sana wa Halima Mdee, na huwa simshabikii sana maana mara nyingi yuko kisiasa zaidi kuliko kimaendeleo.

Huku Kawe ni mbunge wangu lakini HAKUNA mradi ulioanza kwa ushawishi wake, na hii ni awamu yake ya pili.

Kitendo cha Halima Mdee kuombavradhi kwa lugha isiyostahiki bungeni imenipa moyo.
Mtoto kaanza kukua kiakili!

Anaweza kuona kama ni suala dogo, lakini kitendo kinarudisha imani ya usikivu.

Sasa hata akienda wizara ya ujenzi su Halmashauri kuomba na kufuatilia mradi wa barabara atasikilizwa.

Hongera Halima.
 
Hiki ndio nini tena? msamaha wenye masharti?
 
Nimefurah sana kwakweli Mbunge Halima Mdee amefanya jambo la muhimu sana katika maisha yake kama mwanadam anakosea na anajua kama amekosea ni jambo la kumshukuru sana mungu na faraja sana kwa wanadam na mungu. Big up Halima Mdee. Wewe sasa ni mkomavu wa kisiasa.
 
Mimi binafsi sishabikii matusi lakini pia siungi mkono vitendo vya viongozi wa Bunge vyakuwadhalilisha Watanzania asa wawakilishi wetu,kumbuka Bunge sio chombo cha ccm nimali ya Watanzania.Hongera Halima kwakuomba radhi ila tunamtaka na Ndugai awatake radhi wapinzani.

Siyo Ndugai tu hata Tulia na Wabunge wote wa CCM wenye tabia ya kutukana wapinzani
 
Mimi si mpenzi sana wa Halima Mdee, na huwa simshabikii sana maana mara nyingi yuko kisiasa zaidi kuliko kimaendeleo.

Huku Kawe ni mbunge wangu lakini HAKUNA mradi ulioanza kwa ushawishi wake, na hii ni awamu yake ya pili.

Kitendo cha Halima Mdee kuombavradhi kwa lugha isiyostahiki bungeni imenipa moyo.
Mtoto kaanza kukua kiakili!

Anaweza kuona kama ni suala dogo, lakini kitendo kinarudisha imani ya usikivu.

Sasa hata akienda wizara ya ujenzi su Halmashauri kuomba na kufuatilia mradi wa barabara atasikilizwa.

Hongera Halima.

Hope na Supika na Naibu Supika,Musukuma na Kibajaji na wao wataomba radhi kwa matusi wanayotukana wabunge wa upinzani kila wakati
 
Hiki ndio nini tena? msamaha wenye masharti?
Msamaha wa Mdee hauna masharti bali sisi tunamuonya Ndugai kuwa tusi lile lilitokana na tabia yake aliyoonyesha na kuwa naye atumie nafasi hii kujirudi asije tukanwa tena na Mbunge mwingine.
Sawa na baba anaye kasirishwa na mwanae kwa kumwita Mlevi mbwa, kama mtoto akiomba radhi na yeye akaendelea na ulevi itasaidia nini maana na mtoto mwingine naye atamtukana tena
 
Mh Halima James Mdee amemuomba radhi Mh Ndugai,spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mh Kigwangala, naibu waziri wa afya. Kitendo ulichokifanya ni cha kiungwana sana. Waswahili husema kiburi si maungwana. Umeamua kuacha kiburi na kutokuwasikiliza wafuasi wa chama chako humu mitandaoni waliokutaka uendelee kukomaa.
Umeahidi kutokurudia tena kutumia lugha zisizo za staha dhidi ya mbunge mwingine yeyote. Mungu akujaalie adhima yako itimie. Ni wewe ndiye unafahamu wakati mgumu uliokuwa nao wakati wa kuomba radhi na kabla ya kuomba radhi.
Pia umeahidi kuendelea kuwa mahili katika kutoa hoja kamambe za kuikosoa serikali na kuishari. Fanya hivyo huku ukidhibiti jazba ambazo hukufanya kuonge yasopaswa. Upo na Mungu atakusaidia.
 
Back
Top Bottom