Halima Mdee amsambaratisha Magufuli

Nimewahi kuishi Chato kwa muda miaka kadhaa, mwez uliopita tu ndipo nlipoondoka Chato, japo huu mkutano wa Halima Mdee hapa Chato nilikuwepo!! Iko hivi ktk jimbo hili la Chato kumng'oa Magufuli 2015 bado sijaona. Sio kwamba haiwezekani, inawezekana, lakini inatakiwa itumike nguvu na akili kubwa sana, Magufuli kafanya mambo makubwa sana sana Chato. Chato wanampenda kwa maendeleo aliyoyaleta kama vile barabara nzuri, umeme japo sio wa uhakika, huduma za afya na elimu amejitahidi, ujenzi wa ofis nzuri za halmashauri kwakeli Chato kaitoa mbali sana, huwez amin kwasasa barabara za lami zinajengwa mpaka vichochoroni kitu ambachohakifanyiki Kawe _DSM, ukiuliza hii barabara inaenda wapi utasikia "inaenda mwaroni/gatini, jineri n.k). Maghufuli ana vitu viwili vinavyoweza kumtoa madarakani ambavyo wananchi wamekua wakilalamika 1:Maghufuli anadharau wananchi masikin kwa kuwatolea lugha chafu, lugha chafu amekua akiitoa kwenye mikutano ya hadhara na wananchi. 2:Maghuli anakashfa ya kuwa chanzo kuua kiwanda cha PAMBA.
 
Kati ya hao walioshiriki mkutano ni wangapi wapo tayari kupiga kura? Bado na sisitiza kinachowafanya watu wajae kwenye mikutano hii ni ukosefu wa ajira. Watu wangekuwa na kazi usingewaona wakijaa kwenye viwanja hivi kusikiliza watu waliopo kwenye kazi zao.

Na ajabu ni kwamba aliesababisha wasiwe na kazi za kufanya na wasiwe na ajira ni chama kilichopo madarakani!!
 
Mwenyekiti wa BAWACHA Taifa Halima Mdee jana alitikisa Jimboni Chato kwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara kuwahi kuhutubiwa jimboni hapo miaka ya karibuni.

Awali Mdee alilakiwa na umati mkubwa wa watu wakiwa na msururu mrefu wa magari,pikipiki,baiskeli huku akina mama wakiwa kandokando ya barabara wakipunga matawi ya miti.

Ujumbe mkubwa wa Halima Mdee kwa wanaChato ni kuikataa Katiba Haramu ya CCM na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu.

Halima Mdee maarufu kama Tanzanian Iron Lady alipokea kadi 200 za watu walioamua kujitoa CCM na kujiunga Chadema.Huku mamia ya wananchi wengine ambao hawakuwa na chama wakijiunga pia Chadema.

Ikumbukwe jimbo la Chato linaongozwa na mbunge wa CCM John Pombe Magufuli ambaye ni waziri wa Ujenzi.

Ni simulizi hapa Chato kuanzia jana mpaka asubuhi hii kumzungumzia Halima Mdee na Chadema!
 
MAGUFULI hana jipya ni vuvuzela tu asahau kurudi bungeni 2015 imekula kwake janja yake ya nyani imestukiwa
 
Hadithi hadithi...hadithi njoo..uongo wa molemo njoo...Molemo idadi ya watu wanaoonekana kwenye picha pamoja na kuikuza kihivyo bado haijavunja rekodi ya mikutano ya dakta Magufuli...hizo kadi kumi na tano hazina tofauti na zile ambazo Kinana amekuwa akizipokea katika ziara zake, huko sio kumsambaratisha mtu..acha uzushi...subiria desema 14 chaguzi za serkali za mitaa ndio utoe tathmini yako kuwa Mdee amsambaratisha Magufuli

Hapa ni Halima Mdee.Je akija Rais Mtarajiwa Dr Slaa Itakuwaje ...
 
Siasa bwana.....ni mchezo mzuri na mbaya.....umati wa watu hauwezi kutoa majibu positive....wengine wpo tu kusikiliza na kujiongeza maarifa ya jinsi nchi inavyooenda lkn sio kwamba upo pamoja nao....
 
Kati ya hao walioshiriki mkutano ni wangapi wapo tayari kupiga kura? Bado na sisitiza kinachowafanya watu wajae kwenye mikutano hii ni ukosefu wa ajira. Watu wangekuwa na kazi usingewaona wakijaa kwenye viwanja hivi kusikiliza watu waliopo kwenye kazi zao.

poor mind set
 
kutumia akili ni juhadi na inataka busara. Kama umepiga msokoto hilo litakuwa gumu kwako . kumfananisha Magufuli na huyo msagaji
 
Mwenyekiti wa BAWACHA Taifa Halima Mdee jana alitikisa Jimboni Chato kwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara kuwahi kuhutubiwa jimboni hapo miaka ya karibuni.

Awali Mdee alilakiwa na umati mkubwa wa watu wakiwa na msururu mrefu wa magari,pikipiki,baiskeli huku akina mama wakiwa kandokando ya barabara wakipunga matawi ya miti.

Ujumbe mkubwa wa Halima Mdee kwa wanaChato ni kuikataa Katiba Haramu ya CCM na kushiriki kikamilifu katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu.

Halima Mdee maarufu kama Tanzanian Iron Lady alipokea kadi 200 za watu walioamua kujitoa CCM na kujiunga Chadema.Huku mamia ya wananchi wengine ambao hawakuwa na chama wakijiunga pia Chadema.

Ikumbukwe jimbo la Chato linaongozwa na mbunge wa CCM John Pombe Magufuli ambaye ni waziri wa Ujenzi.

Ni simulizi hapa Chato kuanzia jana mpaka asubuhi hii kumzungumzia Halima Mdee na Chadema!

1658198_658862364212406_8498540439566593170_o.jpg

10612779_658862337545742_528341973315421299_n.jpg

10407380_658862304212412_6823844216364614988_n.jpg

10669105_658862190879090_1474681969313438198_o.jpg

JF ni sehemu ya heshima, nilikuwepo kipindi mkutano unafanyika, aliyerudisha kadi ni mtu mmoja tu mke wa Huru Selemani na Mdee alitaja Magufuli wakaitikia "Juu" .Propaganda za uongo huwa sizipendi ni bora kukaa kimya.

Pia picha katika gazeti "..mkutano wa hadhara uliyofanyika juzi katika viwanja vya stendi ya zamani..." hii stendi tupo hapa kila siku hakuna mandhari kama haya katika stedni hii ya zamani, propaganda tuzifanye ila ziwe za ukweli tusilazimishe kudanganya jamani - very bad!

Huyu (Magufuli) ni kati ya viongozi wachache walioko huko magambani ninaowakubali wanavyojitoa kusaidia taifa na watu masikini. niliwahi kupata clip zake katika youtube:






 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom