Mmawia
JF-Expert Member
- Aug 20, 2013
- 121,947
- 95,237
Ndugu yangu mimi nipo hapa bukoba na nina miaka zaidi ya kumi na tatu,wahaya wanachukizwa sana na dharau kwao wawe ni masikini au tajiri ukiwa na madharau hauna future ktk uongozi.Mfano ni aliyekuwa mbunge wa Nkenge Kamara alikosea kuwajibu ktk kero ya ngedere na nyani kuharibu mazao ya wananchi akawajibu hivi----KAMA MNAONA HAO WANYAMA WANAWASUMBUA BASI MUWAFANYE KITOWEO----Wahaya walikasilika vibaya na wakampiga chini.Nimewahi kuishi Chato kwa muda miaka kadhaa, mwez uliopita tu ndipo nlipoondoka Chato, japo huu mkutano wa Halima Mdee hapa Chato nilikuwepo!! Iko hivi ktk jimbo hili la Chato kumng'oa Magufuli 2015 bado sijaona. Sio kwamba haiwezekani, inawezekana, lakini inatakiwa itumike nguvu na akili kubwa sana, Magufuli kafanya mambo makubwa sana sana Chato. Chato wanampenda kwa maendeleo aliyoyaleta kama vile barabara nzuri, umeme japo sio wa uhakika, huduma za afya na elimu amejitahidi, ujenzi wa ofis nzuri za halmashauri kwakeli Chato kaitoa mbali sana, huwez amin kwasasa barabara za lami zinajengwa mpaka vichochoroni kitu ambachohakifanyiki Kawe _DSM, ukiuliza hii barabara inaenda wapi utasikia "inaenda mwaroni/gatini, jineri n.k). Maghufuli ana vitu viwili vinavyoweza kumtoa madarakani ambavyo wananchi wamekua wakilalamika 1:Maghufuli anadharau wananchi masikin kwa kuwatolea lugha chafu, lugha chafu amekua akiitoa kwenye mikutano ya hadhara na wananchi. 2:Maghuli anakashfa ya kuwa chanzo kuua kiwanda cha PAMBA.