Halima Mdee akwaa kisiki mahakamani

Halima Mdee akwaa kisiki mahakamani

Mwanajamii

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2008
Posts
7,063
Reaction score
71
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetupilia mbali pingamizi lililowekwa na Mbunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Halima Mdee, lililokuwa likitaka hati ya madai katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu mwaka 2010 iliyofunguliwa na aliyekuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya (NCCR-Mageuzi), James Mbatia, ifanyiwe marekebisho kwa maelezo kuwa haina msingi wa kisheria.

Uamuzi huo ulitolewa jana na Jaji John Utamwa ambaye baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili alifikia uamuzi wa kukubaliana na hoja za wakili wa mlalamikaji, Mohamedi Tibanyendela, aliyetaka pingamizi hilo litupwe na mahakama.

Jaji Utamwa alisema kwa mujibu wa hati ya madai, mlalamikaji ameeleza malalamiko yake yote kwa mapana dhidi ya mdaiwa na maelezo hayo yanajitosheleza kumfanya mdaiwa kujibu tuhuma hizo zilizoelekezwa kwake.

"Hivyo mahakama hii haikubaliani na pingamizi la mdaiwa anayetetewa na Wakili Edson Mbogoro anayetaka hati ya madai ifanyiwe marekebisho kwa vile hawezi kujibu baadhi ya tuhuma alizotuhumiwa nazo kwasababu zinamkera, kumtia kichefuchefu…..

Kwa hiyo mahakama hii leo inasema tuhuma hizo hazikeri wala kutia kichefuchefu hivyo ina muamuru mdaiwa kuzijibu na inatupilia mbali pingamizi la mdaiwa," alisema Jaji Utamwa.

Jaji Utamwa aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba mosi mwaka huu, ambapo kesi hiyo itakuja kwa ajili ya kutajwa na kuangalia muda wa jinsi ya kuendelea nayo, kwani Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 2010 inataka kesi za uchaguzi zimalizike ndani ya mwaka mmoja
tangu zilipofunguliwa. Kesi hiyo ilifunguliwa Novemba mwaka 2010.

Uamuzi huo unatokana na pingamizi lililowasilishwa na wakili wa Mdee, Mbogoro la kuiomba mahakama hiyo imwamuru mlalamikaji aifanyie marekebisho hati yake ya madai na kuyaondoa baadhi ya madai ambayo Novemba 25 mwaka 2010 Mbatia alifungua kesi ya kupinga matokeo ya ubunge wa jimbo hilo ambayo yalimtangaza Halima Mdee (CHADEMA) kuwa mshindi.

Mbatia anadai kuwa katika mikutano ya kampeni, Mdee alimwita yeye kuwa ni fataki anayefanya mapenzi na watoto wa shule, kibaraka wa CCM na kila wiki analipwa sh milioni 80 na chama hicho, hivyo kuwataka wapiga kura wa Jimbo la Kawe wasimchague Mbatia.

SOURCE. TANZANIA DAIMA

[TD="bgcolor: #ffffff"]
[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #ffffff"]
amka2.gif
[/TD]



 
hivi Mbatia alijua lini hizi tuhuma za kashfa zimemwathiri katika uchaguzi? alipaswa kupeleka malalamiko yake kwa nec kabla ya uchaguzi na wala siyo baada ya kushindwa.......................................halafu katika kampeni hizo ni tuhuma.................hata kama kweli zilisemwa........................zilimwathiri vipi asichaguliwe.....................kwa nini hakuzijibu?
 
sheria bwana, Hapa naona Mdee ana kesi ya kujibu kwa kueleza ni kivipi anatembea na watoto wa shule, anahogwa hizo pesa

Kusema tu malalamiko mengine yanamletea kichefuchefu ni hoja nyepesi kwenye maswali magumu na sababu ya kupoteza muda-
 
kwani kupanda nao gari sio kutembea nao??? i would vote for kutembea as kutembea na sio kufanya mapenzi.... na milioni themanini ndio issue
 
hivi Mbatia alijua lini hizi tuhuma za kashfa zimemwathiri katika uchaguzi? alipaswa kupeleka malalamiko yake kwa nec kabla ya uchaguzi na wala siyo baada ya kushindwa.......................................halafu katika kampeni hizo ni tuhuma.................hata kama kweli zilisemwa........................zilimwathiri vipi asichaguliwe.....................kwa nini hakuzijibu?

I think before we shift the problem, is also well to wonder that " Wasn't Halima( The Respondent) aware that these kind of accusations/statements would affect her in the future?
About how did those statements affect the complainant and if they had any impact on his failure, thats just a game of chance, and we have a lesson to learn out of that.
 
Kuna hatari Halima Mdee, mbunge wa jimbo langu kupoteza kiti chake..

Naona siku hizi kaamua kuwa mwanamitindo
 
mbatia si aliitwaga shoga na mrema huyu...
 
[TABLE="class: MsoNormalTable, width: 598"]
[TR]
[TD]
[/FONT said:

Mbatia anadai kuwa katika mikutano ya kampeni, Mdee alimwita yeye kuwa ni fataki anayefanya mapenzi na watoto wa shule, kibaraka wa CCM na kila wiki analipwa sh milioni 80 na chama hicho, hivyo kuwataka wapiga kura wa Jimbo la Kawe wasimchague Mbatia.

[/FONT said:
[/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]



kwani kupanda nao gari sio kutembea nao??? i would vote for kutembea as kutembea na sio kufanya mapenzi.... na milioni themanini ndio issue

Are you suggesting or refering? Which one among the above highlighted statements is in the case file?
 
Kwani wagombea walikuwa wa CHADEMA na MBATIA?CCM,CUF hawakuwa na wagombea?je alitajwa kwa jina?kwanini alikaa kimya mpaka aliposhindwa?
 
Kwani wagombea walikuwa wa CHADEMA na MBATIA?CCM,CUF hawakuwa na wagombea?je alitajwa kwa jina?kwanini alikaa kimya mpaka aliposhindwa?

Pamoja na mambo ya hapa na pale nadhani kikubwa kinachomsumbua huyu James (Yakobo) ni kushindwa na mwanamke tu!
 
kama wanataka kuona game ya uchaguzi jinsi tulivyo ichukia ccm halima mdee ashindwe hyo kesi alafu waitishe uchaguzi ndipo ccm watakapo ona game inavyo chezwa
 
CCM wanataka kujiaibisha kwa kutaka re-match na cdm sasa hivi. Halafu kwa kutojua wanagusa majimbo ambayo wanajua wazi hawatapata hata kura alufu. Kama unaakili huwezi kutaka ReKmatch na Mdee au Lema. Hivi wanajua kuwa wanachi bado hawajasahau uchaguzi wa mwaka jana na wengi wanawashwa wanatamani itokee tena nafasi ya kuchagua maana watamalizia hasira zao kwa magamba. Hawajajifunza pale Igunga maana cdm haikuwa hata na jina pale lakini ulimi uliwachomoka.

CCM wangekuwa na akili wangeachana kabisa na mambo ya kura sasa hivi maana watu wanahasira nao wanaweza wakapata hata zero. Pia wanashindwa kuelewa kuwa kwa kufanya hivyo wanawapa cdm muda wakuongea na wananchi tena.

Acha wajaribu maana mchwa huwa unajaribu hata kwenye jiwe.


?
 
Mbatia kushindwa na Mdee, inampa shida. Magamba wanataka tumia turufu hiyo kupunguzi idadi ya wa bunge wa CDM.
Ole wenu magamba hizo kura zenu chache mlizo chakachua 2010 zita ishia ndani.
 
Back
Top Bottom