Haya we muwashaji mwenye pepo la uongo mwenye uzima wa kutegemea watu wakusukume kutumia vionjo vyako soma hiyo mwananchi. Mwenzako nilifuatilia kwa siku kadhaa kila hatua.
Katika makabidhiano ya ripoti yaliyoshuhudiwa na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na wajumbe wengine watatu wa PAC, Ndugai alisema; Naielekeza kamati yako ifanye uchambuzi na kutoa maoni na mapendekezo katika kila hadidu rejea.
Katika kufanya uchambuzi kamati ijikite zaidi katika kufanya uchambuzi wa CAG na Takukuru.
Ndugai alisema katika uchunguzi wake, CAG aliwahoji wote waliohusika na jambo hilo na kisha kuwasilisha taarifa yake kwa Takukuru kwa hatua zaidi.
Kamati ifanye kazi kwa kuzingatia kanuni ya tatu na nne kwa kuzingatia nyongeza ya saba ya kanuni za Kudumu za Bunge za mwaka 2014 na kifungu cha tisa kifungu kidogo cha kwanza na cha 31 vya Sheria ya Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge, Sura ya 299, alisema.
Alisema ni matumaini yake kwamba baada ya kumaliza kazi ya kutoa maoni na mapendekezo, taarifa iwasilishwe kwake (Ndugai) ili ajiridhishe kabla ya kuwasilisha bungeni.
Nimemwelekeza Katibu wa Bunge, asimamie na awape ushirikiano unaotakiwa ili kazi yenu iweze kuwa ya ufanisi na yenye kiwango, alisema.
Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah aliikabidhi PAC watendaji wanne ambao wataisaidia kufanya kazi hiyo.
Akizungumza baada ya makabidhiano hayo, Zitto alisema kamati yake itazingatia maagizo ya Ndugai kutokana na masuala ya kimahakama yaliyomo ndani ya ripoti hiyo.
Kwa hiyo PAC haitakuwa na utaratibu wa kawaida ambao tunafanya tunapowaita watu wakati wa kuhoji mahesabu yao. Nimeshtuka kidogo maana Bunge limeipa nguvu sana PAC katika jambo hili kwa kuwaelekeza kutumia sheria namba tatu. Sisi tutaitumia nguvu hiyo kutenda haki katika jambo hili zima, haki kwa Watanzania na watu ambao wametajwa kuhusika katika jambo zima.
Zitto alisema ripoti hiyo inaonyesha jinsi taasisi za kiuwajibikaji zinavyofanya kazi, mambo ambayo huwezi kuyaona katika nchi nyingine.