Hali yazidi kuwa tete escrow, hapatoshi Dodoma

Hali yazidi kuwa tete escrow, hapatoshi Dodoma

‘’Ni kweli kila mtu atavuna alichopanda, kama wanataka kutugeuza wabunge wote ni ‘Rubber stamp’ tuhalalishe hukumu inayotokana na hasira zao za kunyimwa mgao, basi wamegonga mwamba’’.
Alisema mmoja wa wabunge hao anayetokea chama kimoja cha upinzani akijibu kauli ya Makamu Mwenyekiti wa PAC, Deo Filikunjombe aliyenukuliwa na gazeti moja hivi karibuni.


Hivi karibuni Filikunjombe, alisema katika gazeti hilo, kwamba kila mtu atavuna alichopanda katika sakata hilo, baada ya kupokea ripoti ya CAG kutoka kwa Naibu Spika, Job Ndugai.


Ripoti nyeupe, Zitto kapiga mpunga, anashindwa namna ya kuchomoka ndio maana kaanza kusema watahoji wahusika nyuma ya pazia sababu anajua hakuna mtuhumiwa kama alivyokuwa akijitamba.

Ifike wakati mtu akizusha jambo ambalo baadae ikabainika si kweli ashtakiwe na alipe gharama aliyoisababisha serikali kutumia fedha nyingi kufanya uchunguzi.nadhani hii itsaidia ana kupunguza uzushi
 
Tuesday, 18 November 2014

RIPOTI IPTL KULIGAWA BUNGE :- KAMATI YA ZITTO KABWE YATUHUMIWA KWA RUSHWA. WAKILI MSANDO NA MALIMA WALITUMIWA NA KAMATI KUOMBA RUSHWA.




wakili Albert Msando kulia anayedaiwa kutumika kuchukua RUSHWA IPTL kwa niaba ya kamati ya PAC akiwa Zitto Kabwe ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ya PAC




IKIWA ni siku chache tu baada ya kutolewa kwa taarifa za kukabidhiwa kwa ripoti ya ukaguzi wa akaunti ya ESCROW, uliofanywa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG), kwa spika na kamati ya mahesabu ya serikali PAC, mengi yameibuka.


Hali hiyo inatokana na kuwepo kwa mgawanyiko wa wabunge kuhusu na jambo hilo huku kila upande ukiwa na mtazamo wake tofauti juu ya jambo hilo, ambalo wabunge wengi wanaamini linapikwa na halizungumzwi ukweli.


Taarifa kutoka Dodoma zinasema kwamba wabunge wengi wameshitushwa na kuvuja kwa taarifa kuwa kamati ya PAC imelivalia njuga suala hilo, baada ya kushindwana kuafikiana mgao wa malipo kutoka kwa wamiliki wa kampuni ya IPTL/PAP ili kulizuia kulimaliza katika Kamati lisifike bungeni mapema mwaka huu.


Taarifa hizo zinasema kamati ya PAC iliwatumia mwanasheria aliyefahamika kwa jina la Albert Msando ambaye ni msaidizi wa kisheria wa Zitto Kabwe na Beatus Malima kujadili juu ya malipo watakayolipwa PAC ili kuidhibiti ripoti hiyo na namna ambavyo PAC ingetoa hukumu ya awali.




Deo Filikunjombe ambaye ni makamu mwenyekiti wa kamati ya PAC.






Vithibitisho ambavyo baadhi ya waandishi wameonyeshwa na baadhi ya wabunge hao, vinaonyesha mijadala iliyokuwa ikiendelea bungeni kuwa mingi ni ya kupikwa na ya kimkakati inayotokana na hasira za kutokupatiwa malipo waliyoomba PAP na hivyo kulitaka bunge lipigie mhuri kitu ambacho ni mgogoro unaotawali na maslahi binafsi.


Haijafahamika mara moja kwamba ni kiasi gani kimeombwa na kamati ya PAC kwa PAP ili walifunge jambo hilo, mlakini baadhi ya wabunge hao wamesema wapo tayari kuweka wazi kila kitu ili kila mtu avune alichopanda.


‘’Ni kweli kila mtu atavuna alichopanda, kama wanataka kutugeuza wabunge wote ni ‘Rubber stamp’ tuhalalishe hukumu inayotokana na hasira zao za kunyimwa mgao, basi wamegonga mwamba’’.
Alisema mmoja wa wabunge hao anayetokea chama kimoja cha upinzani akijibu kauli ya Makamu Mwenyekiti wa PAC, Deo Filikunjombe aliyenukuliwa na gazeti moja hivi karibuni.


Hivi karibuni Filikunjombe, alisema katika gazeti hilo, kwamba kila mtu atavuna alichopanda katika sakata hilo, baada ya kupokea ripoti ya CAG kutoka kwa Naibu Spika, Job Ndugai.




Baadhi ya wanahabari walipotembelea mitambo ya IPTL inayolalamikiwa hivi karibuni




Akizungumza kwa kujiamini, mbunge mwingine ambaye pia ameomba ahifadhiwe jina lake kwa sasa anasema ’’Hata Kamati yenyewe ya PAC imegawanyika vipande vipande, wakubwa wao wamevuta mzigo wa kutosha na wenzao wanawaburuza, halafu kazi nzima ya kamati inapelekeshwa kutoa sifa kwa watu wawili tu ambao ni Zitto na Filikunjombe, huu ni upuuzi’’.


Mbunge huyo alisema sisi sote ni wanasiasa, unafikiri nani atakuwa tayari kufanya kazi, halafu sifa ziwaendee watu wawili tu kwamba wao ndio wanaakili sana na wana uchungu sana na nchi.
‘’Hebu jiulize kamati ina wajumbe zaidi ya 20 lakini kila kitu zitto na deo wanajiweka kimbelembele, sasa na safari hii wanapoumbuliwa kwa madili yao ya rushwa wakae kimbelembele hivyo hivyo’’. Alisema mbunge huyo.


Hata hivyo, taarifa kutoka kwenye ripoti iliyovuja ya CAG haionyeshi kwamba kuna tatizo kwenye ukaguzi walioufanya wa akaunti ya ESCROW, badala yake umeibua madai mapya ambayo sio msingi wa uchunguzi walioagizwa kufanya.


Itakakumbukwa kwamba akaunti ya ESCROW ilifunguliwa rasmi Julai, 5 2006, wakati ripoti ya CAG inaonyesha mapungufu ya kuanzia Januar 2002 mpaka Desemba 2006 huku ripoti yenyewe ilipaswa kujikita kati ya 2006 mpaka 2013 ilipofungwa.


‘’Hatupaswi kuwaadhibu watu kwa sababu tu tunawachukia, au kwa sababu tunachuki na tofauti nao binafsi ama za kisiasa, sisi kama bunge ni lazima tufanye kazi zetu kwa kudhibiti hisia zetu, wanachokifanya kina Zitto, David Kafulila na Deo, ni chuki binafsi na si uzalendo kama wanavyotaka iwe, kama ni wazalendo wasingefanya kama haya wanayofanya’’. alisema mbunge huyo.


Alisema mbunge huyo, wabunge hao baada ya kuona ripoti ya CAG haiwatii hatiani serikali na wanaowachukia wao, wanalazimisha kusema kuwa kuna hasara ya bilioni 321. Waache kuwafanya wabunge watoto wadogo kwa kuwa kila kitu tunakijua.






Wakati hayo yakiendelea, jana asubuhi Mbunge wa Mtera-CCM, Livingstone Lusinde aliiomba mwongozo kwa Naibu Spika, Job Ndugai kuhusiana na kubana kwa ratiba katika suala la akaunti ya ESCROW huku jambo hilo likiwa na hamasa kubwa kwa watanzania.
“Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Kamati ya Uongozi ya Bunge iongeze siku au muda katika kujadili suala hili, kwa kuwa ni jambo kubwa linalohitaji kujadiliwa zaidi, tuna mengi tunayoyajua, makando kando ya wanaotuhumiwa na wanaotuhumu pia, kwa kuwa waswahili wana msemo mmoja ukimuona anayelia sana ujue ndio mchawi mwenyewe,’’alisema.


Alisema wabunge wanaolia sana kuhusiana na jambo hilo, wenyewe wana makando makando katika suala hilo kutokana na kuhusika kwa namna moja au nyingine katika sakata hilo, ambalo anaamini kujadiliwa kwa muda mrefu zaidi ndio jambo litakaloweka haki kwa kila mtu.
Hivyo, aliiomba Bunge iongeze siku zaidi kujaidli suala hilo, ambapo Naibu Spika Ndugai alisema atawasiliana na Kamati ya Uongozi ya bunge kuhusiana na mwongozo huo wa Lusinde ili ufanyiwe kazi kwa kuwa jambo hilo lina umuhimu mkubwa kwa taifa.







attachment.php

attachment.php
Mnawalia jamaa hela zao bureee swala hili lilipofika hatudanganyiki !!!!! Tumbili wetu kasha limaliza
 
habari yenyewe imeandikwa na lile gazeti la kufungia mandazi
ni udaku na naaminini uzushi wa kawaida unless proved otherwise.
 
Hiyo habari ni udaku maana unasikia mara mbunge mmoja, mara jina limehifadhiwa.

"IPTL-Bring Back Our Money" Inaendelea....!

Mkuu! Ben achana nao hao vilaza mwisho wao humu ni kesho nitakapounguruma na vyombo vya habari kutokea kanda ya ziwa. Kuwaweka hadharani pamoja na dalali wao mkuu. Ambaye njaa yake imekimbilia kichwani tena kwenye ubongo wake, hawa vidagaa wanalipwa 60,000 kwa siku na wamekabidhiwa vitendea kazi na Iptl kupitia kwa huyo dalali wao. Ambaye amehamishwa mpaka nyumbani kwake na kupangiwa hotel na hao mafisadi. Stay tuned tomorrow wadau
 
Poetry timeout.
An Africa Thunderstorm
From the west
Clouds come hurrying with the wind
Turning sharply
Here and there
Like a plague of locusts
Whirling,
Tossing up things on its tail
Like a madman chasing nothing.
Pregnant clouds
Ride stately on its back,
Gathering to perch on hills
Like sinister dark wings;
The wind whistles by
And trees bend to let it pass.
In the village
Screams of delighted children,
Toss and turn
In the din of the whirling wind,
Women,
Babies clinging on their backs
Dart about
In and out
Madly;
The wind whistles by
Whilst trees bend to let it pass.
Clothes wave like tattered flags
Flying off
To expose dangling breasts
As jagged blinding flashes
Rumble, tremble and crack
Amidst the smell of fired smoke
And the pelting march of the storm.
 
Mkuu! Ben achana nao hao vilaza mwisho wao humu ni kesho nitakapounguruma na vyombo vya habari kutokea kanda ya ziwa. Kuwaweka hadharani pamoja na dalali wao mkuu. Ambaye njaa yake imekimbilia kichwani tena kwenye ubongo wake, hawa vidagaa wanalipwa 60,000 kwa siku na wamekabidhiwa vitendea kazi na Iptl kupitia kwa huyo dalali wao. Ambaye amehamishwa mpaka nyumbani kwake na kupangiwa hotel na hao mafisadi. Stay tuned tomorrow wadau

Wewe siyo bure utakuwa umetumwa na Kafulila! Kubadiri upepo.
 
habari yenyewe imeandikwa na lile gazeti la kufungia mandazi
ni udaku na naaminini uzushi wa kawaida unless proved otherwise.

Ingeandika na Tanzania Daima isingekuwa udaku? ujumbe umekufikia huo. teh teh teh teh! Ripoti nyeupe.
 
Unahangaika bure; hizo ni diversion tactics za wanamtandao wa escrow; wakisaidiana na waandishi wa habari makanjanja; zote hizo ni haraikati za kujinasua; subiri kamati imalize mahojiano yake na hao watuhumiwa na mwenye ushahidi uaupeleke kwa spika au DPP na takukuru; period; kwa hili hatudanganyiki!!!!!

This time lazima kieleweke na watanzania wajue kama TUMBILI ni Werema au ni Kafulila!!

Ombi Maalumu kwa Watanzania wenye Vipaji vya Uchoraji na Ubunifu wa Mavazi:
Kwa kuwa siku si nyingi mambo kuhusu ESCROW yanakwenda kuwekwa hadharani, na jinsi upepo unavyovuma inaonesha Tumbili amekalia watu kooni. Nawaomba sana ikitokea Tumbili ameshinda kwa niaba yetu Watanzania wachukia Ufisadi tumuenzi kwa kuvaa nguo zenye Nembo/Picha ya Tumbili shujaa...
Kama ni T-shirt au Vitenge tuko tayari kununua, wabunifu wa mavazi kazi kwenu.

Mnaliojane hili? Nawasilisha.
 
Mnawalia jamaa hela zao bureee swala hili lilipofika hatudanganyiki !!!!! Tumbili wetu kasha limaliza

Huwezi ku-comment pasipo ku-quote? Acha upuuzi wengine tunatumia cm za mkononi!
 
Hiyo habari ni udaku maana unasikia mara mbunge mmoja, mara jina limehifadhiwa.

"IPTL-Bring Back Our Money" Inaendelea....!

Umepanic mkuu! Mtavuna mlichopanda kwa njaa zenu. Tumeona habari nyingi humu hususa ni zile za Tanzania Daima zikiwa zinanukuu kutoka chanzo ambacho hakitaki kutajwa jina, hii ni sahihi na Magazeti yote yanaandika hivyo, habari hakukupendeza. Ila ujumbe umekufikia wewe na team yako.
 
Hiyo habari ni udaku maana unasikia mara mbunge mmoja, mara jina limehifadhiwa.

"IPTL-Bring Back Our Money" Inaendelea....!

Kifupi wanatuvuruga tu na kwenye huo mvurugano ndio watapata pa 'kuchomokea'....Mara sio hela za serikali...mara sakata lipo na watu fulani (wasiotajwa milele) wanahusika...mara waache kuwafanya wabunge watoto wadogo kwa kuwa kila kitu tunakijua (kumbe wanajua wanakaa kimya..na ni rubber stamp kweli haswa!)
Hata sioni jipya lao....


 
Unahangaika bure; hizo ni diversion tactics za wanamtandao wa escrow; wakisaidiana na waandishi wa habari makanjanja; zote hizo ni haraikati za kujinasua; subiri kamati imalize mahojiano yake na hao watuhumiwa na mwenye ushahidi uaupeleke kwa spika au DPP na takukuru; period; kwa hili hatudanganyiki!!!!!

This time lazima kieleweke na watanzania wajue kama TUMBILI ni Werema au ni Kafulila!!

Jinsi muda unavyozidi kwenda Simba (WEREMA) anazidi kuwa mdogo kuelekea kuwa TUMBILI na Tumbili(KAFULILA) anaendelea kukua kueleka kuwa SIMBA. Life is sooooooo sweeeet!!!
 
ningeiamini kama ingekuwa imeandikwa na Kubenea
au gazeti la citizen
lengo la hawa mafisadi kumpaka matope Zitto ni kwa vile hawataki ukweli ujulikane
hapa tunataka katibu mkuu na Pinda wote wangolewe na wawajibishwe
fedha zirudi
Ingeandika na Tanzania Daima isingekuwa udaku? ujumbe umekufikia huo. teh teh teh teh! Ripoti nyeupe.
 
ningeiamini kama ingekuwa imeandikwa na Kubenea
au gazeti la citizen
lengo la hawa mafisadi kumpaka matope Zitto ni kwa vile hawataki ukweli ujulikane
hapa tunataka katibu mkuu na Pinda wote wangolewe na wawajibishwe
fedha zirudi
mpigie simu kubenea andike yeye!
ila kuna watu vilaza humu jf sasa kubenea ndo baba yako au? mpaka umuamini kiasi hicho?
wakati yeye mwenye ni mpigaji wa maana tu
 
Back
Top Bottom