DOKEZO Hali ya Kawe ni mbaya, Serikali ichukue hatua dhidi ya Mwamposa na waumini wake

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Heparin

Senior Member
Sep 24, 2021
127
420
Nawasalimu wote kwa jina la Upendo. Amani, baraka na neema za Mwenyezi Mungu ziwe pamoja nanyi.

Kwa wakristu, hongereni kwa kuingia nusu ya pili ya mfungo wenu. Pia, nawatakia ndugu zangu waislam mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, mwenyezi Mungu awakirimie Neema na azipokee sala na funga zenu.

Pasipo kuathiri imani na ibada yao kwa Mungu, nataka nitoe maoni yangu kuhusu uzembe uliopo Tanganyika Packers, kwa waumini wanaosali kwa Mtume Mwamposa.

Binafsi, sina shida yoyote na kusali kwao. Isipokuwa, kumekuwepo na tabia ya watu hawa kulala chini, kwenye uwanja wa wazi usiku kucha wakisubiri huduma hii.

Jumatatu moja Mwaka jana mwezi wa 7 wakati naanza kazi kwenye taasisi moja iliyo karibu na maeneo haya, nilishangaa kuona kusanyiko kubwa la watu waliolala chini ambao kwa hesabu ya haraka hawakuwa pungufu ya 500.

Katika kundi hilo, idadi kubwa ya watu walikuwepo ni wazee, wajawazito na wanawake wenye watoto wachanga sana. Hali hii haikuishia siku hiyo, imekuwepo hadi sasa.

968CD68F-2ED0-4960-A93E-2738D973A6A0.jpeg

Sehemu ndogo ya makundi ya watu waliolala hapo usiku wa kuamkia leo Machi 23, 2023
Mtu yeyote mwenye akili timamu hahitaji elimu ya sayari ya 5 kuona kuwa mazingira haya ni hatari kwa afya ya wahusika.

Kwa kuwa mimi ni mtu mwenye elimu ya fani fulani ya afya, inayohusika na kushughulikia wagonjwa moja kwa moja, huwa nawaza sana kila ninapoona watu hawa asubuhi. Fikiria hali ya sasa ya mvua, kisha mtazame mzee, au mwanamke mjamzito, mama mwenye mtoto mchanga au mgonjwa wa kisukari, presha au kifafa anayelala hapo usiku kucha kwa siku kadhaa akisubiria huduma.

Kibaya zaidi, sehemu za kujisaidia na kupata huduma muhimu za kibinadamu hazitoshi. Mathalani, ukipita hapo asubuhi utakuta watu wanapiga mswaki hadharani na kutema uchafu barabarani, au hata sehemu ileile ambayo huitumia kulala wakati wa usiku.

Baridi kali na vumbi ni chanzo cha magonjwa mengi hasa kwa watoto na wazee. Badala ya kupata huduma za kiroho, watu hawa wanaweza kuondoka hapo wakiwa na mzigo wa magonjwa mengine makubwa zaidi.

Naomba Serikali itazame suala hili kwa umakini. Kama imeshindwa kabisa kuweka utaratibu mzuri wa kumbana Mwamposa kwa kuwa yeye ndiye kiongozi, basi miundombinu ya eneo hili iboreshwe.

Kuacha hali hii iendelee ikiwa hivi itasababisha maafa makubwa. Uponyaji wa kiroho unapaswa kwenda pamoja na uponyaji wa kimwili.

Naomba kutoa hoja!
 
Ila Mwamposa anazingua. Kuliko kujenga hotel Mbeya kwanini asingeanza kujenga hostels kwa ajili ya waumini wake kwanza.

Naamini angefanya hivyo angevuna pesa zaidi za kuweza kujenga mahoteli mengi zaidi.

Inabidi ajifunze kuthamini malighafi yake (waumini) ili kuendelea kuvuna zaidi (sadaka).

 
Hiyo ndo inasemwa kuwa ".......kwa kukosa maarifa".

Hana sehemu rasmi ya kufanyia hiyo biashara yake ya kukusanya pesa za wenye matatizo. Anajijengea Hotel, kwamba anajiandaa kidunia zaidi na si kiimani sio?

Huyo aliyemruhusu aendelee kutumia TP pale naye achunguzwe.
 
Ila Mwamposa anazingua. Kuliko kujenga hotel mbeya kwanini asingeanza kujenga hostels kwa ajili ya waumini wake kwanza.

Naamini angefanya hivyo angevuna pesa zaidi za kuweza kujenga mahoteli mengi zaidi.

Inabidi ajifunze kuthamini malighafi yake (waumini) ili kuendelea kuvuna zaidi (sadaka).
Hela za kujengea hoteli amezipata kwa hao wanaokosa mahali pa kulala.

Mungu atupe hekima
 
Kutokana na ujinga walio nao wa Tanzania kama tusipotumia fursa kama walivyotumia kina Babu wa loliondo, Askuf kakobe, Mfalme Zumaridi, Geo devie, na Mwamposa
Nina wasiwasi wajukuu zetu wakikuta tulikufa masikini wanaweza kuja kutuchapa viboko kaburini
Wajukuu zetu watarithi ujinga tunaowarithisha wenetu.

Nchi ipo pabaya hii
 
Kutokana na ujinga walio nao wa Tanzania kama tusipotumia fursa kama walivyotumia kina Babu wa loliondo, Askuf kakobe, Mfalme Zumaridi, Geo devie, na Mwamposa
Nina wasiwasi wajukuu zetu wakikuta tulikufa masikini wanaweza kuja kutuchapa viboko kaburini
Actually wajukuu zetu wanakua imara kwasababu wazazi wao watateseka sana

Jamii yetu ya sasa itazaa wajukuu wenye hasira sana na sisi

Watatuchukia na kukojolea makaburi yetu
 
Nawasalimu wote kwa jina la Upendo, amani, baraka na neema za Mwenyezi Mungu ziwe pamoja nanyi.

Kwa wakristu, hongereni kwa kuingia nusu ya pili ya mfungo wenu. Pia, nawatakia ndugu zangu waislam mfungo mwema
kitanda usichokilalia huwezijua kunguni wake. Kifupi ni kuwa watu wana shida nyingi sana na zimekosa utatuzi kabisa.

Mtu yupo tayari kufanya chochote ili mradi apate nafuu. Kuna siku nilikuwa mwanza , mkutano wa Mwamposa alitarajiwa kesho yake saa 10 jioni, lakini watu ( wateja wa maji na mafuta) walishaanza kujikusanya na kulala eneo la tukio-viwanja vya furahisha.

Na mkutano ukiisha huyu jamaa anakuwa wa kwanza kuondoka eneo la tukio tena kwa escort na kuwaacha wateja wake wakilala hapo uwanjani.

It is not fair.
Akumbuke Yesu alilisha wafuasi wake.
Yeye anashindwa vipi kuwapa huduma bora waumini (wateja)wake.
 
Back
Top Bottom