Wana JF
Dalili zinaonyesha kuwa upo mkakati mkubwa umesukwa kuivuruga CHADEMA kwa mbinu mbalimbali. Kwa mfano ukiangalia kwa sasa mara baada ya CCM kumtosa EL na RA vyombo vya habari vya ITV na Redio one vimegeuza mwelekeo na sasa vinapenyeza kiaina habari mbaya zote zinaelekezwa kwa CHADEMA ili kuifanya CDM isikubalike na wananchi.
Upo mkakati unafanyika ili kuwavunja nguvu wabunge wa CHADEMA wakose kujiamini bungeni unaofanywa na Spika wa bunge na baadhi ya vyombo vya habari ikiwemo Radio one na ITV ili ionekene kuwa wabunge wa CHADEMA hawajui kanuni za bunge mfano Spika Makinda ameripotiwa kuwa Bunge la bajeti la mwaka huu itabidi lianze kwa wabunge kufundishwa kanuni kwani eti wabunge wengi hasa wa upinzani ni wapya hawajui kanuni wanaropoka hovyo bungeni hii si kweli hata kidogo wote tunafuatilia bunge na tuna macho ni ujinga kutufanya hatujui nani hafuati kanuni. Mtaona pia yale yaliozungumzwa wiki iliyopita na Katibu wa Bunge ilikuwa moja ya mbinu za mkakati huo unaoratibiwa kistadi isivyorahisi kugundulika na mwanachi wa kawaida.
Mkakakati mwingine ni kuwatumia wabunge mamluki waliondani ya CHADEMA kuanzisha vurugu kwa kutafuta hoja za kuvuruga chama.
Nilitoa angalizo mapema kuwa CCM sasa watatumia sana wale waandishi mahiri ambao wanaaminiwa na wananchi kuivuruga CHADEMA.
CHADEMA isimame imara kwani ikikubali kuvurugwa kama vyama vingine vilivyosambaratishwa na CCM itakuwa ndio mwisho wa imani ya wananchi wa nchi hii kwa vyama vya upinzani. Kumbukeni CHADEMA kilivyosaidia watu wengi kuamka na kujua haki zao na kimefanya CCM kujikuta kiko uchi na wizi wa mali za uuma umepungia. CHONDECHONDE kuweni makini. MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU ILINDE CHADEMA.
Dalili zinaonyesha kuwa upo mkakati mkubwa umesukwa kuivuruga CHADEMA kwa mbinu mbalimbali. Kwa mfano ukiangalia kwa sasa mara baada ya CCM kumtosa EL na RA vyombo vya habari vya ITV na Redio one vimegeuza mwelekeo na sasa vinapenyeza kiaina habari mbaya zote zinaelekezwa kwa CHADEMA ili kuifanya CDM isikubalike na wananchi.
Upo mkakati unafanyika ili kuwavunja nguvu wabunge wa CHADEMA wakose kujiamini bungeni unaofanywa na Spika wa bunge na baadhi ya vyombo vya habari ikiwemo Radio one na ITV ili ionekene kuwa wabunge wa CHADEMA hawajui kanuni za bunge mfano Spika Makinda ameripotiwa kuwa Bunge la bajeti la mwaka huu itabidi lianze kwa wabunge kufundishwa kanuni kwani eti wabunge wengi hasa wa upinzani ni wapya hawajui kanuni wanaropoka hovyo bungeni hii si kweli hata kidogo wote tunafuatilia bunge na tuna macho ni ujinga kutufanya hatujui nani hafuati kanuni. Mtaona pia yale yaliozungumzwa wiki iliyopita na Katibu wa Bunge ilikuwa moja ya mbinu za mkakati huo unaoratibiwa kistadi isivyorahisi kugundulika na mwanachi wa kawaida.
Mkakakati mwingine ni kuwatumia wabunge mamluki waliondani ya CHADEMA kuanzisha vurugu kwa kutafuta hoja za kuvuruga chama.
Nilitoa angalizo mapema kuwa CCM sasa watatumia sana wale waandishi mahiri ambao wanaaminiwa na wananchi kuivuruga CHADEMA.
CHADEMA isimame imara kwani ikikubali kuvurugwa kama vyama vingine vilivyosambaratishwa na CCM itakuwa ndio mwisho wa imani ya wananchi wa nchi hii kwa vyama vya upinzani. Kumbukeni CHADEMA kilivyosaidia watu wengi kuamka na kujua haki zao na kimefanya CCM kujikuta kiko uchi na wizi wa mali za uuma umepungia. CHONDECHONDE kuweni makini. MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU ILINDE CHADEMA.