Hali si hali: Magufuli ana uungwaji mkono kiasi gani ndani ya chama?

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,411
114,363
Yawezekana labda ni mimi tu. Labda ni hisia zangu tu. Labda ni jakamoyo langu tu.

Natamani akili yangu iwe inanihadaa [my mind playing tricks on me...shout out to the Geto Boys. RIP Bushwick Bill].

Kinachoendelea sasa hivi nchini kimeanza kunipa wasiwasi.

Huyu mtu aitwaye Musiba naona kaibua mengi. Au labda niseme kasababisha yaibuke mambo ambayo yananipa hofu.

Yote yaliyotokea kabla ya hii kanda ya sauti inayodaiwa kuwa ni ya Nape Nnauye na Abdul Kinana, nilikuwa napuuzia tu. Kusema ukweli zile sauti zinafanana sana na sauti zao.

Wawili hao wanadaiwa kumteta Rais Magufuli.

Hii kanda imenifanya nijiulize mengi sana.

Najiuliza Magufuli anaungwa mkono kiasi gani na viongozi wa juu wa chama chake, wastaafu na waliopo madarakani.

Kama haungwi mkono na wengi, je, hii serikali yake ni dhoofu kiasi gani?

Manake sioni ni kivipi anaweza kuongoza na kufanya kazi kwa ufanisi kama atakuwa anapingwa kwa kiasi kikubwa na walio wengi kwenye uongozi wa chama chake.

Isije kuwa tuna raisi ambaye katengwa wenzake!
 
Kufikiria Kinana anasema mambo yale nimepata mawazo sana.

Pengine ndo maana Rais anakuwa mkali na mkosoaji wa awamu zilizopita akijua kinachoendelea.

Na pengine pia ndo maana wale wapinzani ambao hawakutegemewa kwenda Ccm wakaenda na kupata madaraka!
 
HUYO NDO ACHUMAN NGABANGA!

NA HII NI TAFAKURI BAADA YA HABARI:
Sijui ni utani au vipi, lakini kuna visa vingi vya kuchekesha vinavyowahusu watani zangu wamakonde, na kifuatacho ni kimoja kilichotaka kuhatarisha mbavu zangu ๐Ÿ˜‚ ๐Ÿ˜‚ ๐Ÿ˜‚ !

Jamaa mmoja alipotea porini na baada ya kutangatanga sana humo porini, jioni, akafika kwenye mji wa wamakonde katikati ya pori na baba mwenye nyumba akamkirimu mgeni wake ipasavyo.

Ulipofika muda wa kulala mwenyeji akamuonesha mgeni chumba cha kulala huku akimtandikia huyo mgeni chini, lakini mgeni alipolalamika kwanini anatandikiwa chini mwenyeji wake akamwambia "humu kuna vitanda viwili tu, kimoja nalalia mimi na chemeeji yako na hicho kingine analala mwenyewe Achuman Ngabanga."

Mgeni bado hakuridhika:"Sasa mbona kitanda cha Achuman Ngabanga kikubwa tu na kinatosha kulala watu wawili? naomba tuchangie kitanda na Achumani."

Mwishowe mwenye mji akamruhusu mgeni achangie kitanda na Achuman Ngabanga ambaye mpaka hapo alikuwa hajarudi nyumbani.
Usiku wa manane mgeni akahisi kuna kitu kama mnyama kinambugudhi kitandani na alipoamka akajikuta ana kwa ana na mbwa mkubwa ambaye naye anataka kulala hapo kitandani, na hapo sasa ikawa tena apiga yowe kumuamsha mwenyeji wake na kulalama "huyu mbwa vipi hamjampa mafunzo, mbona anataka kulala na binadamu kitandani?"

Jibu la mwenyeji lilimuacha hoi mgeni:
"HUYO NDO ACHUMAN NGABANGA MWENYEWE AMERUDI, UNAMPUKUCHIA NINI CHACHA? ....ACHA KUMPUKUCHAPUKUCHA ACHUMAN NGABANGA NAYE ALALE" ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚


SASA WAZEE WETU KULIALIA KOTE KWANINI TENA? HUYO NDIE GAMBA WA MAGAMBA MWENYE GAMBA LAKE IN ACTION!

NDUKI ๐Ÿƒโ€โ™‚๏ธ๐Ÿƒโ€โ™‚๏ธ๐Ÿƒโ€โ™‚๏ธ๐Ÿƒโ€โ™‚๏ธ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚!
 
Kufikiria Kinana anasema mambo yale nimepata mawazo sana.

Pengine ndo maana Rais anakuwa mkali na mkosoaji wa awamu zilizopita akijua kinachoendelea.

Na pengine pia ndo maana wale wapinzani ambao hawakutegemewa kwenda Ccm wakaenda na kupata madaraka!

Mimi nimeogopa.
 
Hiyo voice clip kwangu mimi naona ni genuine! Bila kujali sana sauti lakini mtiririko na maudhui ya mazungumzo yananishawishi kusema siyo ya kughushi. Na inalekea ni ''kambi ya Musiba'' umeivujisha! Na imeivujisha kwa sababu ya mkakati maalum. Nashawishika kuhisi siyo hii voice clip tu ila ''kambi ya Musiba'' wana ushahidi ''mnono'' sana utakaowaweka kambi ya Kinana kwenye hali mbaya...... tena kwenye vikao vya CCM na mbele ya ''wazee'' wa CCM! Muda utaamua!
 
Hiyo voice clip kwangu mimi naona ni genuine! Bila kujali sana sauti lakini mtiririko na maudhui ya mazungumzo yananishawishi kusema siyo ya kughushi. Na inalekea ni ''kambi ya Musiba'' umeivujisha! Na imeivujisha kwa sababu ya mkakati maalum. Nashawishika kuhisi siyo hii voice clip tu ila ''kambi ya Musiba'' wana ushahidi ''mnono'' sana utakaowaweka kambi ya Kinana kwenye hali mbaya...... tena kwenye vikao vya CCM na mbele ya ''wazee'' wa CCM! Muda utaamua!

Ina maana mazungumzo ya watu [hususan hao viongozi] yanakuwa tapped?

Kwa upande mwingine, how could Nape and Kinana be that reckless?
 
Musiba ni kipaza sauti kizuri Sana! The man has guts!!

Bashite na Musiba ni watu pekee wenye ujasiri wa kuvikwa mabomu na kwenda kujilipua sehemu yeyote, bila ya kufikiria au kuogopa consequences.. So far, ngoma inawaendelea vizuri.. Tuendelee kuangalia kitakachokuja kujiri baadae.. Ila Ukweli ni kwamba hawa wawili wamejitengenezea maadui wengi ndani ya chama chao kuliko hata nje..
 
Yawezekana labda ni mimi tu. Labda ni hisia zangu tu. Labda ni jakamoyo langu tu.

Natamani akili yangu iwe inanihadaa [my mind playing tricks on me...shout out to the Geto Boys. RIP Bushwick Bill].

Kinachoendelea sasa hivi nchini kimeanza kunipa wasiwasi.

Huyu mtu aitwaye Musiba naona kaibua mengi. Au labda niseme kasababisha yaibuke mambo ambayo yananipa hofu.

Yote yaliyotokea kabla ya hii kanda ya sauti inayodaiwa kuwa ni ya Nape Nnauye na Abdul Kinana, nilikuwa napuuzia tu. Kusema ukweli zile sauti zinafanana sana na sauti zao.

Wawili hao wanadaiwa kumteta Rais Magufuli.

Hii kanda imenifanya nijiulize mengi sana.

Najiuliza Magufuli anaungwa mkono kiasi gani na viongozi wa juu wa chama chake, wastaafu na waliopo madarakani.

Kama haungwi mkono na wengi, je, hii serikali yake ni dhoofu kiasi gani?

Manake sioni ni kivipi anaweza kuongoza na kufanya kazi kwa ufanisi kama atakuwa anapingwa kwa kiasi kikubwa na walio wengi kwenye uongozi wa chama chake.

Isije kuwa tuna raisi ambaye katengwa wenzake!
Utamuelewa tu musiba wewe subiri usiwe na haraka, wananchi tutamuunga mkono JPM hata kama katengwa na CCM
 
Yawezekana labda ni mimi tu. Labda ni hisia zangu tu. Labda ni jakamoyo langu tu.

Natamani akili yangu iwe inanihadaa [my mind playing tricks on me...shout out to the Geto Boys. RIP Bushwick Bill].

Kinachoendelea sasa hivi nchini kimeanza kunipa wasiwasi.

Huyu mtu aitwaye Musiba naona kaibua mengi. Au labda niseme kasababisha yaibuke mambo ambayo yananipa hofu.

Yote yaliyotokea kabla ya hii kanda ya sauti inayodaiwa kuwa ni ya Nape Nnauye na Abdul Kinana, nilikuwa napuuzia tu. Kusema ukweli zile sauti zinafanana sana na sauti zao.

Wawili hao wanadaiwa kumteta Rais Magufuli.

Hii kanda imenifanya nijiulize mengi sana.

Najiuliza Magufuli anaungwa mkono kiasi gani na viongozi wa juu wa chama chake, wastaafu na waliopo madarakani.

Kama haungwi mkono na wengi, je, hii serikali yake ni dhoofu kiasi gani?

Manake sioni ni kivipi anaweza kuongoza na kufanya kazi kwa ufanisi kama atakuwa anapingwa kwa kiasi kikubwa na walio wengi kwenye uongozi wa chama chake.

Isije kuwa tuna raisi ambaye katengwa wenzake!
 
Yawezekana labda ni mimi tu. Labda ni hisia zangu tu. Labda ni jakamoyo langu tu.

Natamani akili yangu iwe inanihadaa [my mind playing tricks on me...shout out to the Geto Boys. RIP Bushwick Bill].

Kinachoendelea sasa hivi nchini kimeanza kunipa wasiwasi.

Huyu mtu aitwaye Musiba naona kaibua mengi. Au labda niseme kasababisha yaibuke mambo ambayo yananipa hofu.

Yote yaliyotokea kabla ya hii kanda ya sauti inayodaiwa kuwa ni ya Nape Nnauye na Abdul Kinana, nilikuwa napuuzia tu. Kusema ukweli zile sauti zinafanana sana na sauti zao.

Wawili hao wanadaiwa kumteta Rais Magufuli.

Hii kanda imenifanya nijiulize mengi sana.

Najiuliza Magufuli anaungwa mkono kiasi gani na viongozi wa juu wa chama chake, wastaafu na waliopo madarakani.

Kama haungwi mkono na wengi, je, hii serikali yake ni dhoofu kiasi gani?

Manake sioni ni kivipi anaweza kuongoza na kufanya kazi kwa ufanisi kama atakuwa anapingwa kwa kiasi kikubwa na walio wengi kwenye uongozi wa chama chake.

Isije kuwa tuna raisi ambaye katengwa wenzake!
Wale wanaosikika kwenye ile audio clip ni wahusika halisi. Sasa mawasiliano ya watu yanafuatiliwa sana, sijui ni kwa vipi wameshindwa kulitambua hili.
 
Back
Top Bottom