Hali ngumu yaja: TANESCO - Press Release

Hali ngumu yaja: TANESCO - Press Release

Mh! unakwenda mbali sana mkuu, lol
Mkuu we run a business and its affects us so much napatwa na hasira sana mambo kama haya tuna-incur huge amount of cost running the equipments especially when they run on generators.
 
Kaka umesikia Japan wametangaza loadshedding for the next 2 years ? ...naomba tukijadili hali ya umeme tuangalie na kasi ya serikali kuijengea uwezo shirika kwa kuongeza vyanzo vya uzalishaji umeme...

Mkuu scenario ya Japan kila mtu anaijua na ina tofauti sana na kwetu. Ya kwao imesababishwa na "Act of GOD", ni ngumu sana kuizuia. Lakini ya kwetu ni uzembe, uzembe, uzembe.... Hata hivyo tusubiri tu baada ya hiyo miaka miwili hao Japan watakuwa na wameshajitosheleza kwa power tena watakuwa na kiwango extra cha umeme, sisi makali ya mgawo yazidi kuongezeka huku tukiimbiwa nyimbo za kisiasa "Mgawo wa Umeme utakuwa historia".
Tusubiri tu, utaona.
 
Apa ni Usanii tu,Hivi hiyo Gesi ya Pan Africa ikitoka kisimani ni direct to the generators? Akuna matanki ya kuifadhi?
Ulaya yote watu wanatumia gesi,ata nyumba aliokuwa anaishi Osama ilikuwa na pipe ya gesi huko pakistan,inakuwagaje wakati wa Repair na inspection kama hizi zetu? Watu awapiki?No kuna kuwa na Matanki ambayo yanaifadhi gesi at least ya kutosha ata mwezi wakati wa services au dharura! Sasa designer wa hii pipeline akuweka reserve tanks? Hii ni hujuma tu na sio lingine

Mkuu kwanza Gesi si mali ya Pan Africa, wao ni waendeshaji tu. Tena wamepewa na mtu mwingine ambaye alipewa aendeshe. Kuna ufisadi mkubwa sana katika uendeshaji wa gesi hii ya Songosongo. Ufisadi huu huenda ni mkubwa kuliko hata ule wa Richmond/Dowans na mingine mingi tuliyowahi kuisikia.
 
Kaka, gesi inahifadhiwa kwenye hivyo visima, na kama umesoma press release mwanzoni watafunga vichache na baadae vyote, hiyo wamepanga wao wenyewe Panafrican ...

Gas inahifadhiwa kisimani ila inasafirishwa kwenye pipes...huko kwa Osama sina shaka serikali inamiliki visima vya gesi na inafanya maintenance shedule kwa wakati...sadly in TZ serikali ina share chache...wameshika mpini na wasipofanya hii maintenance pia ndio kuharibikiwa zaidi ( kiufundi)

Gesi si mali ya Pan Africa. Ni mali ya watanzania. Serikali ilikopa USD320 milioni kutoka world bank kwa ajili ya uendelezaji wa mradi huo. Songas wakapewa tenda ya kujenga mtambo wa Songosongo na baadaye kuuendesha. Songas nao waka-subcontract kwa Pan Africa. Pan Africa wanalipwa pesa ya uendeshaji na matengenezo lakini hawafanyi matengenezo. Hii total shutdown isingekuwepo kama wangekuwa wanafanya periodic maintenance. Kwa kweli ni hadithi kubwa zaidi ya uijuavyo...
 
Hivi haiwekani kutunza hiyo gas kwenye cylinders/tanks kwa ajili ya matumizi wakati wa dharura?

Ninawezekana, lakini lazima tuingie gharama upya.
TATIZO KUBWA HAPA NI SERA jamani naomba mnielewe.
 
Wakati haya yanaendelea na hiyo press release yao, watu bado tupo kwenye mgao wa umeme.

Kwa mfano leo mitaa ya nyumbani kwetu tutakuwa na mgao kuanzia saa 12 jioni hadi saa 5 (lakini most of the time kwenye mgao wa umeme wa usiku, hawa jamaa sijui kama wanajisahau au laa, huwa wanarudisha siku ya pili asubuhi, inshort mgao wa usiku huwa ni usiku mzima, jana mgao ulikuwa mchana.)

I wish Tanesco wangetoa press inayoelezea hali iliyopo sasa, na huo MGAO MKALI wanaodai utakuwa, na hali itakavyokuwa baada ya hayo matengenezo, Maana kwa maisha ya umeme ninayoishi sasa, me naona hamna mabadiliko zaidi ni kuwa sasa mgao utakuwa ni masaa 24.

I am siki endi tayadi withi thisi kantri.
 
Back
Top Bottom