Hali mbaya sana Muhimbili

Sizinga

Platinum Member
Oct 30, 2007
9,101
6,027
Kuna siku nilienda kumetembelea Aunt angu pala Mwaisela..pembeni kulikuwa na binti mmoja aged 20+ anahema vibaya!!
manesi hawashughuliki nae zaidi ya mama mmoja(ndugu yake). badae kidogo yule mama akampa maji ya kunywa...haikupita muda yule binti kakata roho mbele yetu. Nesi kaja kamshika mshipa wa mkono katoka zake tunaona watu wa vitanda wanaanza kukunjakunja na kuufunika mwili.

Bahati nzuru nilikutana na mshkaji angu mmoja palepale anapiga field final yr, akaniambia hii ni hali ya kawaida kwa hapa Muhimbili na akanipa statistics kwamba kwa siku zaidi ya watu 40 wanakufa pale Muhimbili...!!
Sasa kama hii ni data za kweli basi hali ni mbaya sana. Sijaangalia bado Amana, Mwananyamala, Hindumandal...mahospital mengine nk....na nadhani baada ya Babu wa Samunge hope idadi inaweza ikazidi kipimo. Duh maisha hayana thamani tena Bongo hii.
 
Inasikitisha sana, utakuta hao Manesi walikuwa wanampa shinikizo huyo mama ndugu yake Marehemu ili awape kitu kidogo kabla hawajaanza kumhudumia mgonjwa wake..
 
Kuna siku nilienda kumetembelea Aunt angu pala Mwaisela..pembeni kulikuwa na binti mmoja aged 20+ anahema vibaya!!
manesi hawashughuliki nae zaidi ya mama mmoja(ndugu yake). badae kidogo yule mama akampa maji ya kunywa...haikupita muda yule binti kakata roho mbele yetu. Nesi kaja kamshika mshipa wa mkono katoka zake tunaona watu wa vitanda wanaanza kukunjakunja na kuufunika mwili.

Bahati nzuru nilikutana na mshkaji angu mmoja palepale anapiga field final yr, akaniambia hii ni hali ya kawaida kwa hapa Muhimbili na akanipa statistics kwamba kwa siku zaidi ya watu 40 wanakufa pale Muhimbili...!!
Sasa kama hii ni data za kweli basi hali ni mbaya sana. Sijaangalia bado Amana, Mwananyamala, Hindumandal...mahospital mengine nk....na nadhani baada ya Babu wa Samunge hope idadi inaweza ikazidi kipimo. Duh maisha hayana thamani tena Bongo hii.

Hali ni mbaya hospital zote kwa ukweli hatuna serikali inayojali maisha ya Watanzania zaidi ya kutafuna kodi zetu. Wao wakiumwa huwa wanapelekana India, UK na South Africa, tena siku hizi wanapelekana sana South Africa utafikiri wanaenda kutibiwa bure, kumbe wanakwenda kutumbua Kodi za watanzania wanokufia Muhimbili tena na mpaka posho wanalipana wakienda huko. Inasikitisha sana kuona nchi yetu kila idara inakufa kwa Ari ya Mpya Kikwete, Kasi Mpya ya Kikwete na Nguvu Mpya ya Kikwete kuua idara zote kwa upeo wake mdogo. Yeye akili zake amezielekeza kwenye Ndege na ana bahati siku hizi ajali za ndege zimepungua
 
Nipo nchi moja ughaibuni wanaJF, huwezi kuamini nilikutana na dogo mmoja (Girl) katika kupiga piga stori za hapa na pale basi tukawa tunaulizana historia za hapa na pale, kagusia home kwetu ( my family), nikampa habari ya mama yangu kuwa alisha fariki! akashtuka sana. Akasema kwa nini? Alikuwa kazeeka sana au ajali? Nikasema aliugua tu ndo akafariki, alishangaaa sana. Na akasema hapa kwao, ni nadra kukuta mtu kafa kwa sababu ya magonjwa yanayotibika, watu wanakufa sababu ya uzee au ajali ndo vyanzo vya vifo vilivyozoeleka.

Nachotaka kusema hapa wanaJF ni kuwa, bado mifumo yetu ya kiutawala inaabudu mabepari, mabwanyenye na mijitu iliyojilimbikizia mali nyingi harafu ndo imekuwa miungu watu, ndiyo inaamua kwa fulani wale nyama au maharage. Inasikitisha sana binadamu wenzetu wanapofanya mambo ya ajabu pasipo kujua huo uongozi ni fursa ya kufanya mema kwa ajili ya wengi.

We still need to define our own rules and not to keep following other countries rules. How? Nikuwatolea uzembe viongozi wetu, na wakishautema uongozi tuwawajibishe kwa uzembe.
 
Nipo nchi moja ughaibuni wanaJF, huwezi kuamini nilikutana na dogo mmoja (Girl) katika kupiga piga stori za hapa na pale basi tukawa tunaulizana historia za hapa na pale, kagusia home kwetu ( my family), nikampa habari ya mama yangu kuwa alisha fariki! akashtuka sana. Akasema kwa nini? Alikuwa kazeeka sana au ajali? Nikasema aliugua tu ndo akafariki, alishangaaa sana. Na akasema hapa kwao, ni nadra kukuta mtu kafa kwa sababu ya magonjwa yanayotibika, watu wanakufa sababu ya uzee au ajali ndo vyanzo vya vifo vilivyozoeleka.

Nachotaka kusema hapa wanaJF ni kuwa, bado mifumo yetu ya kiutawala inaabudu mabepari, mabwanyenye na mijitu iliyojilimbikizia mali nyingi harafu ndo imekuwa miungu watu, ndiyo inaamua kwa fulani wale nyama au maharage. Inasikitisha sana binadamu wenzetu wanapofanya mambo ya ajabu pasipo kujua huo uongozi ni fursa ya kufanya mema kwa ajili ya wengi.

We still need to define our own rules and not to keep following other countries rules. How? Nikuwatolea uzembe viongozi wetu, na wakishautema uongozi tuwawajibishe kwa uzembe.

Mi niliishi India miaka 4...pale kitaa waliofariki ninaowajua hawazidi 5...naa wote ni vikongwe japo mmoja mwanacollege alipata ajali...hamna magonjwa ya kizembezembe namna hii hapa Bongo, tena siku hizi vibinti 23+ vikishika mimba ya kwanza tu kujifungua salama ni bahati....wengi wanafariki!! dah
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom