1. Vita ya Kagera
2. Mv Bukoba
3. Virusi vya ukimwi
4. Kuanguka kwa Bei ya kahawa
5. Wakimbizi
6. Uhalifu uliokithiri haswa pori la biharamulo
7. Mnyauko wa migomba ambacho ni chakula kikuu
8. Tetemeko la ardhi
9. Vikwazo vya kielimu na kimiundombinu
And the list is endless
Nitajie mkoa hata mmoja Tanzania ambao umepitia yote haya na bado wakazi wake wakaendelea na maisha yao pasipo utegemezi kwa serikali. Kagera is a home of survivals
1. Vita vya kagera vinaizuiaje kagera kuendelea ili hali vita Vimepiganwa miaka 40 iliyopita, isitoshe athari zilikuwa kwa nchi nzima!!
2. Mv Bukoba??... Mv Bukoba imeizuiaje kagera kuendelea ni Sawa na watu wa Dodoma wakwambie ajali ya treni ya Dodoma inazorotesha mkoa kuendelea au kufika mbali zaidi.
3. Kagera sio mkoa unaongoza kwa maambukizi ya ukimwi, mkoa wa njombe zamani iringa Ndio vinara wa maambukizi na wamekuwa wakishikilia hii title kwa muda mrefu Hata kama ukimwi ulitokea huko, hivyo kisingizio hakina maa hiko
4. Sasa kama hii Ndio sababu na mkoa wa Kilimanjaro usingekuwa wa pili kwa ukwasi isitoshe moja ya mazao tegemezi kilimanjaro ni kahawa tokea enzi za ukoloni.
5. Kigoma wasemaje Sasa kama mnalalamikia wakimbizi, isitoshe wakimbizi ni fursa
6. Haina mashiko, uhalifu unafanyika sana Arusha kushinda hapo Kagera
7. Mnyauko haupo kagera tuu Bali hata Kilimanjaro Ila kagera imebaki kuwa maskini
8. Acha utani mkuu kile kitetemeko cha juzi ndicho kifanye kagera kuwa miongoni mwa mikoa 5 maskini zaidi .. umesahau kuwa kabla ya hilo tetemeko kagera ilikuwa ya pili kwa umaskini.
9. Vikwazo vya kielimu kivipi ili hali wahaya wenyeji wa kagera ni moja ya jamii zilizoelimika zaidi TANZANIA!!
Kimsingi hizi sababu zote hazina mashiko uzijumlishe zote kwa pamoja au moja moja hazishawishi kabisa eti mkoa uko karibu na nchi 3 , mvua za kutosha, wasomi kibao ziwa kubwa , mto mkubwa n.k bado uwe miongoni mwa mikoa maskini zaidi TANZANIA...